Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,927
Kulikuwa na utata mwanzoni - na kwa baadhi ya watu - juu ya msimamo wa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) ambaye pia ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Bw. Seif Sherrif Hamad hususan suala la kile kinachojulikana kama "Muungano wa Mkataba". Katika clip hii (ambayo labda tayari imeshaonekana) Bw. Seif ametangaza bila ya utata kuwa yeye ni "Muumini wa Muungano wa Mkataba".
Kuwa muumini wa Muungano wa "Mkataba" ni kutokuwa Muumini wa Muungano wa sasa kwani katika Muungano wa Mkataba unaopendekezwa na waumini wake Zanzibar inarudi na kuwa nchi huru ikiwa na hakimiya kamili (full sovereignty) na inahusiana na Tanganyika kwenye mambo kadhaa ya kimkataba badala ya ilivyo sasa ambapo nchi mbili ziliamua kusalimisha hakimiya zao kwenye Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kuwa muumini wa Muungano wa namna hii ni kuwa muumini wa kupigania uhuru wa Zanzibar kutoka kwenye Muungano wa sasa; lakini zaidi ni kuwa muumini kuwa Muungano wa sasa ni wa kikoloni ambapo Tanganyika inainyonya Zanzibar. Lakini zaidi ni kuamini kuwa Muungano wa sasa siyo halali.Sasa kama Seif anaamini yote mawili - kwamba Tanganyika inaikalia Zanzibar kama Koloni na kuwa Muungano wa sasa siyo halali basi yampata aendelee mbele kwenye hitimisho la kimantiki - kujiuzulu Umakamu na kukiondoa CUF kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).
Afanye hivi ili chama chake kifanye harakati ya kuiondoa Zanzibar kutoka kwenye Muungano na Wazanzibar wakikubali kwenye kura ya maoni yao basi CUF ikishika madaraka Zanzibar ifikirie namba ya kuingia kwenye "muungano wa Mkataba' na nchi yoyote nyingine (si lazima iwe Tanganyika). Kwa kufanya hivi Seif ataonesha mfano kwa viongozi wengine wote wa Zanzibar wenye kuamini Muungano wa Mkataba kutoka kwenye nafasi zao na pia wale Wazanzibari walioko kwenye huduma ya Muungano wa sasa watoke. Lakini zaidi sana Seif akiamua kujiuzulu nafasi hizo wabunge wake wa CUF walioko kwenye Bunge la Muungano nao waamue kufuata mkumbo ili harakati za Uhuru wa Zanzibar (secession) zianze rasmi zikiongozwa na Seif.
Last edited by a moderator: