Saudi investors eye Tanzanian farmland

Alpha

JF-Expert Member
Aug 30, 2007
662
251
Saudi investors eye Tanzanian farmland

Saudi investors have asked Tanzania if they can lease 500,000 hectares of farmland mainly for rice and wheat farming as part of a plan to secure food supplies for the desert kingdom, officials said.

Senior officials from the Saudi capital's chamber of commerce made the request on the sidelines of a meeting with visiting Tanzanian President Jakaya Kikwete.

'Tanzania is ready to do business with you ... There is 100 million acres (40.5 million hectares) of good arable land,' Kikwete told Saudi businessmen.

Samir Ali Kabbani, head of the chamber's agriculture committee, said: 'We had very positive feedback.'

'He (Kikwete) told us that Tanzanian authorities can lease us plots each of which covers up to 10,000 hectares for a 99-year period,' he added.

The Saudi government has joined private operators to invest in farm projects abroad after a long and costly food sufficiency plan threatened to deplete the desert kingdom's water supplies.

Saudi businessmen and officials will visit Tanzania in the next few weeks.

'They can lease the land from the government,' January Makamba, an aide to President Kikwete, said.

“But we have to make sure we don't end up in a situation similar to that of Nigeria: Huge oil reserves but long queues in front of petrol stations,' Makamba said.

Saudi officials are particularly interested in Tanzania because of its geographic proximity, political stability and the availability of water resources and farmland.

Several Saudi firms have already started investing in agricultural projects from Indonesia to Ethiopia.

Indonesia said in August that Saudi BinLadin Group would invest $4.3 billion on 500,000 hectares for rice farming.

Saudi Arabia's annual wheat needs are estimated at about 2.5 million tonnes and it imported a little over 1 million tonnes of rice in 2008, according to the US Department of Agriculture.
– Reuters

Trade Arabia - Middle East & GCC Business Information | Trade News Portal
 
Saudi investors eye Tanzanian farmland
Riyadh: 3 hours and 16 minutes ago

Saudi investors have asked Tanzania if they can lease 500,000 hectares of farmland mainly for rice and wheat farming as part of a plan to secure food supplies for the desert kingdom, officials said.
[/url]

Hivi Tanzania imejitoshereza kichakula? Kwanini usiwempango wa kuongeza food supply Tanzania
 
Since all Institutions zimeliwa na kufilisiwa..sasa remains the last of tanzanias treasures , the land! Ule usemi nchi imeuzwa unakaribia kuwa reality..i wonder what will happen to those living on those agriculturaly productive 500,000 hectares??
 
Hivi Tanzania imejitoshereza kichakula? Kwanini usiwempango wa kuongeza food supply Tanzania
Kujitosheleza kunashindikana kwa sisi wenyewe kushindwa kutumia ardhi nzuri, mabonde na mito kulima na kupata ziada. sasa kuna ubaya gani kama ardhi iliyopo ambayo hatuitumii tukaikodosha kwa watu ambao wana uwezo wa kuitumia vyema, wakafanya umwagiliaji , wakatumia mashine za kisasa kuendeleza kilimo bora na wakavuna chakula kingi kwa ajili yao na pengine kutugaia sisi wenyewe tunaoshindwa kulima? Mpunga Bonde la Mto Rufiji, Mpunga Kilombero, Mpunga hata kule Mwanza pembezoni mwa ziwa unalimika vizuri tu. Tumefikia wapi?
 
Kujitosheleza kunashindikana kwa sisi wenyewe kushindwa kutumia ardhi nzuri, mabonde na mito kulima na kupata ziada. sasa kuna ubaya gani kama ardhi iliyopo ambayo hatuitumii tukaikodosha kwa watu ambao wana uwezo wa kuitumia vyema, wakafanya umwagiliaji , wakatumia mashine za kisasa kuendeleza kilimo bora na wakavuna chakula kingi kwa ajili yao na pengine kutugaia sisi wenyewe tunaoshindwa kulima? Mpunga Bonde la Mto Rufiji, Mpunga Kilombero, Mpunga hata kule Mwanza pembezoni mwa ziwa unalimika vizuri tu. Tumefikia wapi?

