Sasa ni wazi,bila kadi ya chama Tawala cheo ktk Utumishi wa Umma ni ndoto

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,669
Leo Rais amehutubia Wakuu Wilaya na Wakurugenzi wa Wilaya,Miji na Majiji ndani ya Ikulu Dsm.Kabla ya kula kiapo na kupata semina toka Tume ya Maadili ya Utumishi wa Umma,viongozi hao wateule walipata wasaa wa kuhutubiwa na Waziri Mkuu,Makamu wa Rais,Rais,Kamishna wa Tume ya Maadili na baadae kabisa Waziri wa TAMISEMI.

Rais amesisitiza kuwa ataendelea kuchaguwa watu ambao ni "watii" kwa chama na serikali,amesisistiza kuwa hawezi kuchaguwa watu katika uongozi wa utumishi wa umma kwa hawaamini juu ya Chama cha Mapinduzi na sera ya chama hicho,kwani Serikali iliyopo ni ya chama cha Mapinduzi na wananchi walichaguwa chama hivho kushika dola.Hivyo mtu anayetaka kufanya kazi na utawala huu ajuwe anafanya kazi ya kutekeleza sera ya chama tawala iliyokabishiwa serikali.Ufafanuzi huu wa Rais umekuja baada ya malalamiko kuwa nafasi za U-DAS na DED zimejazwa na makada wa CCM,hivyo Rais alikuwa anasisitiza kuwa ni lazima achaguwe makada sababu ndio wanaoamini juu ya sera na ilani ya CCM.

Akijibu hoja ya uzoefu na maswala ya "Strategic Succesion Plan",Rais JPM amesema mambo ya "kurithishana" uongozi katika utumishi wa umma katika kipindi chake hayapo.Kwamba umekaa ofisini unajuwa kabisa akitoka fulani unafuata wewe hiyo haipo.Hivyo ofisi nyingi zenye mpango mkakati wa "succesion"(?) wauweke kando kwani leo Rais ameahidi kusafisha muundo wote wa watu kuanzia ngazi ya chini mpaka juu,na sasa ameanza juu na anasema atashuka mpaka chini kwenye mizizi kuhakikisha anaweka watu hata kama hawana uzoefu ili mradi wawe wanaendana na kasi yake na kuamini juu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Hakika wale watumishi wa umma wasio na kadi wala muelekeo wa kikada,ambao pengine kutokana na mfumo wa kanuni na taratibu za utumishi wa umma walitegemea "Strategic Succesion Plan" ili kutoka hapo walipo kwenda hatua nyingine,basi wavute subra kidogo.

Naye Waziri Angela Kairuki kapigilia msumari kwa kuwaagiza Wakurugenzi kushirikiana na Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwabaini watu wasioendana na kasi ya Serikali hii na wale wasio na muelekeo wa kutekeleza ilani ya CCM kuwekwa pembeni.Waziri Kairuki anasema huu si wakati wa kuwa "Vuguvugu",ni ama unakuwa Moto au baridi.Watumishi wote wa umma ni lazima wajue wapo pale kufuata matakwa ya ilani ya CCM,kweli mtumishi wa umma hutakiwi kuwa na chama,lkn kwa sasa wanatakiwa wajuwe wanatekeleza ilani na mwatakwa ya CCM,hivyo wawe na mkao wa ki-CCM na kama hawawezi basi wapishe nafasi au wasubiri chama kingine wanachoamani kina sera nzuri waje kuzitekeleza.

Kauli hizi ni kama zinauwa misnigi ya Utumishi wa umma,mipango ya uzoefu,succesion pamoja na Impartiality zinaanza kupotea katika utumishi wa umma.Sasa ni dhahiri wale watu walio "neutral" na wasioeleweka upande wa kisiasa katika utumishi wataisoma namba.

Tunajuwa Rais wetu mpendwa JPM ana nia nzuri juu ya nchi yetu,lakini hili la utumishi wa umma,tunaomba alitazamae upya.Uzoefu katika utumishi wa umma ni zaidi ya elimu,kumtoa mtu moja kwa moja Lumumba na kumkabishi Halmashauri ina mashara yake,kama si leo basi hako mbeleni.Kuudharau mfumo wa "Succesion Plan" katika utumishi wa umma si afya,na si kweli kuwa watumishi wote ni mafisadi.Tusiikatishe tamaa kada ya utumishi wa umma kwa makosa ya watu wachache
 
Usichanganye...kuwa mtii.wa.serekali.iliyo.madarakani ni wajibu wa mtumishi wa umma duniani kote..kuwa.na kadi ya chama ni kitu tofauti...watanzania wako 42 mlns..sio wote wana vyama
 
Kama unataka kuwa millionaire fanya biashara achana na kuajiriwa ni utumwa.Mabillionare mfano Mengi,Bakhresa na wengineo wengi hawakuajiriwa na serikali.Ukiwa na pesa wanakufuata wao.
Amsel (Amschel) Bauer Mayer Rothschild, 1838: "Let me issue and control a Nation's money and I care not who makes its laws".
"Money is power" achana na siasa uchwara kama R.Aziz.It's all about Benjamin.
 
unapotosha mkuu; wapo wanachama wa ccm zaidi ya milioni 5 na wote hawawezi kua viongozi; vile vile kulitumikia Taifa not necessarily kupata mamlaka. you can be a good citizen and a good believer of your chosen faith inatosha kabisa...
 
Mfumo wa chama kimoja huna kadi ya Ccm hutapata huduma ya serikali maana unaipinga serikali tutafika tu!
mentality ya siasa zetu ni uadui sio siasa za kizalendo; once we change that cursed behaviour then we shall move forward as a nation.
 
Unazuia siasa uku teuzi za watumishi wako nizakisiasa? Sasa unachotaka nini? Kwamba umetekeleza ilani ya chama chako na uchaguliwe tena 2020 pasipo upinzani? Huu ni woga na utoto kisiasa. Toka nje jifunze kuvumilia mawazo kinzani, after all we ni zao la mawzo kinzani la sivyo ungepata wapi u.r.a.i.s?
Mkuu umemaliza kote aisee, kashasahau.
 
Unazuia siasa uku teuzi za watumishi wako nizakisiasa? Sasa unachotaka nini? Kwamba umetekeleza ilani ya chama chako na uchaguliwe tena 2020 pasipo upinzani? Huu ni woga na utoto kisiasa. Toka nje jifunze kuvumilia mawazo kinzani, after all we ni zao la mawzo kinzani la sivyo ungepata wapi u.r.a.i.s?
Kabisa Una mawazo kama yangu ahsee, rais wa sasa alipata nafasi ya kupitishwa kugombea sbb ya nguvu ya upinzani,kwa hiyo upinzani umemsaidia kupata urais huo,lkn yeye anapousaliti na kuukandamiza anajipatia radhi ahsee.Kwa science ya kawaida wanaotumbuliwa kwa sasa kwa ufisadi mkubwa mkubwa lazima walikuwa wameunda mfumo wa kuendelea kuinyonya nchi hata mamlaka kuu zilikuwa zikiwalinda.Baada ya kuona wanachi wamechoka na wanaunga upinzani,na hatoki mtu,ndiyo wakampitisha yeye,ndiyo maana alijinadi yeye kama yeye na si chama.Sasa waliopika ile presha mpaka yeye akachaguliwa anatakiwa awathamini.

Anayeanzisha ubaguzi (uccm) na kuwabagua wengine hatodumu,hiyo ni PRINCIPLE YA MUNGU MWENYEWE,hata kwenye familia watoto 5 kama ni wa mama mmoja na kumbagua mmoja wa kambo,Yule mmoja anapata mibaraka na kufanikiwa katika maisha kuliko wale wengine.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom