Sasa ni wakati muafaka ''Brothe K'' Uchukue nafasi ya '' Mzee Majuto''

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,276
14,512
brother-k-wa-futuhi.jpg


Huyu jamaa japo hana muda mrefu kuliko hata wale wachekeshaji wa mizengwe, kwa mtazamo wangu ndiyo mchekeshaji pekee aliobaki mwenye uswezo wa kuvaa viatu vya mzee majuto.

hakuna cha
Jotii, mkandamizajo, mpoki, mkwele wana nani.

Brother K, kaza uzi fanya maboresho ututoe wabongo kwenye ulimwengu wa vichekesho.
 
nafasi ya Majuto hawezi chukua mtu kama hayo na hakuna wakuichukua
Majuto anaigiza kwa sauti yake halisi na unacheka, akilia unacheka, akitembea unacheka, akiongea unacheka, akicheka unacheka, majuto anavaa kawaida tu na unafurahi. Brother K hizo package hana na hatakuanazo
 
nafasi ya Majuto hawezi chukua mtu kama hayo na hakuna wakuichukua
Majuto anaigiza kwa sauti yake halisi na unacheka, akilia unacheka, akitembea unacheka, akiongea unacheka, akicheka unacheka, majuto anavaa kawaida tu na unafurahi. Brother K hizo package hana na hatakuanazo
akiweka vizuri package zake anatoka mkuu.
kwanza ni mvuto kwa watu hayo mengine ni maboresho tu.
huyu jamaa akitoka futuhi inakufa.
 
Mkuu Brother K ninamkubali lakini Joti mmmh ni Habari nyingine aiseee... Halafu Joti kila siku yuko kwenye Kiwango, kwa wale wanaomfahamu Joti toka kipindi kile wanaigiza kwenye tamthilia na mpoki ITV, NAFIKIRI wanaelewa nini namaanisha.
Ingia Youtube tafuta JOTI TV utaelewa maanisha nini!
JOTI anabadilika katika kila character kiufupi hatabiriki!!!
 
brother-k-wa-futuhi.jpg


Huyu jamaa japo hana muda mrefu kuliko hata wale wachekeshaji wa mizengwe, kwa mtazamo wangu ndiyo mchekeshaji pekee aliobaki mwenye uswezo wa kuvaa viatu vya mzee majuto.

hakuna cha
Jotii, mkandamizajo, mpoki, mkwele wana nani.

Brother K, kaza uzi fanya maboresho ututoe wabongo kwenye ulimwengu wa vichekesho.
Na katika mahojiano ya mwisho ya marehem majuto nakumbuka aliulizwa swali kuwa:ni mwigizaji gani unamkubali katika sanaa ya maigizo ambayo unaamini anaweza kuchukua mikoba yako:kwa kweli mzee majuto alimtaja huyo braza k.tena akasisitiza sana kuwa sanaa anaiweza na akiendelea hivyo atatoka
 
Na katika mahojiano ya mwisho ya marehem majuto nakumbuka aliulizwa swali kuwa:ni mwigizaji gani unamkubali katika sanaa ya maigizo ambayo unaamini anaweza kuchukua mikoba yako:kwa kweli mzee majuto alimtaja huyo braza k.tena akasisitiza sana kuwa sanaa anaiweza na akiendelea hivyo atatoka
asante mkuu.
 
Huyu jamaa namkubali sana. Anavaa uhalisia wa jambo mpaka unasahau kuwa unaangalia TV.
Binafsi ukimuondoa mzee Majuto huyu ndiye huwa naweza kumfuatilia.
Hao akina Joti huwa wanaigiza kuwa wanaigiza badala ya kuuvaa uhalisia.
 
smart and humble.
anajua maisha ya kawaida hivyo hata akiigiza maigizo au vichekesho vyake vinaakisi uhalisia.
kama ile movie "mzee kirungu" hata majuto kafunikwa.
Hapo kwenye humble nakubaliana na wewe
Jamaa anajijua kabisa kua ni mkali lakini bado anaishi vizuri tu na watu
Ila tatizo lake ni moja ,hana usimamizi mzuri na pia haweki kazi zake mitandaoni yani kwa kifupi hajawa kwenye ulimwengu wa teknolojia kiivo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom