Saudia yapeleka maski zenye virusi vya corona nchini Yemen

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,990
17,879
Saudia yapeleka maski zenye virusi vya corona nchini Yemen
Apr 02, 2020 02:27 UTC
Waziri wa Habari wa Yemen amesema kuna uwezekano mkubwa kwamba ndege za kivita za muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia zimedondosha maski (barakoa) zenye virusi vya corona katika miji mbalimbali ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu.
Shirika la habari la Middle East Monitor limemnukuu Dhaifullah al-Shami, Waziri wa Habari wa Yemen akitoa tangazo hilo ambapo pia ameviomba vyombo vya habari kuwatahadharisha wananchi wa Yemen dhidi ya kugusa au kuvaa maski hizo zinazodondoshwa na ndege za kivita za muungano vamizi katika mji mkuu Sana'a na miji mingine.
Ameashiria kuhusu taathira hasi za uvamizi wa kijeshi nchini humo ulioifanya Yemen ikumbwe na mgogoro mkubwa zaidi wa kibinadamu duniani na kueleza bayana kuwa, "tumepigwa na butwaa kuona vikosi vya muungano (vamizi) wa kijeshi vikisambaza maski katika maeneo yote ya mji mkuu Sana'a na mikoa kadhaa ya nchi hii."
Waziri wa Habari wa Yemen amesema kuwa, nchi hiyo haijarekodi kesi yoyote ya ugonjwa wa Covid-19 ambao umeshaua makumi ya maelfu ya watu katika nchi mbalimbali duniani na kusisitiza kuwa, muungano huo vamizi utabeba dhima ya mripuko wowote wa corona nchini humo.
Hii ni katika hali ambayo, hapo jana, duru za habari ziliripoti kuwa, muungano huo vamizi unaoongozwa na Saudia katika vita vya Yemen umekiuka mara 108 makubaliano ya usitishaji vita katika mji wa al-Hudaydah katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita.
Bandari ya al-Hudaydah nchini Yemen ndio njia kuu ya upelekaji misaada ya kibinadamu katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo masikini iliyoharibiwa vibaya na vita pamoja na mashambulio ya anga ya jeshi vamizi la Saudi Arabia na washirika wake tokea mwaka 2015

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Saudi washushieni na kitimoto .nyama tamu iio

Sent from my SM-A105G using Tapatalk
 
Kuna mambo yananichamgamya sana hivi hawa virus wanaweza kubaki hai kwenye sehemu walipogusa kwa muda gani ndo waweze kuendelea kubaki kwenye hizo mask?
Dk 10-12 tu hivi. Hizo ni propaganda za redio mbau tu.
 
Kuna mambo yananichamgamya sana hivi hawa virus wanaweza kubaki hai kwenye sehemu walipogusa kwa muda gani ndo waweze kuendelea kubaki kwenye hizo mask?
Tizama hapa
Screenshot_20200329-133607_WhatsApp~2.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yemen bado hawana mgonjwa wa corona sasa mask za nini?
Kwa sasa kila mbaya wako atakusaidia kujikinga na kusambaa na hili gonjwa
Wayemen wengi sana wapo Saudia na wameoana na kuzaana miaka na miaka
Inawezekana wanawapa kwa wao kuogopa tu
Maana hata USA ameomba poo kwa hasimu wake China
Ule usemi wa muombee njaa adui yako unabadilika kwa kasi sana sasa

Kwa sasa hata neno Terrorist linabadika maana yake taratibu na tutaheshimiana tu
Dunia kamwe haitakuwa kama zamani
Adjustments.jpg



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Saudia yapeleka maski zenye virusi vya corona nchini Yemen
Apr 02, 2020 02:27 UTC
Waziri wa Habari wa Yemen amesema kuna uwezekano mkubwa kwamba ndege za kivita za muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia zimedondosha maski (barakoa) zenye virusi vya corona katika miji mbalimbali ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu.
Shirika la habari la Middle East Monitor limemnukuu Dhaifullah al-Shami, Waziri wa Habari wa Yemen akitoa tangazo hilo ambapo pia ameviomba vyombo vya habari kuwatahadharisha wananchi wa Yemen dhidi ya kugusa au kuvaa maski hizo zinazodondoshwa na ndege za kivita za muungano vamizi katika mji mkuu Sana'a na miji mingine.
Ameashiria kuhusu taathira hasi za uvamizi wa kijeshi nchini humo ulioifanya Yemen ikumbwe na mgogoro mkubwa zaidi wa kibinadamu duniani na kueleza bayana kuwa, "tumepigwa na butwaa kuona vikosi vya muungano (vamizi) wa kijeshi vikisambaza maski katika maeneo yote ya mji mkuu Sana'a na mikoa kadhaa ya nchi hii."
Waziri wa Habari wa Yemen amesema kuwa, nchi hiyo haijarekodi kesi yoyote ya ugonjwa wa Covid-19 ambao umeshaua makumi ya maelfu ya watu katika nchi mbalimbali duniani na kusisitiza kuwa, muungano huo vamizi utabeba dhima ya mripuko wowote wa corona nchini humo.
Hii ni katika hali ambayo, hapo jana, duru za habari ziliripoti kuwa, muungano huo vamizi unaoongozwa na Saudia katika vita vya Yemen umekiuka mara 108 makubaliano ya usitishaji vita katika mji wa al-Hudaydah katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita.
Bandari ya al-Hudaydah nchini Yemen ndio njia kuu ya upelekaji misaada ya kibinadamu katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo masikini iliyoharibiwa vibaya na vita pamoja na mashambulio ya anga ya jeshi vamizi la Saudi Arabia na washirika wake tokea mwaka 2015

Sent using Jamii Forums mobile app
Mashia kwa uongo na uzushi hata shetani anajifunza kwenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom