papason
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 5,119
- 5,683
Hatimaye msimamo wa serikali juu ya kupeleka marekebisho ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii umeota mbawa rasmi baada ya kuthibitika rasmi mbele ya kamati ya kudumu ya maendeleo ya jamii ya Bunge iliyokutana na Kamati ya wafanyakazi wa migodini.
Imethibitika rasmi kuwa wizara ya kazi na ajira haijaandaa muswada huo, akitoa maelezo ya wizara mbele ya kamati katibu mkuu wa wizara hiyo ndugu shitindi amedai kwamba wizara ya kazi imejipanga kupeleka miscellaneous amendments kwa mwanasheria mkuu wa serikali badala ya kupeleka bungeni mswaada wa marekebisho ya sheria hiyo kandamizi iliyopitishwa na wabunge mwanzoni wa mwaka huu huko Dodoma. Pamoja na kubanwa kila kona na wanakamati wa wafanyakazi wa migodini, bwana shitindi alikomaa kibabe kabisa kwenye msimamo wa serikali kupitia wizara ya kazi na ajira ni kupeleka miscellaneous amendments kwa mwanasheria mkuu wa serikali na si vinginevyo!.
Katika amendments hiyo katibu mkuu alisema kifungu kitakachorekebishwa ni kile Na.44 cha sheria ya PPF ambacho ndo pekee kitaruhusu wanachama wa PPF kuchukua mafao yao. Wanachama wa mifuko mingine kama NSSF fao la kujitoa halitarudishwa kamwe! Na hivyo sheria hiyo kubaki kama ilivyo kwa wafanyakazi waliopo kwenye mifuko mingine kusubiri miaka 55 au 60 kuchukua mafao yao.
Mwanakamati mmoja wa wafanyakazi wa migodini alitaka kujua ni kwa nini wizara imekaidi kuandaa muswada wa sheria kama ilivyo pendekezwa na bunge lililopita badala yake inaleta miscellaneous ammendments, mpiganaji huyo aliishia kupigwa beat zito kabisa na katibu mkuu wa wizara ya kazi na ajira-Shitindi, tena huku akisaidiwa na baadhi ya wajumbe wa kamati ya kudumu ya maendeleo ya jamii ya bunge.
Kwa kweli wafanyakazi na hasa wa sekta binafsi tujilaumu wenyewe, kwa maana hatuku- ungana wala ufanya jitihada kubwa ktk kutetea fao hilo, tuliiamini serikali na kamati ya bunge ambao nao wametuingiza mjini rasmi!
Matumaini yetu yamebaki kwa wabunge wachache wa upinzani kututetea!
Lakini bado wafanyakazi tuna nafasi ya mwisho na hasa tukiitumia vizuri kabla ya kuanza bunge mwezi ujao!
Imethibitika rasmi kuwa wizara ya kazi na ajira haijaandaa muswada huo, akitoa maelezo ya wizara mbele ya kamati katibu mkuu wa wizara hiyo ndugu shitindi amedai kwamba wizara ya kazi imejipanga kupeleka miscellaneous amendments kwa mwanasheria mkuu wa serikali badala ya kupeleka bungeni mswaada wa marekebisho ya sheria hiyo kandamizi iliyopitishwa na wabunge mwanzoni wa mwaka huu huko Dodoma. Pamoja na kubanwa kila kona na wanakamati wa wafanyakazi wa migodini, bwana shitindi alikomaa kibabe kabisa kwenye msimamo wa serikali kupitia wizara ya kazi na ajira ni kupeleka miscellaneous amendments kwa mwanasheria mkuu wa serikali na si vinginevyo!.
Katika amendments hiyo katibu mkuu alisema kifungu kitakachorekebishwa ni kile Na.44 cha sheria ya PPF ambacho ndo pekee kitaruhusu wanachama wa PPF kuchukua mafao yao. Wanachama wa mifuko mingine kama NSSF fao la kujitoa halitarudishwa kamwe! Na hivyo sheria hiyo kubaki kama ilivyo kwa wafanyakazi waliopo kwenye mifuko mingine kusubiri miaka 55 au 60 kuchukua mafao yao.
Mwanakamati mmoja wa wafanyakazi wa migodini alitaka kujua ni kwa nini wizara imekaidi kuandaa muswada wa sheria kama ilivyo pendekezwa na bunge lililopita badala yake inaleta miscellaneous ammendments, mpiganaji huyo aliishia kupigwa beat zito kabisa na katibu mkuu wa wizara ya kazi na ajira-Shitindi, tena huku akisaidiwa na baadhi ya wajumbe wa kamati ya kudumu ya maendeleo ya jamii ya bunge.
Kwa kweli wafanyakazi na hasa wa sekta binafsi tujilaumu wenyewe, kwa maana hatuku- ungana wala ufanya jitihada kubwa ktk kutetea fao hilo, tuliiamini serikali na kamati ya bunge ambao nao wametuingiza mjini rasmi!
Matumaini yetu yamebaki kwa wabunge wachache wa upinzani kututetea!
Lakini bado wafanyakazi tuna nafasi ya mwisho na hasa tukiitumia vizuri kabla ya kuanza bunge mwezi ujao!