Sasa ni dhahiri, nchi imo kwenye tatizo la umeme

Wimana

JF-Expert Member
Jun 28, 2012
2,449
717
Wadau, kwa hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme ilivyo hapa Jijini Arusha, ni wazi kuwa Tanzania kwa sasa tumo kwenye tatizo kubwa la umeme. Tangu wiki hii ianze, kila siku umeme unakatika, majuzi eneo la Njiro umeme ulikatwa hadi usiku kabisa. Juzi umeme ulikatwa katikati ya mji kwa siku nzima, jana eneo la Themi halikuwa na umeme siku nzima, leo huku Njiro wamekata asubuhi na hadi sasa hawajarudisha na kwa siku zote hizo hawakutoa taarifa yoyote!

Kwa miezi ya Juni hadi Novemba nimekuwa huko Kilombero mjini Ifakara. Kwa muda huo wote umeme ulikuwa ukikatwa siku za Jumanne na Alhamisi, na wakazi wote wa Ifakara wanajua juu ya 'mgao huo' ambao haukuwahi kutangazwa!

Hivi kwa nini Wizara, Tanesco na Serikali zimekaa kimya bila kutoa taarifa rasmi ili tujipange namna ya kuishi bila umeme? Tutendeeni haki jamani.
 
Mimi kitaani kwnagu nimekinukisha haiwezekani kama vipi waje wangoe mita yao na hatutaki kuonan nguzo zenu za umeme wangoe waondoke nazo.

Mpigie simu bosi wao 0767042009 mkurugenzi wao alisema usipouona umeem mumpigie.
 
Mi naichukia Tanesco kuliko Shetani. Wanatufanyia mgao kinyemela na kama haitoshi wanatuletea Volts 160 badala ya 220. Pumbaf kbs.
 
Umeme hamna, Arushani mgao kila kona kama leo 19/12/13 hakuna umeme sehemu kubwa ya Ar mjini sasa huko vijijini ndiyo sijui hali ikoje.
 
Mi naichukia Tanesco kuliko Shetani. Wanatufanyia mgao kinyemela na kama haitoshi wanatuletea Volts 160 badala ya 220. Pumbaf kbs.

Volts pungufu 60 tutaomba Kenya kupitia Namanga! He he he.
 
Waziri wake naye si yupo kwenye mawaziri mzigo?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Chagua ccm tena toka urais, ubunge, udiwani. Rais kikwete yuko busy angani kama popo, badala ya kutumikia watu wake!
 
Thread za maana kama hizi haziwezi pata watu... watu wako bize na thread za Mwigulu kumuonea wivu Mbowe..... kuchagua CCM ni kuchagua Mauti

inasemekana Mgao wa umeme ni sera ya ccm , hivyo usitegemee buku 7 kuja kupinga hili .
 
mi nishalalamika sana,hata leo hapa kahama ni magenereta tu mara wakate mara warudishe,nasubiri sanduku la kura 2015
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom