Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,991
Katika Jamii zetu kuna imani mbalimbali zilizojengeka, mfano kuhusu Mnyama anaitwa KAKAKUONA, ndege anayeitwa BUNDI, na mdudu anaitwa KUNGUNI. Kakakuona akionekana huwa ni habari kubwa, na haminiwa kwamba ana uwezo wa kutoa ubashiri wa mambo yajayo. Bundi akionekana mahali huaminiwa kwamba ni ishara kwamba kuna jambo baya litatokea muda si mrefu. na mtu ukiambiwa una DAMU YA KUNGUNI, maana yake unaandamwa na lawama na kukataliwa na jamii bila sababu. Tatizo lako ni hiyo damu ya kunguni uliyonayo!
Hivi karibuni, tarehe 29 Januari 2019, tulipata taarifa kwamba Bundi alionekana katika bunge letu. Spika Job Ndugai alipotoa taarifa hiyo, alisisitiza kwamba Bundi ni ndege wa kawaida. lakini tarehe 6 Februari 2019, siku ya Mahakama, Rais Magufuli alimshauri Spika Ndugai apeleke viongozi wa dini wakaombee bunge ili asionekane tena. Inaonekana jambo hili lilimtisha Rais Magufuli. taarifa ya kuonekana Bundi ilijadiliwa sana kwenye mitandao ya jamii wakati huo, baada ya hapo maisha yakaendelea, watanzania kila mtu akipambana na hali yake.
Kufuatia matukio ya hivi karibuni, hususan uamuzi wa Bunge letu kupitisha azimio kutofanya kazi na CAG, pamoja na maamuzi mengine yaliandamana na uamuzi huo, likiwemo kuwafungia wabune Halima Mdee na Godbless Lema kuhudhuria mikutano ya bunge kwa muda tofauti, na pia vitendo mbalimbali vya kujenga chuki, vya dharau kwa watu mbalimbali. Hapa naongelea maneno ya kejeli aliyoongea Spika Job Ndugai, pale alipoamua kuongelea suala la Godbless Lema kujibizana na Naibu Spika, na kufikia hatua ya kutaja madeni ya Godbless Lema anayodaiwa, na kudai kwamba ndiyo sababu ya kumfanya aonekane kama "amechanganyikiwa". Kufuatia matukio yote hayo, nimetafakari sana tukio lile la Bundi kuonekana Bungeni.
Kwanza ni mara ya kwanza kusikia Bundi kaingia bunge letu, bila kukaribishwa kama alivyoalikwa Pierre Liquid na wengineo kabla yake. lakini pia ni mara ya kwanza bunge letu kupitisha azimio la aina hii, la kukataa kufanya kazi na CAG. kwa mujibu wa waliomnukuu spika wa zamani Pius Msekwa, uamuzi wa aina hii haujawahi onekana popote duniani. kwa hiyo tukubaliane kwamba hili pia ni tukio la pekee. Pia ni mara yangu ya kwanza kusikia mtu wa hadhi kama Job Ndugai kupandwa na ghadhabu na kutaja madeni ya mtu aliye chini yake akiwa na lengo la kumdhalilisha, na kumbe anajidhalilisha mwenyewe.
Siamini saana habari za bundi kuhusishwa na imani mbalimbali, lakini kwa hili, naomba kuweka tofauti. kwa hili tukio la bundi kuonekana bungeni na matukio haya ambayo yametikisa nchi na kutuingiza kwenye mgogoro wa kikatiba, nadhani Bundi alikuwa na ujumbe maalum kwa watanzania. Bundi alikuwa anatahadharisha kuhusu mambo mabaya yatakayotokea kupitia katika huo ukumbi wa bunge. Pamoja na Spika Ndugai kubeza uwepo wa bundi, na pia kubeza ushauri wa Magufuli wa kuleta viongozi wa dini waje kufanya maombi, mambo hayo mabaya kabisa yametokea.
