Sasa tunakubaliana kwamba mliipenda sana maiti ya Tundu Lissu kuliko uhai wake

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Swali la kujiuliza; nani anaemuogopa Tundu Lissu hata kufikia hatua ya kujaribu kumuua? Kumuua mchana wa Jua kali. Serikali? Magenge ya wahalifu? Wanasiasa wenzake? Lakini Tundu Lissu ametupa majibu ya kila swali ambalo tunaendelea kujiuliza;

Matukio kama haya ya 'kuogofya' na 'kusikitisha' yanapotokea watu huunganisha matukio kadhaa kupata kitu kamili. Tundu Lissu ni 'mwiba mkali' kwa serikali hii. Watu wanaokosolewa nae; hawana uthubutu wa kuvumilia ukosoaji wake.

Kabla ya kupigwa risasi, amekamatwa mara kadhaa na kulazwa mahabusu, amesafirishwa usiku kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kujibu tuhuma za uchochezi. Ameshtakiwa kwa makosa mbalimbali na hawajawahi kumtia hatiani. Tunaunganisha 'dots'

Watu hawa wanaendelea kutuaminisha kwamba hili lilikuwa jaribio hafifu la mauaji kutoka kwa "watu wasiojulikana" dhidi ya Tundu Lissu na Tunaendelea kumshukuru Mungu Tundu Lissu amepona na anaendelea kuimarika kila uchwao.

Shambulio dhidi ya Tundu Lissu lilikuwa jaribio la kuondoa uhai wake. Tazama risasi zilizotumika. Silaha. Sio mchezo wa kuigiza. Tundu Lissu kaumizwa. Mumgu wake ni mwema. Kamfanya kuwa "muujiza unaotembea" na hili limewakera wengi wenye kuhusika.

Unasikia kauli zao, maneno yao yanawahukumu. Ukakasi ni mkubwa. Ni watu wamejawa na ghilba, husuda na chuki dhidi ya Tundu Lissu. Kauli zao hata shetani anaogopa; ni zaidi ya 'ushetani' wenyewe.

Unamsikiliza katibu mkuu wao, unarejea kumsikiliza katibu wao wa itikadi na uenezi kisha unasikiliza wafuasi wao wakisema kwa kupokezana sauti za 'kupayuka' na zenye kujazwa na chuki.

Katibu mkuu wao anasema mwenyekiti wao ndie tiba ya ugonjwa unaitwa 'Tundu Lissu' na kusema Lissu "anajidekeza" na wakati huo "makada" wenzake wanachukizwa nae na hata kusema mbele ya masuala ya 'futiboli' kuhusu habari za mtu huyu.

Katibu wao wa itikadi na uenezi bwana Chakubanga ambaye ni 'spesheli' katika masuala ya "propaganda" anatueleza kwamba Tundu Lissu sio kiumbe wa kwanza kupigwa risasi nchi hii; wapo wengi wa CCM huko Kibiti. Hivyo Lissu asitupigie kelele. Loh!

Kuna kada mwingine kutoka huko CCM nae anatupa simulizi kwamba bwana Tundu Lissu hajashambuliwa kwa risasi za moto isipokuwa kwa vitu vinaitwa "bl(r)anco" ndio maana yupo hai. Hawa watu wamepagawa vibaya.

Waziri nae anayo yake kuhusu hili, wakati polisi walitueleza awali kuhusu uwepo wa kamera za CCTV eneo aliloshambuliwa Tundu Lissu, mwaka mmoja baadae waziri anasema eneo hilo hapajawahi kuwepo 'security cameras' .. inashangaza!

Mkuu wa wilaya huko Kigamboni anasema Askari wa nchi hii hawajawahi kukosa shabaha, hivyo hawawezi kutumia risasi zaidi ya 40 na wasimpate Tundu Lissu; inatia simanzi; nani anawatuhumu askari wetu katika shambulio hilo? Wameanza kujishtukia na 'kuropoka' hapa al'badr inafanya kazi yake.

