Sasa ni zamu ya Urusi kuokoa raia wao katika mji wa Kharson, Ukrean inapania kuchukua jimbo la Kharson lilonyakuliwa na mavamizi

5525

JF-Expert Member
Apr 6, 2014
5,412
6,273
C89B0046-856C-4D1A-B66E-E0411F7FFA3D.jpeg

Maelfu ya raia na maafisa walioteuliwa na Urusi wanahamishwa kutoka eneo la kusini mwa Ukraine la Kherson kabla ya mashambulizi ya Ukraine, anasema kiongozi wa eneo hilo aliyewekwa rasmi na Urusi.

Vladimir Saldo alisema raia 50-60,000 wataondoka katika miji minne kwenye ukingo wa magharibi wa mto Dnieper kwa "kuhama kwa utaratibu".

Idara zote zilizoteuliwa na Urusi katika jiji la Kherson zingevuka mto pia. Picha za runinga za Urusi zilionesha baadhi ya watu wakikusanyika karibu na Dnieper.

Wakiwa kwenye foleni ya kupanda boti, haikufahamika ni wangapi waliokuwa wakiondoka. Uhamisho wa raia na mamlaka kutoka eneo linalochukuliwa kuwa uhalifu wa kivita.

Mshauri wa rais wa Ukraine, Mykhailo Podolyak alisema ilikuwa chini ya mwezi mmoja tangu Urusi ifanye sherehe ya kushirikiana na Kherson: "Ukweli unaweza kuumiza ikiwa unaishi katika ulimwengu wa kufikirika."

Jumatatu jioni, kamanda mpya wa jeshi la Urusi nchini Ukraine, Jenerali Sergei Surovikin, alielezea hali ilivyo ngumu katika mji wa Kherson.

Afisa aliyewekwa rasmi na Urusi, Kirill Stremousov, aliwaonya wakazi wa Kherson kwamba vikosi vya Ukraine vitaanzisha mashambulizi katika mji huo "katika siku za usoni".

"Hakuna mtu atakayerudi nyuma lakini pia tunataka kuokoa maisha yao," aliongeza.

Bwana Saldo, ambaye aliteuliwa kuwa gavana wa eneo hilo na Moscow, aliiambia TV ya Urusi kwamba hakuna mtu anayekaribia kujisalimisha, lakini "haifai" kwa wakazi kubaki katika jiji linalokabiliwa na hatua za kijeshi. "

"Katika siku mbili zilizopita, zaidi ya watu 5,000 wameondoka Kherson," alisema.

Mapema mwezi huu, naibu meya wa Kherson aliyehamishwa alisema ni wakazi 100,000 pekee waliobaki katika jiji la Kherson lenye wakazi 320,000 kabla ya vita.

Meya wa Melitopol iliyo chini ya Urusi, Ivan Fedorov, alionya kwamba raia wa Kherson wanakabiliwa na changamoto kama za kufukuzwa kwa nguvu na kunyimwa makazi yao ili Urusi ijaze jiji hilo na "askari na wasaliti".

Mwezi uliopita, Ukraine ilisema watu milioni 2.5 wamefukuzwa kwa lazima kutoka Ukraine hadi Urusi. Gavana huyo aliyeteuliwa na Urusi aliishutumu Ukraine kwa kujipanga kwa mashambulizi makubwa na kupanga kuharibu bwawa la Kakhovka kwenye Mto Dnieper, eneo ambalo lina mafuriko.
 
Ndugu ngoja tupeane siku tano tu utasikia ya kusikia huko.. urusi wanawajali watu wao wanataka wakae pembeni mahari salama kabla ya dhahama ya kamanda amagedoni....
Si mji wa kwanza Ukrain kurejesha kumbuka Lyman na ni mji muhimu huko donbas, Russia imeshindwa ku-retake

Hakuna hata mji mmoja Ukrain wamerejesha halaf mvamiz akauchukua tena, urusi saiv taaban nafsi zao hawana silaha hawana jeshi, hayo mashambulizi ya Kyiv juzi walikodi drons kutoka Iran na zimedondoshwa kibao, walifanikiwa kuua raia 19 na kuangusha majeng ya raia
 
Subiri ahamishe raia wake halafu uone huo mziki utakaofuata hapo. Watapigwa hadi wachakae
Urusi saiv wanashambuliwa baada ya kushambulia ni wazi Putin ameshindwa vita huwez vamia nchi ukashambulia half ngoma ikageuka na sasa lazima uelewe Ukrain hawatasimama hadi Moscow

Kumbuka Russia alipovamia alifika hadi makao makuu Kyiv, watu wakaingia porini kupiga kazi.

Sasa Kyiv russia ilishindwa akarud zake donbas ambako nako hakukaliki anarudishwa kwao Moscow ni aibu kubwa sana kwa huyu anayejiita super power
 
Putin akili nyingi sana... Mwisho wa siku raia wote wa Ukraine watamuona mwema kuliko Raisi wao Zele
Mkuu ni weye uliyeandika hivi?
Wamaanisha kuna siku raia wa ukrain wangeridhika ardhi yao na mipaka ya nchi iwe mali ya urusi?

Unaonaje huko kwenu Mlima Kilimanjaro Kenya waseme ni mali yao na uwe chini yao? Mama jeska angeliona tamu hili?
 
Huyo huyo anaetegemea ndege za Iran atampiga nani huyo? Wameshaikimbia miji waliyodai wameichukua, hovyo kabisa!
Kwasababu tu hujui, NATO wanachanganyikiwa kwanini hatumii arsenal yake anaamua kununua, usidhani hana akili.

Stock is full anasubiri NATO waingie ulingoni ndio ujue mziki wake.

Ndio maana toka hii OPS inanze westerners wanalalamika Russia anatumia silaha za zamani.

Can you imagined ile meli ya Russia ni ya miaka ya 1950's 😅😅😅
 
Mkuu ni weye uliyeandika hivi?
Wamaanisha kuna siku raia wa ukrain wangeridhika ardhi yao na mipaka ya nchi iwe mali ya urusi?

Unaonaje huko kwenu Mlima Kilimanjaro Kenya waseme ni mali yao na uwe chini yao? Mama jeska angeliona tamu hili?
Tatizo la Ukraine ni kuvunja mkataba wa minsk na kuwakaribusha wanazi mamboleo karibu na mipaka ya warusi. Sasa ile nchi itagawanywa kama ilivyo korea, au ujerumani zamani... Ukraine haitakua ile uliyokua unaifahamu... ni ukweli mchungu ila hatuna budi kuukubali.... nakaribisha tubishane.
 
Kwasababu tu hujui, NATO wanachanganyikiwa kwanini hatumii arsenal yake anaamua kununua, usidhani hana akili.

Stock is full anasubiri NATO waingie ulingoni ndio ujue mziki wake.

Ndio maana toka hii OPS inanze westerners wanalalamika Russia anatumia silaha za zamani.

Can you imagined ile meli ya Russia ni ya miaka ya 1950's 😅😅😅
kuna watu hawaelewi hiv vitu, stoke ya putin ni dam tupu NATO wamestukia mchezo😂
 
Back
Top Bottom