Sasa tuwageukia upinzani- wajirekebishe na kujipanga mapema

Binti Maria

Senior Member
Jun 26, 2007
158
33
Ok, wandugu. Mimi naona hawa CCM tumeshawazodoa vya kutosha na kuna kila dalili kwamba tunayowaambia yanaingilia huku yanatokea kule. Ni wazi pia kwamba kila mwananchi sasa anajua kwamba hawa CCM hawatabadilika hadi watakapobadilishwa. Hata hivyo ukweli ni kwamba wananchi hawataibadili CCM kwa sababu inafanya makosa. Pamoja na makosa haya, lazima patokee wa kuchukuwa nafasi yao.

Kwa upande wangu naona kwamba upinzani tayari wameshakuwa tayari kutawala. Wana sifa zote kuanzia mawazo mazuri-ambayo ndio msingi wa siasa-hadi uadilifu. Yaani, they are both effective and ethical, vitu ambavyo CCM vyote wameshavipoteza. Sasa tatizo la upinzani linakuja nalo ni wao kusambaa huku na huko huku wakijua kwamba wapo wachache. Ni kwa sababu hii naleta hoja kwamba tuanze mapema kuwabana hawa ili wajikusanye wakae pamoja tayari kwa mapambano ya 2010. Katika kufanya hili ni wazi kwamba wapo watakaopoteza na wapo watakaopata. Lakini ni wazi kwamba taifa letu litapona.

Naleta mapendekezo yafuatayo:

i) Wapinzani lazima waikamate Dar. Lazima katika uchaguzi wa 2010 utemi wa CCM Dar ukomeshwe kabisa. Sababu moja ya wapinzani kushindwa kukamata Dar ni ukweli kwamba huwa wanaweka wagombea wachovu. Sasa ili kuondoa hili napendekeza kwamba big shots wote katika uchaguzi wa 2010 wagombee Dar. Napendekeza wajipange kama ifuatavyo:

a) Kawe: asimame Freeman Mbowe

b) Ubungo asimame: Dr Sengodo Mvungi

c) Temeke au Ilala: asimame Profesa Ibrahimu Lipumba

d) Kinondoni: asimame: James Mbatia

e) Kigamboni- watafute

Hii ina maana kwamba lazima wasimamishe mgombea mmoja wa urais ambaye ni, nani tena zaidi ya, Dr Wilbroad Slaa.

Nyie mnasemaje sasa na mawazo haya?
 
Na Mnyika asimame wapi?

Kuna kweli moja imewahi tokea Danganyika hii pale ambapo nabii wako mteule Dr. Sengondo Mvungi alikataliwa hata home kwa kukosa kura za Uraisi hata katika box lililowekwa kituo cha kupigia kura karibu na nyumba yake anakoishi MLIMANI Chuo Kikuuu.

Nashauri upitie tena kukubalika na kutokubalika kwa wapendekezwa wako katika maeneo husika.
 
a) Kawe: asimame Freeman Mbowe

b) Ubungo asimame: Dr Sengodo Mvungi

c) Temeke au Ilala: asimame Profesa Ibrahimu Lipumba

d) Kinondoni: asimame: James Mbatia

e) Kigamboni- Masatu
 
Ok, wandugu. Mimi naona hawa CCM tumeshawazodoa vya kutosha na kuna kila dalili kwamba tunayowaambia yanaingilia huku yanatokea kule. Ni wazi pia kwamba kila mwananchi sasa anajua kwamba hawa CCM hawatabadilika hadi watakapobadilishwa. Hata hivyo ukweli ni kwamba wananchi hawataibadili CCM kwa sababu inafanya makosa. Pamoja na makosa haya, lazima patokee wa kuchukuwa nafasi yao.

Kwa upande wangu naona kwamba upinzani tayari wameshakuwa tayari kutawala. Wana sifa zote kuanzia mawazo mazuri-ambayo ndio msingi wa siasa-hadi uadilifu. Yaani, they are both effective and ethical, vitu ambavyo CCM vyote wameshavipoteza. Sasa tatizo la upinzani linakuja nalo ni wao kusambaa huku na huko huku wakijua kwamba wapo wachache. Ni kwa sababu hii naleta hoja kwamba tuanze mapema kuwabana hawa ili wajikusanye wakae pamoja tayari kwa mapambano ya 2010. Katika kufanya hili ni wazi kwamba wapo watakaopoteza na wapo watakaopata. Lakini ni wazi kwamba taifa letu litapona.

