Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,470
- 215,289
Imefahamika sasa kwamba kazi ya Kitume inayofanywa na Chadema ya kusajili wanachama wake kwa njia ya kisasa iitwayo Chadema Digital ni kama MHURI WA MOTO, ni alama isiyofutika, iko kama chanjo ya NDUI, kila anayejisajili anahisi kama sasa ndio kapewa Uraia wa Tanzania.
Njama zote za kishamba za kuzuia wenye kumbi za mikutano kuwapa kumbi hizo Chadema zimegonga mwamba, na zimeshindwa kuzuia mafuriko ya wananchi kujitokeza kusajiliwa, tunazo taarifa za wenye kumbi kupewa vitisho ambapo wameelezwa kwamba atakayeruhusu Chadema Digital kwenye ukumbi wake atapewa kesi ya Uhujumu Uchumi ama utakatishaji pesa.
Wilaya ya Kyela ni miongoni mwa maeneo kulikotolewa onyo hili, ambako CHADEMA DIGITAL ilifanyika kwenye Ukumbi wa MUNGU, chini ya miti na kufanikiwa kwa kishindo. Nachukua nafasi hii kuwapongeza Wenye kumbi za mikutano waliopuuza Vitisho na kukubali Chadema digital kwenye kumbi zao, wala hawana haja ya kuogopa, kwa vile hakuna mahali popote kwenye dunia tuliyomo ambako SHETANI aliwahi kumshinda Mungu.
Maeneo mengine walikozuiliwa waliamua kufanyia usajili kwenye Kolido na kwenye vichochoro vya wazi, lakini zoezi hili halijawahi kukwama na halitasimama, Gari lishawaka, Pisha njia.
Njama zote za kishamba za kuzuia wenye kumbi za mikutano kuwapa kumbi hizo Chadema zimegonga mwamba, na zimeshindwa kuzuia mafuriko ya wananchi kujitokeza kusajiliwa, tunazo taarifa za wenye kumbi kupewa vitisho ambapo wameelezwa kwamba atakayeruhusu Chadema Digital kwenye ukumbi wake atapewa kesi ya Uhujumu Uchumi ama utakatishaji pesa.
Wilaya ya Kyela ni miongoni mwa maeneo kulikotolewa onyo hili, ambako CHADEMA DIGITAL ilifanyika kwenye Ukumbi wa MUNGU, chini ya miti na kufanikiwa kwa kishindo. Nachukua nafasi hii kuwapongeza Wenye kumbi za mikutano waliopuuza Vitisho na kukubali Chadema digital kwenye kumbi zao, wala hawana haja ya kuogopa, kwa vile hakuna mahali popote kwenye dunia tuliyomo ambako SHETANI aliwahi kumshinda Mungu.
Maeneo mengine walikozuiliwa waliamua kufanyia usajili kwenye Kolido na kwenye vichochoro vya wazi, lakini zoezi hili halijawahi kukwama na halitasimama, Gari lishawaka, Pisha njia.