Sekondari ya Kemebos haitakiwi kuwa inaonekana 10 bora

Chosen man

JF-Expert Member
Dec 30, 2017
520
722
Shule ya sekondari ya Kemebos iliyopo Bukoba mkoani Kagera haipaswi kuwa inaonekaka katika "Top ten schools" kwa sababu kimsingi hakuna shule inayoitwa Kemebos.

Katika shule ya Kaizirege ndipo ambapo wanafunzi wote hufundishwa na wakati wa mitihani ya kitaifa huchukuliwa wanafunzi bora kadhaa kutoka Kaizirege na kuwasajili kama Kemebos kwa lengo la kuuhadaa umma wa Watanzania wasiojua.

Kimsingi hizi shule mbili ni shule moja na walimu ni hao hao na watoto wanasoma pamoja isipokuwa hutenganishwa siku za mitihani pekee.

Matokeo yake utasikia eti Kemebos imekuwa ya kwanza ilhali ni ujanja ujanja mtupu na baadhi ya walimu wanaonekana katika orodha ya walimu bora wa masomo kumbe si kweli. Matokeo halisi yanapaswa kuchanganywa ya KAIZIREGE na KEMEBOS pamoja ndio uhalisia utaonekana.

Nahitimisha kwa kusema "HAKUNA SHULE INAITWA KEMEBOS"
 
Unaweza kuwa na hoja lakini uwasilishaji wa ovyo. Kusema Hakuna shule inaitwa Kemebos ni uongo maana jina Hilo ni la shule yenye usajili wa NECTA.

Labda utufafanulie huo utaratibu wa kiholela wa kuchukua wanafunzi Bora wa shule Fulani na kuwaweka pamoja Kwa kuwapa jina lisilosajiliwa la Kemebos unawezekanaje??
 
Shule ya sekondari ya Kemebos iliyopo Bukoba mkoani Kagera haipaswi kuwa inaonekaka katika "Top ten schools" kwa sababu kimsingi hakuna shule inayoitwa Kemebos.

Katika shule ya Kaizirege ndipo ambapo wanafunzi wote hufundishwa na wakati wa mitihani ya kitaifa huchukuliwa wanafunzi bora kadhaa kutoka Kaizirege na kuwasajili kama Kemebos kwa lengo la kuuhadaa umma wa Watanzania wasiojua.

Kimsingi hizi shule mbili ni shule moja na walimu ni hao hao na watoto wanasoma pamoja isipokuwa hutenganishwa siku za mitihani pekee.

Matokeo yake utasikia eti Kemebos imekuwa ya kwanza ilhali ni ujanja ujanja mtupu na baadhi ya walimu wanaonekana katika orodha ya walimu bora wa masomo kumbe si kweli. Matokeo halisi yanapaswa kuchanganywa ya KAIZIREGE na KEMEBOS pamoja ndio uhalisia utaonekana.

Nahitimisha kwa kusema "HAKUNA SHULE INAITWA KEMEBOS"
Huu ujanja upo kweli, nilikuja kupewa matokeo ya mtoto wangu naambiwa inabidi ahamishiwe shule nyingine ya vilaza ambayo ni ya kwao,ili amalizie form 4 kule na ile ya pale alipokuwa anasoma hawamhitaji kwani ataharibu matokeo, nilimuhamishia faster shule nyingine kabisa isio ya kwao, ila kibaya ilibidi arudie form 3, thanks God sasa yuko University, na wale walioambiwa wabaki ile shule wenye akili anawarudi kama wamesimama, hizi shule za private ni majanga sana...
 
Unaweza kuwa na hoja lakini uwasilishaji wa ovyo. Kusema Hakuna shule inaitwa Kemebos ni uongo maana jina Hilo ni la shule yenye usajili wa NECTA.
Labda utufafanulie huo utaratibu wa kiholela wa kuchukua wanafunzi Bora wa shule Fulani na kuwaweka pamoja Kwa kuwapa jina lisilosajiliwa la Kemebos unawezekanaje??
Labda we hukai Tanzania mbona jambo hili si shule hiyo tu janja janja hizo maeneo mengi tu zipo sana

Au ni mnufaika wa shule hizo pia??
 