I like the "kutugaiya" part!
Mtegemea cha ndugu hufa maskini.Tukiwa na mawazo kuwa ngoja tuwape ili nao watugaiye basi hatufiki mbali.
Mkuu,
Watanzania hawajashindwa kulima bali wanachohitaji ni support ya kuweza kulima kisasa kwa maana ya pembejeo, matrekta, mipango ya umwagiliaji maana kutegemea mvua nako kunatuangusha, miundombinu ili mazao yao yaweze kufika kwenye masoko n.k.Na serikali inaweza kufanikisha hili kama kutakuwepo na matumizi mazuri ya mapato ya taifa.Kutafuta watu waje walime vyao tu..sijui! Ningeelewa kama wangekuja kuwekeza wakalima ili tuweze kuwa na mazao ya chakula ya kutosha ili tuepukane na aibu ya njaa inayolikumba taifa mara kwa mara.
 
I like the "kutugaiya" part!
Mtegemea cha ndugu hufa maskini.Tukiwa na mawazo kuwa ngoja tuwape ili nao watugaiye basi hatufiki mbali.
Mkuu,
Watanzania hawajashindwa kulima bali wanachohitaji ni support ya kuweza kulima kisasa kwa maana ya pembejeo, matrekta, mipango ya umwagiliaji maana kutegemea mvua nako kunatuangusha, miundombinu ili mazao yao yaweze kufika kwenye masoko n.k.Na serikali inaweza kufanikisha hili kama kutakuwepo na matumizi mazuri ya mapato ya taifa.Kutafuta watu waje walime vyao tu..sijui! Ningeelewa kama wangekuja kuwekeza wakalima ili tuweze kuwa na mazao ya chakula ya kutosha ili tuepukane na aibu ya njaa inayolikumba taifa mara kwa mara.
Dada angu umo katika ndoto hapo. Wazee wetu wakulima katika hayo mabonde wanachoweza ni kulima sana sana ekari mbili tena wanapatishwa shida na magugu, matokeo yake wanavuna vijipeto tu vya mpunga ambavyo hata havikidhi haja ya familia. Kuna ubaya gani kuwakodisha ardhi watu ambao wataitumia neema hiyo ya mwenyezi-mungu (ardhi) ilivyo na kuzalisha chakula cha ziada kwa ajili ya Binaadamu.
 
May be JK analengo la maana kwenye hili, JK had never proposed anything which make sense. May be this will be tie braker!

Waarabu wanataka kulima, i wanna see that.
 
Hecta 500,000 is a huge land...that is over 1.2 mil acres kwa sie tuliozea kupima miguu 70 kwa 70..!!

Mimi naunga mkono hili wazo...tunahitaji wawekezaji kama hawa kuja kutuamsha Watanzania. Ni jukumu letu kuhakikisha wakija "TUNAWATUMIA VEMA" na sio wao wanatutumia sisi...mradi kama huu ukiwekwa vizuri utainua sana hali ya maisha ya Watanzania vijijini. Zitajengwa barabara, reli, zahanati, mashule, police posts n.k

Enyi Wazalendo mliopo kwenye idara mbali mbali zinazohusika jifunzeni makosa yaliyofanyika kwenye mikataba ya madini...Hecta nusu milioni kwa miaka 99 sio kitu kidogo. Ikiwezekana mradi huu umalize kabisa tatizo la chakula Tanzania japo kwa miaka 99..!!
 