Wanaonekana ni watu walioumizwa na jaribio la kumuua Tundu Lissu 'kutofanikiwa' na wamechukizwa zaidi baada ya kuona kiumbe huyu amepona risasi 16 na amefanikiwa kutoka kwenye 'operesheni' 23 sasa.. wanashangaa huu muujiza.

Hawa watu walitamaani maiti ya Tundu Lissu isiagwe DSM au Dodoma. Ipelekwe kuzikwa mara moja Ikungi, pahali alipozaliwa 'mtanzania' huyu. Tundu Lissu anatueleza kwamba watu hawa hawakupenda kuona anapewa heshima ya 'kibunge' hata kidogo.

Ukiwatazama, unarejea maswali ya awali, kwanini watu hawa walikuwa wanashinikiza apelekwe Muhimbili kupata matibabu na sio nje ya nchi? Kwanini watu hawa waliumizwa na Tundu Lissu kupelekwa Nairobi, Kenya kupata matibabu?

Wapo wengine wenye kusema akirejea auwawe kwa kupigwa risasi. Wanaandika hayo mtandaoni. Tena kwa kurudia-rudia; Polisi wanaona. Wamefumba macho. Hawachukui hatua za kisheria dhidi yao. Hii ni ishara kwamba mtu huyu anawatikisa ipasavyo.

Wameshindwa kujibu hoja zake, Wakampiga risasi nyingi. Wameshindwa kujibu hoja zake, sasa wanapanga kumuua kabisa kama akirejea Tanzania. Tundu Lissu amewashinda mahakamani; amewashinda jukwaani sasa wanataka uhai wake.

Sasa wamepanga kumfunga magereza. Wanaamini ndio njia sahihi ya kumtuliza na kumfanya atulie. hawana hoja jadilifu. Wanatumia 'magereza' kukandamiza yoyote wanaemchukia. Wamekwenda mahakamani kuomba mahakama imfutie dhamana yake; awekwe mahabusu kama Mbowe na Esther Matiko.

Wamejaribu na wamefanikiwa. Walimpeleka Lema mahabusu. Wamempeleka Mbowe/Matiko mahabusu sawa na mtu aliyefungwa miezi mitano. Sasa wanataka mahakama impeleke Tundu Lissu huko, akiwa na matundu 16 ya risasi na operesheni 23 katika mwili wake.

Mawakili wa serikali kupeleka ombi la mahakama kumfutia dhamana Tundu Lissu, 'kisheria' wanaweza kuwa sahihi, lakini uungwana na UTU ulipaswa kuwa busara yao. Hapa ndio naamini ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali inabeba taswira nzima ya serikali katika hili.

Unaweza vipi kuomba mahakama imfutie dhamana mtu ambaye anaendelea kupata matibabu nje ya nchi? Majeraha ya risasi na operesheni nyingi mwilini? Tena wadhamini wake wakiendelea kufika mahakamani; pia mawakili wake. UTU ndani yao haupo? Wametumwa na serikali, hawajajituma!

Mwili wa Tundu Lissu umechanwa'chanwa kwa risasi lakini mawakili wa serikali wanataka akauguze majeraha hayo magereza na sio hospitali. Wanachukizwa wakiona anaendelea kupata nafuu. Walitamani kuona anapelekwa Ikungi akiwa marehemu.

Tundu Lissu huyu ambaye kapigwa risasi 16 mwilini kwake; katibu mkuu wa CCM anasema Tundu Lissu 'anajidekeza' na hajawahi kushika jembe, looh! Hivi kujidekeza mbele ya bunduki ya 'kivita' inawezekana vipi? Bashiru rudisha akili ulipoazima, chutama!!

Wakati huo spika wa bunge nae anasema anaufunga mshahara wa Tundu Lissu. Spika wa bunge ambalo halijawahi kujadili taarifa ya hali ya afya ya Tundu Lissu anamtaka Lissu arejee jimboni bila ruhusa ya madaktari.

Kauli zao zinatuonesha matendo yao. Hizi hasira zao ni sehemu tu ya maumivu yao kwa kumuona Tundu Lissu amesimama wima. Wamejawa na hofu katika vifua vyao. Wameshika dola lakini wanakerwa na 'msingidani' huyu. Hofu ni kubwa juu yao.