290853032_1628244350909346_6840046045118563327_n.jpg
 
Labda ungesema wanafanyiwa/iba mitihani ungekuwa na hoja,kigezo cha shule kutambulika ni ule usajili tu.
Kitu kingine ni kushiriki mitihani ya taifa kama ilivyopangwa bila kuvunja sheria.
Hilo suala la wanafunzi kufundishwa wapi..na nani... na 2anafanyia wapi mitihani..hiyo ni mikakati ya uongozi wa shule.lipo ndani ya uwezo wao,serikali haina ubavu wa kuingilia hasa kwakuwa hakuna sababu ya msingi.
 
Shule ya sekondari ya Kemebos iliyopo Bukoba mkoani Kagera haipaswi kuwa inaonekaka katika "Top ten schools" kwa sababu kimsingi hakuna shule inayoitwa Kemebos.

Katika shule ya Kaizirege ndipo ambapo wanafunzi wote hufundishwa na wakati wa mitihani ya kitaifa huchukuliwa wanafunzi bora kadhaa kutoka Kaizirege na kuwasajili kama Kemebos kwa lengo la kuuhadaa umma wa Watanzania wasiojua.

Kimsingi hizi shule mbili ni shule moja na walimu ni hao hao na watoto wanasoma pamoja isipokuwa hutenganishwa siku za mitihani pekee.

Matokeo yake utasikia eti Kemebos imekuwa ya kwanza ilhali ni ujanja ujanja mtupu na baadhi ya walimu wanaonekana katika orodha ya walimu bora wa masomo kumbe si kweli. Matokeo halisi yanapaswa kuchanganywa ya KAIZIREGE na KEMEBOS pamoja ndio uhalisia utaonekana.

Nahitimisha kwa kusema "HAKUNA SHULE INAITWA KEMEBOS"
Tatizo ni Serikali ilizuia mchujo hivyo ni kama namna ya kuchuja wanafunzi na kupata wanafunzi bora wanaowakilisha kemebos .
 
Imesajiliwa lakini haina wanafunzi wanaosoma hapo kama wanafunzi, wote wanasoma Kaizirege
Kumbe shule yenye jina hilo ipo, sasa hoja yako ni ipi!

Huo ni utaratibu waliojiwekea wenyewe na serikali sidhani kama itaingilia hapo kwa sababu hakuna hoja ya maana.
 
Shule ya sekondari ya Kemebos iliyopo Bukoba mkoani Kagera haipaswi kuwa inaonekaka katika "Top ten schools" kwa sababu kimsingi hakuna shule inayoitwa Kemebos.

Katika shule ya Kaizirege ndipo ambapo wanafunzi wote hufundishwa na wakati wa mitihani ya kitaifa huchukuliwa wanafunzi bora kadhaa kutoka Kaizirege na kuwasajili kama Kemebos kwa lengo la kuuhadaa umma wa Watanzania wasiojua.

Kimsingi hizi shule mbili ni shule moja na walimu ni hao hao na watoto wanasoma pamoja isipokuwa hutenganishwa siku za mitihani pekee.

Matokeo yake utasikia eti Kemebos imekuwa ya kwanza ilhali ni ujanja ujanja mtupu na baadhi ya walimu wanaonekana katika orodha ya walimu bora wa masomo kumbe si kweli. Matokeo halisi yanapaswa kuchanganywa ya KAIZIREGE na KEMEBOS pamoja ndio uhalisia utaonekana.

Nahitimisha kwa kusema "HAKUNA SHULE INAITWA KEMEBOS"
Unafikiri ni kwanini wanafanya hivyo
 
Back
Top Bottom