Yebo Yebo,
Kuna wakati nilikwenda Guatemala ambako Marekani imechukua mashamba makubwa tu ya ndizi, Chiquita, Dole, n.k ambazo unakuta zimejaa kwenye super markets zao. Fikra zangu wakati huo ni kwamba hawa wakulima wa Guatemala must be rich or well to do kwa kuwa wana soko kubwa tu la ndizi Marekani. I was wrong. Kilichotokea ni kwamba hayo mashamba yanamilikiwa na kampuni za Kimarekani ( kama ambavyo Wasaudi watamiliki mashamba tutakayowaruhusu ku lease kwa miaka 99) na Watanzania tutabaki kuwa ma campesino tu au wapagazi wa kuchota maji katika mashamba hayo.Huu si uwekezaji utakaomsaidia Mtanzania kujikwamua na kujiongezea kipato chake. Hatutafaidika na soko la mchele au ngano Saudia kwa sababu wanaomiliki mashamba si Watanzania. Are you getting my drift? Anayetajirika na ndizi za Guatemala si Mguatemala. Ni corporate America. We are going to find ourselves in the same situation.
 
Dada angu umo katika ndoto hapo. Wazee wetu wakulima katika hayo mabonde wanachoweza ni kulima sana sana ekari mbili tena wanapatishwa shida na magugu, matokeo yake wanavuna vijipeto tu vya mpunga ambavyo hata havikidhi haja ya familia. Kuna ubaya gani kuwakodisha ardhi watu ambao wataitumia neema hiyo ya mwenyezi-mungu (ardhi) ilivyo na kuzalisha chakula cha ziada kwa ajili ya Binaadamu.

Mkuu,
SIJUI KAMA umeelewa point yangu!
Hebu isome tena vizuri halafu ongezea na ile ya Jasusi utaona nilichukuwa namaanisha.
 
Yebo Yebo,
Kuna wakati nilikwenda Guatemala ambako Marekani imechukua mashamba makubwa tu ya ndizi, Chiquita, Dole, n.k ambazo unakuta zimejaa kwenye super markets zao. Fikra zangu wakati huo ni kwamba hawa wakulima wa Guatemala must be rich or well to do kwa kuwa wana soko kubwa tu la ndizi Marekani. I was wrong. Kilichotokea ni kwamba hayo mashamba yanamilikiwa na kampuni za Kimarekani ( kama ambavyo Wasaudi watamiliki mashamba tutakayowaruhusu ku lease kwa miaka 99) na Watanzania tutabaki kuwa ma campesino tu au wapagazi wa kuchota maji katika mashamba hayo.Huu si uwekezaji utakaomsaidia Mtanzania kujikwamua na kujiongezea kipato chake. Hatutafaidika na soko la mchele au ngano Saudia kwa sababu wanaomiliki mashamba si Watanzania. Are you getting my drift? Anayetajirika na ndizi za Guatemala si Mguatemala. Ni corporate America. We are going to find ourselves in the same situation.

Jasusi,
1.Ni kweli unayosema............unajua nini........watasema itaongeza ajira (mambo ya sera) na kodi kwa serikali.......
2.10%.........i.e.pesa ya uchaguzi ati.....

On the other hand however....hebu tuangalie pia mashamba ya maua kule Kenya......similar thing is happening there, kwani wamiliki wa yale mashamba ni kampuni za Ulaya.....how does Kenya benefit?.......how do we position ourselves ili tu-benefit............Serikali inahitaji wawe wawazi kwenye haya mambo ili kupata mawazo ya wananchi.........
 
CUF wanarudisha waarabu ,ha ha ha ,ama kweli ukimuelekezea mwenzio kidole kimoja vyengine vinne vinaluelekea mwenyeo ,ila endeleeni na leteni tafasiri nyingine Saudi Bin Laden ni ndugu na yule Bin Laden orijino asieonekana invisible Bin Laden.