Kauli hizi za viongozi na wanachama wa CCM zikiendelea kuachwa kwenye matukio kama haya, Nchi yetu itaendelea kuwa sehemu yenye kuogopesha; sifikirii kama tunapaswa kuiweka nchi yetu huko, haiwezekani.

Tuendelee kuombea akili za hawa watu; wamevurugwa; wanateseka; wanapita wakati mgumu kuliko hata Tundu Lissu aliyepo hospitali katika matibabu.

MMM, Martin Maranja Masese
 
Ninaamini hakuna sheria inayoruhusu mtu kufutiwa dhamana ya kushindwa kufika mahakamani huku mtuhumiwa akiwa kwenye kitanda cha oparesheni, kumbuka wakati ombi hili linafikishwa mahakamani Lissu alikuwa huko kitandani anafanyiwa oparesheni! Kama ipo itakuwa ni ya enzi za Hitler.
 
Mungu aliwajibu nia yao mbaya ya kutaka kumuua TL kwa kumuweka hai mpaka leo, lakini inaonekana roho ya kusikia sauti ya Mungu hawana!

Kwa mara nƴingine Mungu amewatumia ujumbe kupitia kwa mwanae hakimu yule wa Kisutu kuwaeleza kuwa mbona roho za utu na ubinadamu hawana!? Sina uhakika kama sauti hii wameisikia na kuielewa!

Ƙwa kuwa ibilisi shetani anatenɗa kazi ndani yao, waache waendelee kujipaka kinyesi.
 
Mungu aliwajibu nia yao mbaya ya kutaka kumuua TL kwa kumuweka hai mpaka leo, lakini inaonekana roho ya kusikia sauti ya Mungu hawana!
Kwa mara nƴingine Mungu amewatumia ujumbe kupitia kwa mwanae hakimu yule wa Kisutu kuwaeleza kuwa mbona roho za utu na ubinadamu hawana!? Sina uhakika kama sauti hii wameisikia na kuielewa!
Ƙwa kuwa ibilisi shetani anatenɗa kazi ndani yao, waache waendelee kujipaka kinyesi.
Jiwe hiyo roho ya namna hiyo iko Rwanda Burundi na Congo afrika ya kati Sudan somalia.Tanzania hatuna roho ya uharibifu kama yako.Mungu akikasirika hats kama una madaraka kiasi gani atakuaibisha siku moja na Italia na kusaga meno

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watafahamika kwa maandishi yao humu. Mungu hajawahi kushindwa.
 
Daaah kwa hali tuliyofikia sasa watz inasikitisha sana

Yaani chuki mioyoni mwetu imetamalaki kweli kweli upendo umepotea

Yaani inafikia hatua anamchukia MTU kweli kweli hata hajishtukia MTU anatamani MTU mwingine aliuwe kisa tu eti anamchukia

Kwakweli mi natamani siku tushikane mapanga huku mtaani ili hii chuki ipotee kabisa

Na alaaniwe yule alikuja kutupandikiza hii chuki na visasi vyake

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana ndugu.
Hata Mwenyezi Mungu huwa anatoamuda wa rehema huenda kesho wakabadilika wakawa watu wazuri.

Ila wakiendeleza chuki hizi, ipo siku watalipwa sawasawa na wanachokipanda huenda ndoto zako zikatimia.

Pole sana mzalendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bandiko lako ni zuri kupindukia, nilitamani kuendelea kusoma ingaewa nipo masjid kwa muda huu, ghafla limeisha. M/Mungu ni mwema kwa mabaya wale walio mfanyia Mh: T.Lissu ipo siku watalipwa kwa ubaya wao!
 
