Kwa wanaofuatilia mwenendo wa siasa zetu na kile kinachoendelea kwenye michezo hasa klabu ya simba watakubaliana nami kwamba sasa siasa za Awamu ya tano rasmi zimehamia klabu ya simba.
Kufuatia mabadiliko ya uendeshaji klabu, Simba ilifanya mabadiliko ya katiba yake na kuruhusu uwekezaji kwa mmiliki atakayepewa baada ya uongozi kuamua. Kuna uitaratibu wa mmiliki kupata hisa ya asilimia 49 na wanachama asilimia 51.
Kwa takribani miezi miwili hivi kumeibuka sintofahamu huko na kinachoendelea kinaonekana Serikali imeingilia kati sasa kwenye klabu ya simba.
KAULI YA MZEE KILOMONI.
Huyu mzee ameibuka na kauli mpya kwamba sasa yeye akiwa mwenyekiti wa Baraza la wadhamini anamtaka Mo mmiliki wa klabu amtafute na ampe msimamo wa serikali kwamba wawekezaji wanatakiwa wawe watatu ambao ndio watagawana hizo asilimia 49 za hisa unaotokana na uwekezaji wao.
Wiki mbili zilizopita alisikika Mo akisema anahujumiwa na wasaidizi wake, sasa unatoka msimamo wa serikali kupitia kwa Kilomoni. Hii ni siasa kwenye klabu ya simba.
MASWALI YA KUJIULIZA
Nani kamtuma kilomoni kutoa msimamo wa serikali wakati klabu ya Simba inaongozwa na Katiba yake iliyowapa nguvu wanachama kuamua mambo yao?
Jee Msimamop huo umezingatia uwekezaji ambao umeshafanywa na Mo hadi sasa kiasi cha kuchomekewa ajenda mpya ya umiliki wa utatu kwenye hisa za muwekezaji jee huku si kumuhujumu Mo na klabu ya simba?
Kwa nini Serikali imejiingiza sasa wakati uwekezaji umeshaanza kufanyika huku si kufanya hadaa ili muwekezaji apate hasara za mamilioni pale atakapoamua kujiondoa au kuendelea na uekezaji?
Kuna dhamira gani hapa ?
KUTUMIKA KWA MZEE KILOMONI.
Kuna kikao chochote cha baraza la wadhamini kukutana na kupitisha maazimio? na kama kimefanyika kimezingatia misingi ya uwekezaji ambao tayari imefanywa. Kuna suala la utawala na mawasiliano ya ndani kwa nini Mzee Kilomoni anakuja kwenye Media? Hapa kuna nini?
HITIMISHO.
Kuna kila dalili kuwa sasa siasa za Magufuli zimeingia Simba na Mo ni mlengwa. Katika hali hio tusitarajie ufanisi wa michezo ambao tulikuwa tunaona mwanga kupitia klabu ya simba. Serikali itafute njia sahihi za kuingilia mambo ili kuepusha vurumai na mikanganyiko.
Nyuma ya sakata la Mzee Kilomoni kuna siasa zimepenyezwa Simba na zitaathiri sekta ya michezo nchini.
Kama kauli ya Kilomoni ni kweli basi Serikali ya Rais Magufuli haitaepuka kuhusishwa na hujuma kwa Mwekezaji wa simba na klabu yenyewe.
Kishada
Kufuatia mabadiliko ya uendeshaji klabu, Simba ilifanya mabadiliko ya katiba yake na kuruhusu uwekezaji kwa mmiliki atakayepewa baada ya uongozi kuamua. Kuna uitaratibu wa mmiliki kupata hisa ya asilimia 49 na wanachama asilimia 51.
Kwa takribani miezi miwili hivi kumeibuka sintofahamu huko na kinachoendelea kinaonekana Serikali imeingilia kati sasa kwenye klabu ya simba.
KAULI YA MZEE KILOMONI.
Huyu mzee ameibuka na kauli mpya kwamba sasa yeye akiwa mwenyekiti wa Baraza la wadhamini anamtaka Mo mmiliki wa klabu amtafute na ampe msimamo wa serikali kwamba wawekezaji wanatakiwa wawe watatu ambao ndio watagawana hizo asilimia 49 za hisa unaotokana na uwekezaji wao.
Wiki mbili zilizopita alisikika Mo akisema anahujumiwa na wasaidizi wake, sasa unatoka msimamo wa serikali kupitia kwa Kilomoni. Hii ni siasa kwenye klabu ya simba.
MASWALI YA KUJIULIZA
Nani kamtuma kilomoni kutoa msimamo wa serikali wakati klabu ya Simba inaongozwa na Katiba yake iliyowapa nguvu wanachama kuamua mambo yao?
Jee Msimamop huo umezingatia uwekezaji ambao umeshafanywa na Mo hadi sasa kiasi cha kuchomekewa ajenda mpya ya umiliki wa utatu kwenye hisa za muwekezaji jee huku si kumuhujumu Mo na klabu ya simba?
Kwa nini Serikali imejiingiza sasa wakati uwekezaji umeshaanza kufanyika huku si kufanya hadaa ili muwekezaji apate hasara za mamilioni pale atakapoamua kujiondoa au kuendelea na uekezaji?
Kuna dhamira gani hapa ?
KUTUMIKA KWA MZEE KILOMONI.
Kuna kikao chochote cha baraza la wadhamini kukutana na kupitisha maazimio? na kama kimefanyika kimezingatia misingi ya uwekezaji ambao tayari imefanywa. Kuna suala la utawala na mawasiliano ya ndani kwa nini Mzee Kilomoni anakuja kwenye Media? Hapa kuna nini?
HITIMISHO.
Kuna kila dalili kuwa sasa siasa za Magufuli zimeingia Simba na Mo ni mlengwa. Katika hali hio tusitarajie ufanisi wa michezo ambao tulikuwa tunaona mwanga kupitia klabu ya simba. Serikali itafute njia sahihi za kuingilia mambo ili kuepusha vurumai na mikanganyiko.
Nyuma ya sakata la Mzee Kilomoni kuna siasa zimepenyezwa Simba na zitaathiri sekta ya michezo nchini.
Kama kauli ya Kilomoni ni kweli basi Serikali ya Rais Magufuli haitaepuka kuhusishwa na hujuma kwa Mwekezaji wa simba na klabu yenyewe.
Kishada