Ila wamesema wanakodi eneo kwa ajili yao na si Tanzania ,nafikiri hapo itabidi muelewane kikweli sio watalima kwa ajili ya Tanzania ,wao watalipia hiyo miaka 99 ,aidha wafanyakazi watakuwa na hiari yao kama watawachukua wazalendo au watawaagizia kutoka vietnam na ufilipino ,vile vile wana uwezo wa kuzungurusha ukuta kushinda ule uliozungushwa na wayahudi ,hivyo kuingia ndani kwa kitambulisho ,wao wanaweka geti tu na inakuwa njia ya kuingia ni kutumia geti hakuna kwengine ,ila kama wazalendo wataajiriwa basi nahakikisha baada ya mwaka tu kila mmoja ana gari si ya kawaida maana wao wanataka kuona kile wanachokiekeza kina shinda wengine ni watu wa mashindano hivyo hata wafanyakazi wao watakuwa waringa kwani bila ya shaka yeyote mahitaji ya lazima na ya kisasa yatapatikana katika maeneo yao na mishahara nje nje labda wafuasi wa Sultani CCM waweke uchoyo na kuamua wasiwalipe wafanyakazi kiasi kikubwa cha fedha.
 
Mtazamo wangu , swala hili liamuliwe na wananchi. Siyo serikali, ipigwe kura ya maonini, ni suala nyeti sana. Tumeona migodi iliyouzwa na madhara yake, mashirika ya umma,[ nasikia Kiwira Coal mines na Mgololo paper company mashine zinauzwa as scrapes ]. Sasa tukiuza [ wenyewe wanaita kukodi] ardhi kwa miaka 99, that is a lifetime !!Wakulima wataenda wapi ? tutafaidika na nini? Watalima nini? Tunaogopa EAC kwa ajili ya ardhi, sasa inakuwaje leo tunawapa watu wa mashariki ya kati? Maji wanayosema mengi yako wapi ?Mbona Mbarali watu wanagombania maji na mwekezaji aliyepewa Kapunga Rice farm? Maji yapo mengi lakini pia tujue kwamba yatahamishwa kutoka eneo moja kwenda lingine, eneo lile la zamani itakuwaje? Hili swala lina kila dalili ya manyanyaso sana kwa wananchi.
 
Watanzania wabishi. Foreign capital ni muhimu kwa nchi kama Tanzania. Kama waSaudi wanaleta capital, waacheni waleta capital.

Haya mambo ya watanzania watafanya hivi au vile sioni maendeleo yake. Mfano mkubwa ni Standi ya mabasi Ubungo. Investor wa Tanzania anachojua ni kukusanya mapato tu na hakuna maendeleo mengine.
 
Kwa nini Matajiri Tz wasichukuwe mashamba makubwa na kuzalisha mchele mwingi kwa ajili ya Saudia??

Naunga mkono hoja yako ya kuwa Watanzania Matajiri Tz wachukuwe mashamba makubwa na kuzalisha mchele mwingi kwa ajili ya Saudia; lakini kumbuka Matajiri wetu wengi wao wameshakuwa waumini wa UFISADI, na mfumo utakaoratibu hili zoezi nao waweza kutawaliwa na UFISADI. Kumbuka EPA, MEREMETA, TRL, RICHMOND/DOWANS, Kigamboni etc
 
Naunga mkono hoja yako ya kuwa Watanzania Matajiri Tz wachukuwe mashamba makubwa na kuzalisha mchele mwingi kwa ajili ya Saudia; lakini kumbuka Matajiri wetu wengi wao wameshakuwa waumini wa UFISADI, na mfumo utakaoratibu hili zoezi nao waweza kutawaliwa na UFISADI. Kumbuka EPA, MEREMETA, TRL, RICHMOND/DOWANS, Kigamboni etc

Matajiri wa Tz ,aloo bora asikodishwe mtu,kama atalipwa mtu itakuwa mwisho wa dunia,lazima watu wadai mishahara kwa maandamano ,na yeye ataiambia serikali hajapata na kuvuna kiasi kikubwa kwa kukosekana mvua na kina cha maji kupungua ,hapo hata tanesco watanufaika ikiwa jamaa analalamika kuwa kina cha maji kimepungua,wakati keshawakatia wakuu wa polisi chao ,mkuu wa FFU nae chake ,waziri husika nae kidogo na wote vipolo vya mchele kila mwisho wa mwezi . Jamani tunaelewana ni sisi kwa sisi na tabia zetu bado zimeganda ukandamizaji si mnakiona Chama tawala kinavyofanya ukandamizaji kule Pemba ,watu ndio hawa hawa,matajiri ndio hawahawa mafisadi,wataenda kukopa benki kwa kisingizio cha kuwekeza mashamba na halipi mpaka anaingia kaburini ,waacheni watu wenye fedha zao ambao hawatahitajia benki zetu kutaka mokopo kwa feza za kigeni.