Mungu aliwajibu nia yao mbaya ya kutaka kumuua TL kwa kumuweka hai mpaka leo, lakini inaonekana roho ya kusikia sauti ya Mungu hawana!
Kwa mara nƴingine Mungu amewatumia ujumbe kupitia kwa mwanae hakimu yule wa Kisutu kuwaeleza kuwa mbona roho za utu na ubinadamu hawana!? Sina uhakika kama sauti hii wameisikia na kuielewa!
Ƙwa kuwa ibilisi shetani anatenɗa kazi ndani yao, waache waendelee kujipaka kinyesi.
Usiposikia onyo la kwanza la Mungu ukashupaza shingo jiandae kukutwa na ya Farao,
Tutaraji hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UMEULIZA " Swali la kujiuliza; nani anaemuogopa Tundu Lissu hata kufikia hatua ya kujaribu kumuua?

JIBU: WANAOOGOPEA VITI VYAO, kama kina Mbowe, Lowassa na wengine wengi tuu

Sent using Jamii Forums mobile app[/Q
Uchunguzi ungefanyika na kuleta ripoti amabayo ingedhihirisha kuwa waliofanya shambulio ni CDM, Hapo tunge waelewa lakini mlivyopigwa UPOFU wa MACHO na AKILI Mpaka wasomi na watawala mnaleta hoja dhaifu kama hiyo bila kufikiri kuwa POLISI wanapaswa kuchunguza tukio hata kama ni la mtu kujinyonga mwenyewe.
MAGAMBA a.k.a TIMU POLONIUM Hakika hamjawahi kupata aibu Kama hii ya kumshambulia LISSU tangu mzaliwe 1977.
 
Swali la kujiuliza; nani anaemuogopa Tundu Lissu hata kufikia hatua ya kujaribu kumuua? Kumuua mchana wa Jua kali. Serikali? Magenge ya wahalifu? Wanasiasa wenzake? Lakini Tundu Lissu ametupa majibu ya kila swali ambalo tunaendelea kujiuliza;

Matukio kama haya ya 'kuogofya' na 'kusikitisha' yanapotokea watu huunganisha matukio kadhaa kupata kitu kamili. Tundu Lissu ni 'mwiba mkali' kwa serikali hii. Watu wanaokosolewa nae; hawana uthubutu wa kuvumilia ukosoaji wake.

Kabla ya kupigwa risasi, amekamatwa mara kadhaa na kulazwa mahabusu, amesafirishwa usiku kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kujibu tuhuma za uchochezi. Ameshtakiwa kwa makosa mbalimbali na hawajawahi kumtia hatiani. Tunaunganisha 'dots'

Watu hawa wanaendelea kutuaminisha kwamba hili lilikuwa jaribio hafifu la mauaji kutoka kwa "watu wasiojulikana" dhidi ya Tundu Lissu na Tunaendelea kumshukuru Mungu Tundu Lissu amepona na anaendelea kuimarika kila uchwao.

Shambulio dhidi ya Tundu Lissu lilikuwa jaribio la kuondoa uhai wake. Tazama risasi zilizotumika. Silaha. Sio mchezo wa kuigiza. Tundu Lissu kaumizwa. Mumgu wake ni mwema. Kamfanya kuwa "muujiza unaotembea" na hili limewakera wengi wenye kuhusika.

Unasikia kauli zao, maneno yao yanawahukumu. Ukakasi ni mkubwa. Ni watu wamejawa na ghilba, husuda na chuki dhidi ya Tundu Lissu. Kauli zao hata shetani anaogopa; ni zaidi ya 'ushetani' wenyewe.

Unamsikiliza katibu mkuu wao, unarejea kumsikiliza katibu wao wa itikadi na uenezi kisha unasikiliza wafuasi wao wakisema kwa kupokezana sauti za 'kupayuka' na zenye kujazwa na chuki.

Katibu mkuu wao anasema mwenyekiti wao ndie tiba ya ugonjwa unaitwa 'Tundu Lissu' na kusema Lissu "anajidekeza" na wakati huo "makada" wenzake wanachukizwa nae na hata kusema mbele ya masuala ya 'futiboli' kuhusu habari za mtu huyu.

Katibu wao wa itikadi na uenezi bwana Chakubanga ambaye ni 'spesheli' katika masuala ya "propaganda" anatueleza kwamba Tundu Lissu sio kiumbe wa kwanza kupigwa risasi nchi hii; wapo wengi wa CCM huko Kibiti. Hivyo Lissu asitupigie kelele. Loh!