Watanzania tusiache mambo haya kama yalivyo. tusimwachie CAG peke yake, au kuwaachia vyama vya upinzani peke yao. tunaona nguvu kubwa zinazotumika "kuwashughulikia" wale wanaoonekana kuunga mkono waziwazi kauli na msimao wa CAG. Watanzania kwa umoja wetu tujitokeze kupinga maamuzi haya ya kibabe, yaliyopitishwa na wabunge wa CCM, waliolewa madaraka na kujisahau kwamba wanatumikia wananchi. Mtumishi wa kweli wa wananchi, ni CAG na vyama vya upinzani.
Hivi karibuni, tarehe 29 Januari 2019, tulipata taarifa kwamba Bundi alionekana katika bunge letu. Spika Job Ndugai alipotoa taarifa hiyo, alisisitiza kwamba Bundi ni ndege wa kawaida. lakini tarehe 6 Februari 2019, siku ya Mahakama, Rais Magufuli alimshauri Spika Ndugai apeleke viongozi wa dini wakaombee bunge ili asionekane tena. Inaonekana jambo hili lilimtisha Rais Magufuli. taarifa ya kuonekana Bundi ilijadiliwa sana kwenye mitandao ya jamii wakati huo, baada ya hapo maisha yakaendelea, watanzania kila mtu akipambana na hali yake.
Kufuatia matukio ya hivi karibuni, hususan uamuzi wa Bunge letu kupitisha azimio kutofanya kazi na CAG, pamoja na maamuzi mengine yaliandamana na uamuzi huo, likiwemo kuwafungia wabune Halima Mdee na Godbless Lema kuhudhuria mikutano ya bunge kwa muda tofauti, na pia vitendo mbalimbali vya kujenga chuki, vya dharau kwa watu mbalimbali. Hapa naongelea maneno ya kejeli aliyoongea Spika Job Ndugai, pale alipoamua kuongelea suala la Godbless Lema kujibizana na Naibu Spika, na kufikia hatua ya kutaja madeni ya Godbless Lema anayodaiwa, na kudai kwamba ndiyo sababu ya kumfanya aonekane kama "amechanganyikiwa". Kufuatia matukio yote hayo, nimetafakari sana tukio lile la Bundi kuonekana Bungeni.
Kwanza ni mara ya kwanza kusikia Bundi kaingia bunge letu, bila kukaribishwa kama alivyoalikwa Pierre Liquid na wengineo kabla yake. lakini pia ni mara ya kwanza bunge letu kupitisha azimio la aina hii, la kukataa kufanya kazi na CAG. kwa mujibu wa waliomnukuu spika wa zamani Pius Msekwa, uamuzi wa aina hii haujawahi onekana popote duniani. kwa hiyo tukubaliane kwamba hili pia ni tukio la pekee. Pia ni mara yangu ya kwanza kusikia mtu wa hadhi kama Job Ndugai kupandwa na ghadhabu na kutaja madeni ya mtu aliye chini yake akiwa na lengo la kumdhalilisha, na kumbe anajidhalilisha mwenyewe.
Siamini saana habari za bundi kuhusishwa na imani mbalimbali, lakini kwa hili, naomba kuweka tofauti. kwa hili tukio la bundi kuonekana bungeni na matukio haya ambayo yametikisa nchi na kutuingiza kwenye mgogoro wa kikatiba, nadhani Bundi alikuwa na ujumbe maalum kwa watanzania. Bundi alikuwa anatahadharisha kuhusu mambo mabaya yatakayotokea kupitia katika huo ukumbi wa bunge. Pamoja na Spika Ndugai kubeza uwepo wa bundi, na pia kubeza ushauri wa Magufuli wa kuleta viongozi wa dini waje kufanya maombi, mambo hayo mabaya kabisa yametokea.
Watanzania tusiache mambo haya kama yalivyo. tusimwachie CAG peke yake, au kuwaachia vyama vya upinzani peke yao. tunaona nguvu kubwa zinazotumika "kuwashughulikia" wale wanaoonekana kuunga mkono waziwazi kauli na msimao wa CAG. Watanzania kwa umoja wetu tujitokeze kupinga maamuzi haya ya kibabe, yaliyopitishwa na wabunge wa CCM, waliolewa madaraka na kujisahau kwamba wanatumikia wananchi. Mtumishi wa kweli wa wananchi, ni CAG na vyama vya upinzani.