Uchaguzi 2020 Sasa tuwasute wahariri wa magazeti ya Kitanzania

dikteta2020

JF-Expert Member
Aug 14, 2018
595
3,990
Magufuli akiwa na kampeni wanachapisha picha kubwa ya kampeni zake kwa juu kisha chini wanaweka vipicha vidogo vya wapinzani. Magufuli akipumzika kampeni hawaweki picha ya mgombea anayetoa upinzani mkubwa kwake wala habari zake hazipewi kabisa kipaumbele.

Nyie wahariri, jana na leo Tundu Lissu alikuwa Geita na wote hakuna aliyethubutu kuchapisha habari zake kama habari kubwa wala kuweka picha ya mkutano wake mbele! Aibu kwenu na uhuru wenu. Yani kwa siku mbili mfululizo habari ya Msajili na ACT ndiyo habari kubwa.

Sasa tumeshawagundua kuwa Hassan Abbas amewapa maagizo maalum. Tutaanzisha harakati maalum kwa ajili yenu maana inaonekana dhahiri mumeuza uhuru wenu!

Aibu! Aibu! Aibu!

Hatujawahi kushuhudia ushenzi huu hapo kabla!
 
Magufuli akiwa na kampeni wanachapisha picha kubwa ya kampeni zake kwa juu kisha chini wanaweka vipicha vidogo vya wapinzani. Magufuli akipumzika kampeni hawaweki picha ya mgombea anayetoa upinzani mkubwa kwake wala habari zake hazipewi kabisa kipaumbele...
Hamjawahi kuomba msamaha wa wazi kama mlivyowafukuza TBC kwa uwazi,
Ganyeni hivyo ili TV na magazeti yawarudie.
 
Magufuli akiwa na kampeni wanachapisha picha kubwa ya kampeni zake kwa juu kisha chini wanaweka vipicha vidogo vya wapinzani. Magufuli akipumzika kampeni hawaweki picha ya mgombea anayetoa upinzani mkubwa kwake wala habari zake hazipewi kabisa kipaumbele...
UMESAHAU KWAMBA LISSU ALIWAAMBIA HAWANA ELIMU?

SASA NDIO MNAONA UMUHIMU WA MEDIA COVERAGE?

ETI MUANZISHE2 HARAKATI, ZIPI ?
Kuyanunua yoote kila siku na kuyachoma au
 
Ni wajinga kiwango cha SGR,maana na imani hats mauzo hao kwa mda huu ni siri yao.watakufa kwa stress.yaacheni hivyohivyo.

Social network shikamoo.
Maana yangu nimenunua kasimu kangu haka,huu ni mwaka wa tank sijawahi kununua gazet wala kuangalia TBC,CHANEL TEN,na uchafu mwingine mwingi kasoro ITV ba yenyewe online.
 
Kiliko kununua vijarida vyao bora kununua gb za kutosha, kule hakuna habari tena
 
Vyombo vya habari ambavyo haviwezi kutetea uhuru wake vyenyewe haviwezi kuwa na msaada wowote kwa jamii.

Acha walambe miguu ili wakwepe kufungiwa.

Hii inadhihirisha wazi kuwa hatuna vyombo vya habari tuna magenge ya wahuni tu walioko vyumba vya habari.
 
Nani anasoma magazeti siku hizi? Waache wafe vibudu. Mambo yote kwenye mitandao ya kijamii sasaivi. Ni heri ukose nauli kuliko ukose bundle sasaivi
Wanapatiwa ruzuku na Mtu fulani kwa kazi maalum. Dhambi hii ndiyo inayoitafuna ccm hivi sasa. Pesa za Umma zimegeuzwa kuwa za mtu mmoja na yeye kuzigawa vile apendavyo na pia kwa hata walio nje ya mpangilio kama hawa Wahariri NJAA.
 
Back
Top Bottom