Kuna kada mwingine kutoka huko CCM nae anatupa simulizi kwamba bwana Tundu Lissu hajashambuliwa kwa risasi za moto isipokuwa kwa vitu vinaitwa "bl(r)anco" ndio maana yupo hai. Hawa watu wamepagawa vibaya.

Waziri nae anayo yake kuhusu hili, wakati polisi walitueleza awali kuhusu uwepo wa kamera za CCTV eneo aliloshambuliwa Tundu Lissu, mwaka mmoja baadae waziri anasema eneo hilo hapajawahi kuwepo 'security cameras' .. inashangaza!

Mkuu wa wilaya huko Kigamboni anasema Askari wa nchi hii hawajawahi kukosa shabaha, hivyo hawawezi kutumia risasi zaidi ya 40 na wasimpate Tundu Lissu; inatia simanzi; nani anawatuhumu askari wetu katika shambulio hilo? Wameanza kujishtukia na 'kuropoka' hapa al'badr inafanya kazi yake.

Wanaonekana ni watu walioumizwa na jaribio la kumuua Tundu Lissu 'kutofanikiwa' na wamechukizwa zaidi baada ya kuona kiumbe huyu amepona risasi 16 na amefanikiwa kutoka kwenye 'operesheni' 23 sasa.. wanashangaa huu muujiza.

Hawa watu walitamaani maiti ya Tundu Lissu isiagwe DSM au Dodoma. Ipelekwe kuzikwa mara moja Ikungi, pahali alipozaliwa 'mtanzania' huyu. Tundu Lissu anatueleza kwamba watu hawa hawakupenda kuona anapewa heshima ya 'kibunge' hata kidogo.

Ukiwatazama, unarejea maswali ya awali, kwanini watu hawa walikuwa wanashinikiza apelekwe Muhimbili kupata matibabu na sio nje ya nchi? Kwanini watu hawa waliumizwa na Tundu Lissu kupelekwa Nairobi, Kenya kupata matibabu?

Wapo wengine wenye kusema akirejea auwawe kwa kupigwa risasi. Wanaandika hayo mtandaoni. Tena kwa kurudia-rudia; Polisi wanaona. Wamefumba macho. Hawachukui hatua za kisheria dhidi yao. Hii ni ishara kwamba mtu huyu anawatikisa ipasavyo.

Wameshindwa kujibu hoja zake, Wakampiga risasi nyingi. Wameshindwa kujibu hoja zake, sasa wanapanga kumuua kabisa kama akirejea Tanzania. Tundu Lissu amewashinda mahakamani; amewashinda jukwaani sasa wanataka uhai wake.

Sasa wamepanga kumfunga magereza. Wanaamini ndio njia sahihi ya kumtuliza na kumfanya atulie. hawana hoja jadilifu. Wanatumia 'magereza' kukandamiza yoyote wanaemchukia. Wamekwenda mahakamani kuomba mahakama imfutie dhamana yake; awekwe mahabusu kama Mbowe na Esther Matiko.

Wamejaribu na wamefanikiwa. Walimpeleka Lema mahabusu. Wamempeleka Mbowe/Matiko mahabusu sawa na mtu aliyefungwa miezi mitano. Sasa wanataka mahakama impeleke Tundu Lissu huko, akiwa na matundu 16 ya risasi na operesheni 23 katika mwili wake.

Mawakili wa serikali kupeleka ombi la mahakama kumfutia dhamana Tundu Lissu, 'kisheria' wanaweza kuwa sahihi, lakini uungwana na UTU ulipaswa kuwa busara yao. Hapa ndio naamini ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali inabeba taswira nzima ya serikali katika hili.

Unaweza vipi kuomba mahakama imfutie dhamana mtu ambaye anaendelea kupata matibabu nje ya nchi? Majeraha ya risasi na operesheni nyingi mwilini? Tena wadhamini wake wakiendelea kufika mahakamani; pia mawakili wake. UTU ndani yao haupo? Wametumwa na serikali, hawajajituma!

