Science kweli ni ngumu au hapa kwetu tu!!!

Sep 14, 2011
36
5
Hili swala la watanzania wengi kukimbia masomo ya science inamaanisha wengi hatujiwezi kuyamudu ni magumu sana au ni mfumo wa Mitaala yetu ya Tanzania ndiyo inasababisha!

Kwa hili kama mzalendo wa nchi unadhani nini kinasababisha wengi tuyakimbie!
 
We kama umeyakimbia ni wewe 2,ucdhan kila m2 ni kilaza mwenzio bwana..
 
Mi nipo Science, Unapozungumzia sayansi,inamaana kuwa ni vitendo zaidi na si theory sana.. Ndio unatakiw kuanza na theory kidogo baadae vitendo sana. Sasa kwa Tanzania hatuna huwezo wa kufanya vitendo yaani practical kutokana na vifaa kutokuwepo au pungufu.. Sasa hii itamfanya mwanafunz kuona kuwa haelewi kinachoendelea na kuchukua masomo hayo ni magumu.. Tukiachana na vifaa pia WALIMU wa sayansi ni wachache na kati ya hao wachache wapo ambao wapo SHALLOW,hawayawez mambo anaingia darasani ila anachofundisha hakielewek.. Sasa unategemea Mwanafunzi atasema masomo ni marahisi..
 
Hili swala la watanzania wengi kukimbia masomo ya science inamaanisha wengi hatujiwezi kuyamudu ni magumu sana au ni mfumo wa Mitaala yetu ya Tanzania ndiyo inasababisha!

Kwa hili kama mzalendo wa nchi unadhani nini kinasababisha wengi tuyakimbie!

kaka acha kukalili kuwa asiyesoma sayansi kuwa amekimbia au yeye ni kilaza,kwa mifano midogo tu chukua record ya baadhi ya waliokuwa wanakukimbiza shule wote wameenda sayansi???.....watu wameacha kwa sababu kibongo bongo haina ishu zaidi ya kuwa tuta chuo ila angalia wanao piga masomo ya biashara wanakula bata tu sasa wewe kama unadhani kusoma sayansi ni uwezo baki na hiyo ideology.
 
Mi nipo Science, Unapozungumzia sayansi,inamaana kuwa ni vitendo zaidi na si theory sana.. Ndio unatakiw kuanza na theory kidogo baadae vitendo sana. Sasa kwa Tanzania hatuna huwezo wa kufanya vitendo yaani practical kutokana na vifaa kutokuwepo au pungufu.. Sasa hii itamfanya mwanafunz kuona kuwa haelewi kinachoendelea na kuchukua masomo hayo ni magumu.. Tukiachana na vifaa pia WALIMU wa sayansi ni wachache na kati ya hao wachache wapo ambao wapo SHALLOW,hawayawez mambo anaingia darasani ila anachofundisha hakielewek.. Sasa unategemea Mwanafunzi atasema masomo ni marahisi..
kaka wewe ni mmoja kati waloelewa nini kinatakiwa kizungumziwe,Hamy D bado hujafaham unachotakiwa ukifanye humu ndani,Ndetichia upo sawa kaka hiyo nayo sababu mojawapo,nimekupata Bujibuji tupo pamoja kaka!
 
We kama umeyakimbia ni wewe 2,ucdhan kila m2 ni kilaza mwenzio bwana..
Kaka ningesema watu wengi wanayakimbia ningemaanisha mimi si mTanzania,lakini hiyo lugha niliyotumia ni hekima kuonyesha najigamba kuwa mTz,upo kaka!
 
Kwa Tanzania application ya sayansi ndogo sana sababu theory sana kuliko practical ndiyo maana wanasayansi wa Bongo nao wapo barabarani kusaka ajira sasa je kulikuwa na aja mwanasayansi kukosa cha kufanya?Tafakali
 
theory ndogo kuliko practical=tuimalishe practical kwa kununua vifaa ikiwezekana tutengeneze hapa kwetu, pli walimu wengi wa science hawajaandaliwa vya kutoshA, na wenye uwezo wa science ndiyo wanakimbia science mfano mh. bilali G
 
kwanza kahistoria nako kanachangia yote hayo ila tukubali wabongo wengi ni vilaza sana hafu ukijumlisha na system iliyopo ya kukariri ndo kabsaaaaaaaaa unaua bendi
c unajua science hasa hesabu huwezi karirri kabla hujaelewa?
 
Kiukweli iwe sayansi au arts inaweza ikafanywa kuwa ngumu au kuwa rahisi hasa katika nyanja ya elimu.Hapa Tanganyika na Afrika kwa ujumla maandalizi yamasomo nimabaya.Ebu angalia mtoto anafika darasa la saba anafanya masomo kwa theories tu na akibatika kwenda sekondari anaanza upya na masomo ya science mengi anasoma theories kwani hamna labaratory.Kidato cha nne ataambiwa practical pengine alternative.Akienda Advance angalau kidogo sasa niambie hapo mtu ataifauruje vzr sayansi au kuipenda.Mahandalizi ndo tatizo,nadhani kuanzia primary to sec mtoto angekuwa anapata mafunzo kwa practical tungekuwa mbali maana ata walimu wengekuwepo.Angalia ata hili sasa mtu mwenye E sayansi anaenda kusoma shahada aje afundishe Adv or O level.
Kuna umuhimu wakufanya reforms kubwa kwenye mfumo wa elimu ila sijui nani tumfunge kengere.
 
Sidhani kama ni sahihi kufikiria kuna masomo rahisi. Ila sayansi inapoteza mvuto kwa watu wengi wanaosoma pengine kwa sababu ya msingi mbovu wa ufundishaji wa masomo yake na hasa hisabati,pamoja na ukosefu wa kazi kwa sababu ya ukuaji mdogo wa viwanda na utafiti tanzania. Kwa mtazamo wangu, jinsi mambo yanavyobadilika kutakuwa na mahitaji makubwa ya wataalamu wanaofanya kazi zenye misingi ya science. Tusiangalie future kwa kufikiri matatizo yaliyopo ni ya kudumu na hayatakuwa na mabadiliko.
 
Jamani,masomo ya sayansi ni magumu ukilinganisha na ya arts,hebu linganisha physics na kiswahili au geography,vp kuhusu maths na history? Au chemistry na language?kwa asili yake tu masomo ya sayansi si marahisi yanahitaji commitment ya hali ya juu,sasa tatizo linakuja why should i take science and not arts subjects?mtu wa arts anasoma kwa raha na maisha yake yanakuwa bomba,maana atasoma let say course za administration kwa miaka mitatu na atakuwa bosi wa engineer aliyekomaa na pcm na 4 years kwa bsc.engineering,mwalimu wa sayansi kakomaa na pcb au pcm anakutana mwalimu mwingine staff moja kasoma hkl wanalipwa kipato sawa,huyu wa sayansi unakuta anafundisha vipindi 32 kwa wiki maana wapo wachache na masomo yana vipindi vingi,wakati huyu wa arts anakuwa na vipindi 4 kwa wiki maana wapo wengi na masomo ya arts mengi yana vipindi vichache tu,at the same time accademic wako na headmaster wako ni arts,so wanakupngia kazi,kwa hiyo nisome sayansi ili iwe nn?
 
Acha kujidanganya. Kuhusu ajira private ni tofauti sana. Science kama nyanga zinaenda mshahara ni mnene sana
 
Back
Top Bottom