Matajiri wetu lazima mshahara utakuwa mbinde na mtu atakuwa hana uwezo wa kufanya lolote ,wakijikusanya wanaitiwa polisi na majibwa ,hivi tunaona wale wanaomfanyia kazi Mkapa kule kwenye mgodi si mmesikia hawajaona mshahara si kuongezwa wala bonus hakuna kitu kama hicho ,kwenye mashamba ya miwa ,si waliuliwa jamaa na walipokusanyika si waliitiwa polisi.

Ila hawa Wasaudi nina hakika watu na familia zao watanufaika tu ,hakuna mjadala juu ya hilo.Tumeona Zimbabwe mashamba waliyoyadai kuwa watayashughulikia na kuwapopkonya wazungu leo nyasi wanalala simba ,hakuna kilicholimwa wala kuvunwa , wazungu ambao ni raia wa Zimbabwe walifukuzwa leo lana na njaa imewaandama.

So wapeni watu wenye uwezo wa kufanya na kutimiza sheria za uajiri.
 
Jasusi,
1.Ni kweli unayosema............unajua nini........watasema itaongeza ajira (mambo ya sera) na kodi kwa serikali.......
2.10%.........i.e.pesa ya uchaguzi ati.....

On the other hand however....hebu tuangalie pia mashamba ya maua kule Kenya......similar thing is happening there, kwani wamiliki wa yale mashamba ni kampuni za Ulaya.....how does Kenya benefit?.......how do we position ourselves ili tu-benefit............Serikali inahitaji wawe wawazi kwenye haya mambo ili kupata mawazo ya wananchi.........

Mkuu hapo umenena, hata mimi nimejiuliza kuwa how will it work for our benefit? Badala ya ku lease,je tunaweza ku facilitate kilimo kiwe bora kwa msaada wao huo ili tuweze kuwauzia mazao bora?

Kimsingi mkataba uwe wa kibiashara zaidi na wao wasaidie kwenye miundo mbinu na kufanikisha kilimo bora,process ikienda hivyo mabadiliko ya kiuchumi yataonekana na pia wananchi nao watapata chakula kwasababu eka laki tano ni eneo kubwa,na kutokana na maelezo hapo juu mazao/chakula wanachohohitaji kununua/kulima pia ni kingi.

Pia kama ikiwezekana badala ya kuchukua ekari laki tano kwenye eneo moja,wanaweza kuzigawa kwenye maeneo mbali mbali nchini ili kuwe na good wealth distribution kwani wakazi wa maeneno hayo watanufaika kwa kupata fursa ya kuuza mazao yao na kujiwekea ziada kwa chakula ama domestic needs.

Ama pia wazo jingine ni kwamba mpango mzima upelekwe kwa wakulima wadogo wadogo wawezeshwe kwenye maeneo yote ambayo ni suitable kwa kilimo, ama wananchi wanategemea kilimo,kuwe na project itakayowasaidia ku apply kilimo bora,na wawekezaji hao na kununua kutoka kwa wananchi....It is possible,ilishafanyika kwenye zao la kahawa.

Ni mawazo tu,cha msingi viongozi wetu wasikurupuke tu kwa kuona mipesa,kwani inaweza ikawanufaisha wachache na huku ardhi tumeshatoa...Ni muhimu kujaribu kuona kwamba chain ya investment hiyo inayainua maisha ya mwananchi wa kawaida wa Tanzania ambapo asilimia kubwa ya wakaazi wake wanategemea kilimo.
 
Back
Top Bottom