Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,115
- 35,121
Tukio la karne na kihistoria la Spika wa Bunge la Tanzania (Job Ndugai) kuwaapisha chap chap wakina Halima Mdee na wenzake 18 nje ya ukumbi wa Bunge bila kuwepo kwa Wabunge wengine, wala kikao rasmi cha Bunge au kusimikwa kwa Siwa kumezusha mjadala wa kisiasa na Kikatiba.
Mtihani huo sasa umehamia upande wa pili wa kumtaka Spika Ndugai kuwaapisha chap chap Wabunge wapya wawili wa kuteuliwa na Rais ili wakaanze kutumikia mara moja majukumu ya Kibunge.
Safari hii, sijui wataapishiwa wapi?
Sote tunasubiri kuona na kujifunza mapya kutoka kwa Ndugai.
Mtihani huo sasa umehamia upande wa pili wa kumtaka Spika Ndugai kuwaapisha chap chap Wabunge wapya wawili wa kuteuliwa na Rais ili wakaanze kutumikia mara moja majukumu ya Kibunge.
Safari hii, sijui wataapishiwa wapi?
Sote tunasubiri kuona na kujifunza mapya kutoka kwa Ndugai.