Mwili wa Tundu Lissu umechanwa'chanwa kwa risasi lakini mawakili wa serikali wanataka akauguze majeraha hayo magereza na sio hospitali. Wanachukizwa wakiona anaendelea kupata nafuu. Walitamani kuona anapelekwa Ikungi akiwa marehemu.

Tundu Lissu huyu ambaye kapigwa risasi 16 mwilini kwake; katibu mkuu wa CCM anasema Tundu Lissu 'anajidekeza' na hajawahi kushika jembe, looh! Hivi kujidekeza mbele ya bunduki ya 'kivita' inawezekana vipi? Bashiru rudisha akili ulipoazima, chutama!!

Wakati huo spika wa bunge nae anasema anaufunga mshahara wa Tundu Lissu. Spika wa bunge ambalo halijawahi kujadili taarifa ya hali ya afya ya Tundu Lissu anamtaka Lissu arejee jimboni bila ruhusa ya madaktari.

Kauli zao zinatuonesha matendo yao. Hizi hasira zao ni sehemu tu ya maumivu yao kwa kumuona Tundu Lissu amesimama wima. Wamejawa na hofu katika vifua vyao. Wameshika dola lakini wanakerwa na 'msingidani' huyu. Hofu ni kubwa juu yao.

Kauli hizi za viongozi na wanachama wa CCM zikiendelea kuachwa kwenye matukio kama haya, Nchi yetu itaendelea kuwa sehemu yenye kuogopesha; sifikirii kama tunapaswa kuiweka nchi yetu huko, haiwezekani.

Tuendelee kuombea akili za hawa watu; wamevurugwa; wanateseka; wanapita wakati mgumu kuliko hata Tundu Lissu aliyepo hospitali katika matibabu.

MMM, Martin Maranja Masese

Duuuh, hakika "HUU NI MSUMARI WA MOTO, KWA WALENGWA"
 
Taarifa za kinabii zinaeleza kwamba kila aliyehusika na njama za shambulio la lissu atakufa kabla yake , maono yanaonyesha kwamba mwaka huu pekee watakufa watano , hawa wote wana maradhi ya muda mrefu
Mwacheni Ruge apate attention yake maana amefariki. Duh! Maana si kwa kulazimisha huku! Kwasasa habari ya mjini ni marehemu, mgonjwa baadae. Tukishazika tutaendelea na harambee za mavazi ya jamaa.
 
Swali la kujiuliza; nani anaemuogopa Tundu Lissu hata kufikia hatua ya kujaribu kumuua? Kumuua mchana wa Jua kali. Serikali? Magenge ya wahalifu? Wanasiasa wenzake? Lakini Tundu Lissu ametupa majibu ya kila swali ambalo tunaendelea kujiuliza;

Matukio kama haya ya 'kuogofya' na 'kusikitisha' yanapotokea watu huunganisha matukio kadhaa kupata kitu kamili. Tundu Lissu ni 'mwiba mkali' kwa serikali hii. Watu wanaokosolewa nae; hawana uthubutu wa kuvumilia ukosoaji wake.

Kabla ya kupigwa risasi, amekamatwa mara kadhaa na kulazwa mahabusu, amesafirishwa usiku kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine kujibu tuhuma za uchochezi. Ameshtakiwa kwa makosa mbalimbali na hawajawahi kumtia hatiani. Tunaunganisha 'dots'

Watu hawa wanaendelea kutuaminisha kwamba hili lilikuwa jaribio hafifu la mauaji kutoka kwa "watu wasiojulikana" dhidi ya Tundu Lissu na Tunaendelea kumshukuru Mungu Tundu Lissu amepona na anaendelea kuimarika kila uchwao.

Shambulio dhidi ya Tundu Lissu lilikuwa jaribio la kuondoa uhai wake. Tazama risasi zilizotumika. Silaha. Sio mchezo wa kuigiza. Tundu Lissu kaumizwa. Mumgu wake ni mwema. Kamfanya kuwa "muujiza unaotembea" na hili limewakera wengi wenye kuhusika.

