Sasa nimeujua ukweli, nakihama chama cha mapinduzi

Mkorosai

Member
Nov 17, 2010
65
0
Nilijiunga na chama cha mapinduzi baada ya kumaliza shule nikiwa na matumaini makubwa na chama changu, nimeendelea kuishi kwa matumaini nikijua kuwa matatizo yaliyoko hapa nchini yanatokana na mfumo mbaya wa dunia. Nilikuwa naviogopa vyama vya upinzani kama ukoma nikjua kuwa ni wababaishaji na watu wanaotafuta ulaji na umaarufu tu.

Sasa nimebaini kuwa wana CCM wengi tunaishi katika dunia ya uoga, hatuwezi kuzungumza mawazo yetu na tunamuogopa sana mwenyekiti wetu kama vile yeye ni mungu mdogo. tunaishi katika kivuli cha kugandamizwa na wala hakuna mahala tunapoweza kusikilizwa au kuwasikiliza viongozi wetu.

Kwa jinsi uchaguzi ulivyoendeshwa na kwa jinsi ambavyo CHADEMA wameonyesha kwa kumsusa Mwenyekiti wetu bila woga wala kumtusi mtu, nimeamini kuwa lolote lawezekana hata mimi naweza kuondoka ktk hiki chama na maisha yangu yakaendelea kama kawaida!

Nawaomba CHADEMA mnikaribishe kwenye chama chenu, mnipatie maelekezo namna ya kupata kadi ya chama chenu ili niwakabidhi hii niliyo nayo ya CCM. Mimi naishi Tabata nafanya kazi kwenye taasisi ya umma hapa Dar.
 
Hongera ndugu.Kujiunga upinzani ni haki ya raia. C.C.M kimepoteza mwelekeo na hakina jambo jipya. Ikiwa umegundua maovu ya C.C.M basi jaribu na kuwaelimisha na wengine. Chama pekee kinachoelekea kuleta maendeleo ya kweli ktk nchi hii ni CHADEMA pekee. Hivyo tukiunge mkono.
 
Mkuu karibu sana na UKOMBOZI UMETIMIA KUWA MMOJA WAPO WA KUIOKOA NCHI YAKO TOKA MIKONONI MWA MAFISADI!
 
Pole kwa kuchelewa kuijua taswira halisi ya CCM!!:A S crown-1:
 
Nilijiunga na chama cha mapinduzi baada ya kumaliza shule nikiwa na matumaini makubwa na chama changu, nimeendelea kuishi kwa matumaini nikijua kuwa matatizo yaliyoko hapa nchini yanatokana na mfumo mbaya wa dunia. Nilikuwa naviogopa vyama vya upinzani kama ukoma nikjua kuwa ni wababaishaji na watu wanaotafuta ulaji na umaarufu tu.

Sasa nimebaini kuwa wana CCM wengi tunaishi katika dunia ya uoga, hatuwezi kuzungumza mawazo yetu na tunamuogopa sana mwenyekiti wetu kama vile yeye ni mungu mdogo. tunaishi katika kivuli cha kugandamizwa na wala hakuna mahala tunapoweza kusikilizwa au kuwasikiliza viongozi wetu.

Kwa jinsi uchaguzi ulivyoendeshwa na kwa jinsi ambavyo CHADEMA wameonyesha kwa kumsusa Mwenyekiti wetu bila woga wala kumtusi mtu, nimeamini kuwa lolote lawezekana hata mimi naweza kuondoka ktk hiki chama na maisha yangu yakaendelea kama kawaida!

Nawaomba CHADEMA mnikaribishe kwenye chama chenu, mnipatie maelekezo namna ya kupata kadi ya chama chenu ili niwakabidhi hii niliyo nayo ya CCM. Mimi naishi Tabata nafanya kazi kwenye taasisi ya umma hapa Dar.

Ulikuwa kweli m-CCM? Na uko serious au ni mamluki unataka kuja kupata siri Chadema. Hebu sema namba yako ya kadi ya sisiem. Mana usije ukawa kama kishongo sijui kisongo na mbwembwe. Baada ya hayo mi nakutakia kila la kheri ila uwe critical kwa kila step unayofanya maishani mwako ili usijilaumu laumu. Mana mziki wa chadema sio wa kitoto.
 
karibu sana lakini endelea kutoa elimu kwa wananchi wanofikiri kuwa bila ccm hawezi kuishi kaa ukijua kuwa siku chadema ikiunda serikali na kuchua hatamu ya uongozi kwa nafasi ya urais, wananchi wa tabaka la chini na kati watafarijika sana. Ndipo watakapokuja na maneno haya KWANINI HATUCHUKUA MAAMUZI MAPEMA YA KUCHAGUA CHADEMA. THE TIME HAS COME LET US DO CHANGES.
 
KARIBU SAAAAAAAAAANA MKUU..........ni swala zaidi la mabadiliko ya kifikra yenye kuleta maendeleo kwa watu wote katika nyanja zote muhimu......karibu tena karibu sana
 
nashukuru kwa mialiko yenu na kunikaribisha, nami nawaahidi kuwa bega kwa bega na ninyi kuwaambia wenzangu kuwa muda wa kuogopa ogopa na kusujudia Viongozi ambao wako madarakani hata kama ni kwa hila, umekwisha. Nfikiri tanzania yenye watu wajisiri ndiyo imeisha piga hodi sasa. Mimi nami nataka kuwa mmoja wa watu jasiri katika taifa langu.

Lakini ndugu zangu hamjanielekeza nifanye taratibu gani au nimuone nani ili kujiunga na chama hiki! Kadi niliyo nayo ya kijani sasa siitaki nataka kuikabidhi kwa kamanda yeyote wa CHADEMA.
 
Tafuta tawi la chadema lililo karibu nawe, pata semina kidogo kisha chukua kadi ya uanachama. Karibu!
 
Huku maeneo ya Tabata ninakoishi sijawahi kuona tawi la CHADEMA wala simjui kiongozi yeyote wa chama hiki. Naomba mnisaidie ili nijue pa kwenda na ikiwezekana uchaguzi mdogo wa jimbo la Segerea unaokuja mimi nami nihesabiwe ktk kura za mgombea wa CHADEMA. Nimejua ujinga wa CCM, sasa siwezi kuendelea kuishi kwa propaganda tu!
 
Waweza baki bila chama pia ukipigania mgombea binafsi agenda

Hilo nalo neno, lakini naona kama CHADEMA ina mvuto wa kutosha, maana wamethubutu kumwambia Mwenyekiti wa CCM tena kwa unyenyekevu kuwa kuna matatizo mahala fulani na wakamuonyesha kuwa wana nguvu angalau za kuacha kumsikiliza!
 
Hongera kwa kufahamu kuwa ulikuwa umepotea njia na karibu sana Chadema.
Itakuwa jambo njema sana kama kabla yakujiunga/wakati wakujiunga umeweza kuwashawishi familia yako/waliokaribu wewe kama sehemu tu ya kupima uelewa wako na sababu ya kwanini unahamia Chadema na kuacha CCM, huu utakuwa mtihani mzuri ili kujijenga kama mwana Chama imara na asiyeyumba na ambaye anaweza kuleta mabadiliko.
Karibu karibu tena Chadema mwambie na mwenzako.
 
Karibu Mkolosai CHADEMA ni chama makini, kinafuata kanuni, na ilani ya chama imetulia haina ubaguzi.
 
Back
Top Bottom