Naleta mapendekezo yafuatayo:

i) Wapinzani lazima waikamate Dar. Lazima katika uchaguzi wa 2010 utemi wa CCM Dar ukomeshwe kabisa. Sababu moja ya wapinzani kushindwa kukamata Dar ni ukweli kwamba huwa wanaweka wagombea wachovu. Sasa ili kuondoa hili napendekeza kwamba big shots wote katika uchaguzi wa 2010 wagombee Dar. Napendekeza wajipange kama ifuatavyo:

a) Kawe: asimame Freeman Mbowe

b) Ubungo asimame: Dr Sengodo Mvungi

c) Temeke au Ilala: asimame Profesa Ibrahimu Lipumba

d) Kinondoni: asimame: James Mbatia

e) Kigamboni- watafute

Hii ina maana kwamba lazima wasimamishe mgombea mmoja wa urais ambaye ni, nani tena zaidi ya, Dr Wilbroad Slaa.

Nyie mnasemaje sasa na mawazo haya?

Sasa wapinzani wasiposhinda Dar es salaam then itakuwaje?
 
Kabla ya kugawa majimbo kwanza nadhani ungewashauri wapinzani wawe na agenda ya upinzani. Then upinzani, ambao sasa haupo ndio utaanza kuexist. Baada ya hapo utaratibu mwingine wote wa kugawana majimbo etc unaweza kufuata.
 
Wapinzani bado sana kama hali yenyewe ndo hii wasubiri labda karne ya 23!
 
Kabla ya kugawa majimbo kwanza nadhani ungewashauri wapinzani wawe na agenda ya upinzani. Then upinzani, ambao sasa haupo ndio utaanza kuexist. Baada ya hapo utaratibu mwingine wote wa kugawana majimbo etc unaweza kufuata.

mimi nakubaliana nawe Zemarcopolo kuwa Tanzania bado ni nchi ya chama kimoja sasa hivi.
 
Wapinzani bado sana kama hali yenyewe ndo hii wasubiri labda karne ya 23!

Jamani hollo, swali kwako kwanza, hivi wapinzani ni kina nani? inaonekana labda tunatafuta watu tusiowajua kama wapo, wanatakiwa kuwapo, au kama kuwapo kwao kunamaanisha nini.
 
Jamani hollo, swali kwako kwanza, hivi wapinzani ni kina nani? inaonekana labda tunatafuta watu tusiowajua kama wapo, wanatakiwa kuwapo, au kama kuwapo kwao kunamaanisha nini.
vyama vya upinzani chadema,CAF sijui na nini vile maana viko utitiri!vyote vinaipinga CCM!
 
a) Kawe: asimame Freeman Mbowe

b) Ubungo asimame: Myika

c) Temeke au Ilala: asimame Profesa Ibrahimu Lipumba

d) Kinondoni: asimame: Duni Hajj

e) Kigamboni- MSANII

Ila nasema kuwa hii haitowezekana mpaka kitakaposimama chama imara tena jeuri dhidi ya mafisadi.
LAbda tuanzishe harakati za kuupinga ukoloni (kutawaliwa na mafisadi kiuchumi, utamaduni na kisiasa) tunaofanyiwa na kikundi kidogo cha watu dhidi ya wengi
 
e) Kigamboni- MSANII

Ila nasema kuwa hii haitowezekana mpaka kitakaposimama chama imara tena jeuri dhidi ya mafisadi.
LAbda tuanzishe harakati za kuupinga ukoloni (kutawaliwa na mafisadi kiuchumi, utamaduni na kisiasa) tunaofanyiwa na kikundi kidogo cha watu dhidi ya wengi


Ahaaa haaa, hapo umepatia hasa. Lakini sijui utapambana na nani huko.

Nakuunga mkono pia kwamba sasa hivi wapinzania wanahitaji kuwa ngangari hasa maana haya majamaa ya CCM hayana mchezo.
 
Mkuu Kitila Mkumbo
ni wazi kuwa tunaonewa (wananchi) na kunyanyaswa pamoja na kupuuzwa (mayowe yetu kupitia JF). Ni budi harakati za uhuru wa kweli zianze mapema ili wananchi waamue kwa kura...
Bahati mbaya siipendi siasa lakini wakiniomba ushauri nina kajimchango ka mawazo kwa wapinzani.....
 
Mkuu Kitila Mkumbo
ni wazi kuwa tunaonewa (wananchi) na kunyanyaswa pamoja na kupuuzwa (mayowe yetu kupitia JF). Ni budi harakati za uhuru wa kweli zianze mapema ili wananchi waamue kwa kura...
Bahati mbaya siipendi siasa lakini wakiniomba ushauri nina kajimchango ka mawazo kwa wapinzani.....

tuanzeje?
manake hapa mimi ni follower number one wa sera za uwazi na ukweli, kasoro tu ni kupata kichwa chakutuongoza.
 
Ahaaa haaa, hapo umepatia hasa. Lakini sijui utapambana na nani huko.

Nakuunga mkono pia kwamba sasa hivi wapinzania wanahitaji kuwa ngangari hasa maana haya majamaa ya CCM hayana mchezo.