Unasikia kauli zao, maneno yao yanawahukumu. Ukakasi ni mkubwa. Ni watu wamejawa na ghilba, husuda na chuki dhidi ya Tundu Lissu. Kauli zao hata shetani anaogopa; ni zaidi ya 'ushetani' wenyewe.

Unamsikiliza katibu mkuu wao, unarejea kumsikiliza katibu wao wa itikadi na uenezi kisha unasikiliza wafuasi wao wakisema kwa kupokezana sauti za 'kupayuka' na zenye kujazwa na chuki.

Katibu mkuu wao anasema mwenyekiti wao ndie tiba ya ugonjwa unaitwa 'Tundu Lissu' na kusema Lissu "anajidekeza" na wakati huo "makada" wenzake wanachukizwa nae na hata kusema mbele ya masuala ya 'futiboli' kuhusu habari za mtu huyu.

Katibu wao wa itikadi na uenezi bwana Chakubanga ambaye ni 'spesheli' katika masuala ya "propaganda" anatueleza kwamba Tundu Lissu sio kiumbe wa kwanza kupigwa risasi nchi hii; wapo wengi wa CCM huko Kibiti. Hivyo Lissu asitupigie kelele. Loh!

Kuna kada mwingine kutoka huko CCM nae anatupa simulizi kwamba bwana Tundu Lissu hajashambuliwa kwa risasi za moto isipokuwa kwa vitu vinaitwa "bl(r)anco" ndio maana yupo hai. Hawa watu wamepagawa vibaya.

Waziri nae anayo yake kuhusu hili, wakati polisi walitueleza awali kuhusu uwepo wa kamera za CCTV eneo aliloshambuliwa Tundu Lissu, mwaka mmoja baadae waziri anasema eneo hilo hapajawahi kuwepo 'security cameras' .. inashangaza!

Mkuu wa wilaya huko Kigamboni anasema Askari wa nchi hii hawajawahi kukosa shabaha, hivyo hawawezi kutumia risasi zaidi ya 40 na wasimpate Tundu Lissu; inatia simanzi; nani anawatuhumu askari wetu katika shambulio hilo? Wameanza kujishtukia na 'kuropoka' hapa al'badr inafanya kazi yake.

Wanaonekana ni watu walioumizwa na jaribio la kumuua Tundu Lissu 'kutofanikiwa' na wamechukizwa zaidi baada ya kuona kiumbe huyu amepona risasi 16 na amefanikiwa kutoka kwenye 'operesheni' 23 sasa.. wanashangaa huu muujiza.

Hawa watu walitamaani maiti ya Tundu Lissu isiagwe DSM au Dodoma. Ipelekwe kuzikwa mara moja Ikungi, pahali alipozaliwa 'mtanzania' huyu. Tundu Lissu anatueleza kwamba watu hawa hawakupenda kuona anapewa heshima ya 'kibunge' hata kidogo.

Ukiwatazama, unarejea maswali ya awali, kwanini watu hawa walikuwa wanashinikiza apelekwe Muhimbili kupata matibabu na sio nje ya nchi? Kwanini watu hawa waliumizwa na Tundu Lissu kupelekwa Nairobi, Kenya kupata matibabu?

Wapo wengine wenye kusema akirejea auwawe kwa kupigwa risasi. Wanaandika hayo mtandaoni. Tena kwa kurudia-rudia; Polisi wanaona. Wamefumba macho. Hawachukui hatua za kisheria dhidi yao. Hii ni ishara kwamba mtu huyu anawatikisa ipasavyo.

Wameshindwa kujibu hoja zake, Wakampiga risasi nyingi. Wameshindwa kujibu hoja zake, sasa wanapanga kumuua kabisa kama akirejea Tanzania. Tundu Lissu amewashinda mahakamani; amewashinda jukwaani sasa wanataka uhai wake.

Sasa wamepanga kumfunga magereza. Wanaamini ndio njia sahihi ya kumtuliza na kumfanya atulie. hawana hoja jadilifu. Wanatumia 'magereza' kukandamiza yoyote wanaemchukia. Wamekwenda mahakamani kuomba mahakama imfutie dhamana yake; awekwe mahabusu kama Mbowe na Esther Matiko.

