GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,052
- 107,528
Kama kuna Mtu ambaye nilikuwa nabisha na nakataa kabisa kuhusu ‘ Dhihaka ‘ za Watanzania wenye Akili nyingi dhidi ya Uelewa na Uwezo wa Maarifa aliyonayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul C. Makonda basi nilikuwa ni Mimi GENTAMYCINE ila kwa nilichokisikia leo na Mimi sasa rasmi nakubaliana na Watanzania wote hao.
Katika moja ya ‘ Promo ‘ ya Clouds fm hasa kuelekea katika Tamasha zima la leo la FIESTA Jijini Dar es Salaam Uwanja wa Uhuru ambayo aliifanya Mkuu wa Mkoa Paul C. Makonda amesikika ndani humo akisema kuwa Kesho tarehe 9 Disemba ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika na Tanzania Bara.
Yawezekana labda Watanzania wengi ( Mimi na Wewe ukimuondoa tu Mwerevu Paul Makonda ) tulisoma na Kufundishwa Somo la Historia na Walimu ‘ Wabovu ‘ kiasi kwamba muda wote tulipokuwa Darasani walikuwa wakituambia na kutufundisha kwamba tarehe 9 Disemba ni Siku ya Uhuru wa Tanzania ( ambao unazihusisha Tanzania Bara na Tanzania Visiwani ) wakati kumbe kwa Walimu ‘ Werevu ‘ na waliomfundisha ‘ Mwerevu ‘ Paul C. Makonda ( Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ) walimwambia kuwa kila tarehe 9 Disemba huwa ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika na Tanzania Bara.
Najua kuna Wale Watetezi wake hapa wenye ‘ Visokolokwinyo ‘ vingi watakuja na Kubisha na hata kusema kuwa ‘ naongopa ‘ au ‘ namsingizia ‘ na kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul C. Makonda hajatoa hilo ‘ Boko ‘ la Kufungia mwaka huu wa 2019 hivyo kwakuwa mara kwa mara Clouds fm wanarudia hiyo ‘ Promo ‘ yao ya FIESTA ambayo wamemrekodi Mkuu huyo wa Mkoa nawaomba muisikilize ili mjue ya kwamba huwa ‘ Sikurupuki ‘ pale nikileta ‘ Hoja ‘ hapa Jamvini.
Eti Kesho tarehe 9 Disemba ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika na Tanzania Bara. Hovyo kabisa pamoja na Cheo chako hicho!
Katika moja ya ‘ Promo ‘ ya Clouds fm hasa kuelekea katika Tamasha zima la leo la FIESTA Jijini Dar es Salaam Uwanja wa Uhuru ambayo aliifanya Mkuu wa Mkoa Paul C. Makonda amesikika ndani humo akisema kuwa Kesho tarehe 9 Disemba ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika na Tanzania Bara.
Yawezekana labda Watanzania wengi ( Mimi na Wewe ukimuondoa tu Mwerevu Paul Makonda ) tulisoma na Kufundishwa Somo la Historia na Walimu ‘ Wabovu ‘ kiasi kwamba muda wote tulipokuwa Darasani walikuwa wakituambia na kutufundisha kwamba tarehe 9 Disemba ni Siku ya Uhuru wa Tanzania ( ambao unazihusisha Tanzania Bara na Tanzania Visiwani ) wakati kumbe kwa Walimu ‘ Werevu ‘ na waliomfundisha ‘ Mwerevu ‘ Paul C. Makonda ( Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ) walimwambia kuwa kila tarehe 9 Disemba huwa ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika na Tanzania Bara.
Najua kuna Wale Watetezi wake hapa wenye ‘ Visokolokwinyo ‘ vingi watakuja na Kubisha na hata kusema kuwa ‘ naongopa ‘ au ‘ namsingizia ‘ na kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul C. Makonda hajatoa hilo ‘ Boko ‘ la Kufungia mwaka huu wa 2019 hivyo kwakuwa mara kwa mara Clouds fm wanarudia hiyo ‘ Promo ‘ yao ya FIESTA ambayo wamemrekodi Mkuu huyo wa Mkoa nawaomba muisikilize ili mjue ya kwamba huwa ‘ Sikurupuki ‘ pale nikileta ‘ Hoja ‘ hapa Jamvini.
Eti Kesho tarehe 9 Disemba ni Siku ya Uhuru wa Tanganyika na Tanzania Bara. Hovyo kabisa pamoja na Cheo chako hicho!