Mkuu, ili upinzani uwe ngangari inabidi msikilize ushauri wa Watanzania walio ndani na nje ya Tanzania.

Watanzania wanawashauri kwamba muweke ubinafsi pembeni ili muunde chama kimoja chenye nguvu mapema iwezekanavyo ili chama hicho kiweze kushiriki katika uchaguzi wa 2010 maana vyama vya upinzani vilivyopo sasa vimeshaonyesha havina nguvu na hivyo kufanya vibaya katika chaguzi za 1995, 2000 na 2005.

Mtengeneze sera zenu mtakazozitumia katika uchaguzi wa 2010 na hatimaye kuzitumia kuendesha nchi kama mkifanikwa kuchukua nchi toka kwa chama cha mafisadi, na sioni kwa nini mshindwe kuchukua nchi maana Watanzania tulio wengi tumechoshwa na CCM na hatuoni mabadiliko yoyote ndani ya chama hicho zaidi ya mafisadi kushika utamu.

Watanzania pia wanawashauri badala ya kukaa mijini mwende vijijini ambapo ndiyo wengi wa Watanzania wanaishi ili mkajitangaze huko na pia kuwafahamisha matatizo mbali mbali ya nchi yetu yanayosababishwa na chama cha mafisadi.

Mkishindwa kuutekeleza ushauri wa Watanzania walio wengi, basi na nyinyi mtaonekana machoni mwa Watanzania wengi kama ni wasanii tu ambao mmeweka maslahi yenu mbele badala ya yale nchi na hivyo kutoona umuhimu wa kuunda chama chenye nguvu. Tunawapa pongezi kubwa kwa kufunua uozo mbali mbali kuhusiana na EPA, Richmond, mikataba mibovu ya madini n.k. lakini kamwe msitegemee kuingia madarakani kupitia hivi vyama vya upinzani vilivyopo sasa bila kuufuata na kuutekeleza ushauri wa Watanzania. UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU. YES WE CAN BUILD A BETTER TANZANIA WITHOUT MAFISADI NA MWALIMU ALISEMA, IT CAN BE DONE JUST PLAY YOUR PART.
 
Wapinzani bado sana kama hali yenyewe ndo hii wasubiri labda karne ya 23!

Wakiamua kubadilika kwa kusikiliza ushauri wa Watanzania wanaweza wakafanya kweli, lakini wakiendelea kupuuza ushauri tunaowapa na kuendekeza ubinafsi wao basi wataendelea kuwa wapinzani milele.
 
Niliwahi kusema huko nyuma kuwa; ilikuwaje wakulima wa Mpanda Kati wakagoma rushwa ktk uchaguzi 2005 na wakachagua Chadema,halafu wajanja wa Dsm tukachagua CCM?

Tatizo ni aina ya wapiga kura wetu?
 
Wapinzani watake OVER sasa halafu walete mambo tuendelee tukiyachambua ili tujue nani ni nani na kwanini etc etc.
 
Wapinzani watake OVER sasa halafu walete mambo tuendelee tukiyachambua ili tujue nani ni nani na kwanini etc etc.

Nadhani mkuu wapinzani wamechangia sana kuleta mambo mengi yanayoongelewa hapa jamvini. Unless unataka kusema kuwa walete mambo zaidi maana so far wanafanya kazi nzuri sana.
 
In any case... wapinzani have long way to go!

Ukitaka kupata mafanikio makubwa kwenye upinzani... hakikisha... umechukua majimbo yote ya Dar es Salaa, Mwanza... na Mbeya... nawahakikishia wapinzani wakiweza kuteka majiji hayo wakawa na serikali zao za mitaa... the job is done... kwa kuwa li-nchi nilikubwa sana... anzeni na hilo... hivyo nakubaliana na mtoa hoja... kwamba waweze wagombea heavy duty dar es salaam.

Lakini ilikuwa ni udhaifu mkubwa... at Dar es Salaam CCM ndio imeshinda kwa kishindo... ilikuwa ni aibu kubwa sana... kwa wananchi wapenda upinzani
 
In any case... wapinzani have long way to go!

Ukitaka kupata mafanikio makubwa kwenye upinzani... hakikisha... umechukua majimbo yote ya Dar es Salaa, Mwanza... na Mbeya... nawahakikishia wapinzani wakiweza kuteka majiji hayo wakawa na serikali zao za mitaa... the job is done...

Lakini ilikuwa ni udhaifu mkubwa... at Dar es Salaam CCM ndio imeshinda kwa kishindo... ilikuwa ni aibu kubwa sana... kwa wananchi wapenda upinzani

Mkuu wangu kasheshe.

Kushinda kwa kishindo kwa ccm in the light ya upotevu wa pesa kule BoT kwa sasa uko tainted sana. Ni vigumu sana kusema kwa hakika kama ccm ilishinda kwa kishindo.
 
Back
Top Bottom