Wamejaribu na wamefanikiwa. Walimpeleka Lema mahabusu. Wamempeleka Mbowe/Matiko mahabusu sawa na mtu aliyefungwa miezi mitano. Sasa wanataka mahakama impeleke Tundu Lissu huko, akiwa na matundu 16 ya risasi na operesheni 23 katika mwili wake.

Mawakili wa serikali kupeleka ombi la mahakama kumfutia dhamana Tundu Lissu, 'kisheria' wanaweza kuwa sahihi, lakini uungwana na UTU ulipaswa kuwa busara yao. Hapa ndio naamini ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali inabeba taswira nzima ya serikali katika hili.

Unaweza vipi kuomba mahakama imfutie dhamana mtu ambaye anaendelea kupata matibabu nje ya nchi? Majeraha ya risasi na operesheni nyingi mwilini? Tena wadhamini wake wakiendelea kufika mahakamani; pia mawakili wake. UTU ndani yao haupo? Wametumwa na serikali, hawajajituma!

Mwili wa Tundu Lissu umechanwa'chanwa kwa risasi lakini mawakili wa serikali wanataka akauguze majeraha hayo magereza na sio hospitali. Wanachukizwa wakiona anaendelea kupata nafuu. Walitamani kuona anapelekwa Ikungi akiwa marehemu.

Tundu Lissu huyu ambaye kapigwa risasi 16 mwilini kwake; katibu mkuu wa CCM anasema Tundu Lissu 'anajidekeza' na hajawahi kushika jembe, looh! Hivi kujidekeza mbele ya bunduki ya 'kivita' inawezekana vipi? Bashiru rudisha akili ulipoazima, chutama!!

Wakati huo spika wa bunge nae anasema anaufunga mshahara wa Tundu Lissu. Spika wa bunge ambalo halijawahi kujadili taarifa ya hali ya afya ya Tundu Lissu anamtaka Lissu arejee jimboni bila ruhusa ya madaktari.

Kauli zao zinatuonesha matendo yao. Hizi hasira zao ni sehemu tu ya maumivu yao kwa kumuona Tundu Lissu amesimama wima. Wamejawa na hofu katika vifua vyao. Wameshika dola lakini wanakerwa na 'msingidani' huyu. Hofu ni kubwa juu yao.

Kauli hizi za viongozi na wanachama wa CCM zikiendelea kuachwa kwenye matukio kama haya, Nchi yetu itaendelea kuwa sehemu yenye kuogopesha; sifikirii kama tunapaswa kuiweka nchi yetu huko, haiwezekani.

Tuendelee kuombea akili za hawa watu; wamevurugwa; wanateseka; wanapita wakati mgumu kuliko hata Tundu Lissu aliyepo hospitali katika matibabu.

MMM, Martin Maranja Masese
Hata warundi ambao tunaamini viongozi wetu wana chimbuko huko hawana akili ya wanyama kama watanzania wa sasa hivi.
Ni nini kimetufika? au ni nini tumelishwa?
Nina imani ni Mungu peke yake atatukomboa kutoka kwenye jinamizi hili. Na Mungu ameshaanza toka aliposhuka kuja kusimama risasi arobaini zisiweze kutoa uhai wa kiumbe chake alionyesha nia ya kutukomboa. Kwa wenye ufahamu kidogo wanatakiwa wawe macho sana na hali hii. Ukipingana na mpango wa Mungu utapata kipigo kutoka kwake. Na usiombee au ulizia yaliyompata firauni na jeshi lake alipojaribu kuzuia msafara ukielekea nchi ya ahadi. Beware!!
 
Ahaha mwimbo mbaya haimbiwi mtoto kuna dalili kubwa izirael akaanzia segerea akamalizia belgium kulingana na ramli yako
Taarifa za kinabii zinaeleza kwamba kila aliyehusika na njama za shambulio la lissu atakufa kabla yake , maono yanaonyesha kwamba mwaka huu pekee watakufa watano , hawa wote wana maradhi ya muda mrefu
 
Back
Top Bottom