Sata aanika ufisadi wa utawala wa Banda taratibu

KunjyGroup

JF-Expert Member
Dec 7, 2009
352
26
Jana Mh. Sata alisema
  • Rais Banda alinunua Lexus 4 x 4 mbili kwa K3.6billion sawa na $720,000 na gari hizo zilikuja na ndege. Sata aliuliza, “Why buy two cars at such a price? Is it really necessary? Bring them by plane?”
  • NAPSA (Kama NSSF yakwetu) ilichotwa 1. $98million by unknown company. 2. $15million by unknown local company. 3. K75billion by unknown individual.
    Aliyekuwa finance director, Mrs. Chiwele alifukuzwa kazi na utawala wa Rais Banda baada yakukataa malipo ya hovyo. Rais Sata kamurudisha kazini na kasema, “Her dismissal will be treated as paid leave and ‘m reinstating her effective today.”
  • Food Reserve boss and finance director (Lazarous Mawere) wamefukuzwa kazi jana, “On national interest….” Hawa jamaa, namjua Mawere, ana magari ya haina ya Scania yanaobeba mahindi wamekula hela ya umma. Kwanza walinunua magari, wakajipa contract yakubeba mahindi wenyewe kwa bei waliyopanga wao.
  • National Service (JKT ya Zambia) wamepewa kazi na Sataa. “As far as I know, you are supposed to be the richest military wing. Thus, ‘m taking you back to your original job; building bridges and agriculture” na akasisitiza kwamba haona sababu yakupewa makampuni ya nje mikataba yakujenga madaraja wakati Nationa service ipo.
  • Juzi rais aliaanika ufisadi kataka ununuzi wa unga kwa wanajeshi. Awali wanajeshi walukuwa wananunuliwa unga na kugawiwa. Mara hii raisn Sata kasema “We know the price of mealie meal but the price it was being bought at is too high and contracts were given to their friend who flamed up prices.” Mara hii rais kasema wanajeshi wapewe hela tu ya unga wakanunue wenyewe na anajua bei ya unga.
Hayo ni machachetu nimeona ni share na wana JF.
Natamani ingekuwa hizi Tz
 
Honestly haya mafunuo ndio yanayowafanya CCM wang'ang'anie madaraka. Haya mafisadi yetu, matakataka waliyoficha itachukua mwaka kuyafichua.
 
Mara mbili yake ndivyo walivyotufanya ccm, na ndo maana wanaogopa kuachia madaraka kwa hiari, bahati mbaya nguvu ya umma lazima ishinde mwisho wa siku.
 
Hata Zambia walitaka kuchakachua wananchi wakawahi kutoka mitaani na kudai kutangazwa kwa matokeo, sasa wanakula matunda matamu ya kupiga kura, kuzilinda na kuzitetea na hii nchi soon itapita hatua kubwa kiuchumi na hata nafuu ya maisha itakuwepo kubwa
 
Tufanye kweli 2015 tupate mabadiliko.
Siku hadi siku, watu wanaendelea kuchoka. Siku moja watasema hapana
 
Ee mungu baba tujaalie nasi watanzania tumpate Sata wetu katika uchaguzi mkuu ujao. Eemen
 
80% ya watanzania wanaishi katika hali inayotia huzuni! watu hawana matumaini sababu ya mambo kama Banda!! Viongozi kama Sata huishi milele hata kama wakifa hubaki wakikumbukwa kwa mambo wanayowafanyia binadamu wenzao. Hakika Sata ni moja ya marais tunaowasubiri kwa muda mrefu Africa.
 
Jana Mh. Sata alisema

  • NAPSA (Kama NSSF yakwetu) ilichotwa 1. $98million by unknown company. 2. $15million by unknown local company. 3. K75billion by unknown individual.
    Aliyekuwa finance director, Mrs. Chiwele alifukuzwa kazi na utawala wa Rais Banda baada yakukataa malipo ya hovyo. Rais Sata kamurudisha kazini na kasema, "Her dismissal will be treated as paid leave and ‘m reinstating her effective today."
  • National Service (JKT ya Zambia) wamepewa kazi na Sataa. "As far as I know, you are supposed to be the richest military wing. Thus, ‘m taking you back to your original job; building bridges and agriculture" na akasisitiza kwamba haona sababu yakupewa makampuni ya nje mikataba yakujenga madaraja wakati Nationa service ipo.
  • Juzi rais aliaanika ufisadi kataka ununuzi wa unga kwa wanajeshi. Awali wanajeshi walukuwa wananunuliwa unga na kugawiwa. Mara hii raisn Sata kasema "We know the price of mealie meal but the price it was being bought at is too high and contracts were given to their friend who flamed up prices." Mara hii rais kasema wanajeshi wapewe hela tu ya unga wakanunue wenyewe na anajua bei ya unga.
Hayo ni machachetu nimeona ni share na wana JF.
Natamani ingekuwa hizi Tz

we need realistic presidents like him. I wish he was my president
 
Sata ndiye atakayetuamshia watanzania, kwa hali ilivyo ccm hawatakaa wapende habari hizi zivume masikioni mwa watanzania
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom