yule mzee mkewe anamtesa sana, kabadilisha hadi itikadi na msimamo kisa the 2nd wife..laahBora umekiri Dr. Slaa alikubali kuingia kwenye mfuko wenu, natumai wale wasiosikia sasa atleast wataanza kuelewa kwamba Dr. Slaa alifika bei ya CCM wakamchukua.
Hoja imesimama kwa miguu kumi na 12 na imepita mkuuKwa wasionifahamu (angalau kwa ufahamu wa humu JamiiForums), mimi ni kada kindakindaki wa CCM. Nimejiunga na chama hiki miaka ya mwanzoni mwa 80 baada tu ya kuhitimu shahada yangu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Nilisomea sheria. Nikafanya kazi chamani, serikalini na hata kwenye vyombo vya ulinzi na usalama. Naijua nchi hii vyema, hasa kisiasa, ilipotoka-ilipo-na inapokwenda.
Katika utumishi wangu chamani, nimeshiriki kupanga na kutekeleza mipango mingi ya kisiasa. Mipango ya ushindi yenye na isiyo na ushindani. Mipango ya sirini iliyokwenda kutekelezwa sirini na hadharani. Mipango iliyoibakisha CCM madarakani kuanzia uchaguzi wa mwaka 1995 hata sasa. Kuanzia kurejeshwa kwa vyama vingi mwaka 1995, CCM imekuwa ikilenga vyama au chama pinzani chenye nguvu na ku-deal nacho.
Kwa mwaka 1995, NCCR-Mageuzi ililengwa na kusambaratishwa. Mwaka 2000 na 2005 ilikuwa zamu ya CUF. Kuanzia mwaka 2010 hadi sasa, CHADEMA imekuwa target ya CCM kisiasa. Imekuwa mpinzani wa karibu na wa kuharibu wa CCM uchaguzini, uraiani na hata maishani. Wapo makada waliokuwa wakiamini kuwa ili kuisambaratisha CHADEMA, ni lazima kuwasambaratisha viongozi wake. Kuwafanya wasiwe wamoja na hata kucheza na mmojammoja.
Hakika, CCM tulifanikiwa kwa Dr. Slaa na viongozi/wanachama waandamizi wa CHADEMA wengineo. Walinyoosha mikono na kujiunga nasi. Wakabaki akina Mbowe, Lissu, Lema na wengineo. Kazi ikaendelea. Iliendelea katika imani ya kuwa wakidhibitiwa na kumalizwa nguvu zao za kisiasa (zikiwemo na za kiuchumi) CHADEMA itasawajika na kusambaratika kwelikweli. Ilikuwa IMANI POTOFU.
Kama mkongwe wa kisiasa na kiserikali, nimejiridhissha kuwa CHADEMA si viongozi. Ni IMANI inayoishi ndani ya wanachama, wapenzi na mashabiki wao. CHADEMA imejitengeneza katika falsafa ya kiuanaharakati. falsafa ya kupambania usawa, haki, mshikamano, amani na utulivu. Imani hukaa moyoni na rohoni mwa watu. Ni ngumu kuichomoa huko. Wale makada wa CCM waliokuwa wakiamini katika kushughulika na viongozi ili kuidhibiti CHADEMA, sasa wamejiunga nami niliyekuwa nikipingana nao tangu mwanzo.
Sasa wamekuwa wafuasi wa msimamo wangu kuwa siasa ni kushindanisha na kuonesha sera na utekelezaji wake. Katika kuonesha mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, hakuna haja ya kutumika kwa Polisi au chombo chochote cha ulinzi kufanikisha hilo. Kitu halisi huonekana kiurahisi sana. Aliyekuwa Mwenyekiti wetu Mzee Jakaya Kikwete aliwahi kutuusia kuwa tusitegemee polisi hata katika kubishana kwa hoja.
Lakini, bado wapo makada wengi ambao bado wanaamini kuwa CHADEMA ni Mbowe, Lissu na viongozi wengine. Bado wanaamini kuwa 'muunganiko wa tangu enzi' wa CCM na vyombo vya usalama ni nguzo na nyenzo ya ushindi wa chama. Bado wanaamini katika siasa kale za kutumia ulaghai, wizi wa kura, mabavu na vitisho kubaki madarakani-eti tubaki kuwa chamadola. Wanajidanganya.
Utafika wakati, vyombo vya ulizi na usalama vitatamani kusikia kwanza sera bila hela na kushawishiwa na ahadi bila zawadi. Vitatamani kuona ushindani wa nje na ndani ya uwanja wa kisiasa kabla ya kuelendelea kulinda maslahi ya nchi badala ya chama. Vitatuacha solemba tukilia na kusaga meno. Tuoneshe maendeleo na maendeleo yaseme tukiwa tuko kimya. Na, imani ya wananchi kwa upinzani itapungua kwa kasi.
Wasiojulikana sasa wamejulikana?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Lakini sio bila kuwepo TUME HURUKifikiria wa matumbo zaidi kuliko kichwa kama wanacho lkini ndo kinasababisha hayo yote wako radhi kupindisha mambo kwa kuwasifia viongozi katika maamuzi yasiyo na maana yoyote ili matumbo yao yajae...nio Arusha kwa Sasa...kwa hii Hali ninayoiona kisiasa na kiuchumi vyama vya upinzani wakizichanga karata zao vizuri 2025. Wabunge wa upinzani wataingi wengi Sana bungeni
AmenNakuunga mkono kwa maana kuwa mimi nijiunga Tanu mwaka 1968 na CCM mwaka 1977 nimesoma shule nzuri. Mchango wangu kuelekea uamuzi wa CCM kukubali sera ya vyama vingi upo. Nyerere alikuwa binadamu mwenye elimu, hekima, busara na upeo wa hali ya juu Kila kiongozi angekuwa anafikiria mbali na siyo tumbo lake, matumbo ya ndugu au rafiki zake tungekuwa mbali sana. Nyerere alijali sana damu ya mtu.
Tujifunze namna ya kuendesha nchi kistaarabu. Hata Simba na Yanga hawapotezi viongozi wa timu pinzani, wanatafuta wachezaji bora ili kushinda msimu husika.Tanzania ni Taifa kubwa tukiwa pamoja. Hili siyo Taifa la kujifunza kutoka Rwanda au Uganda. Tuwe na aibu tusifanye mambo ya ovyo. Historia itatusuta. Nakushukuru sana kwa andiko lako.
Ndiyo kwanza wafuasi wao wamejazwa ges muda ukifika andiko lako litapata majibuKingai, Aziz, Goodluck, Mahita na Jumanne ndo wale wasiojulikana makada wa CCM tawi la dola. Hawa watu wametuharibia Sana CCM. Wanajali matumbo Yao na ya viongozi kuliko maslahi ya Taifa. Imani ya kuikataa CCM na viashiria vyake vyote ni kubwa Sana mtaani. Kuwashughulikia viongozi wa chadema ni sawa na kujilisha upepo.
Leo umekuwa muwazi kweli. Heshima kwako mkuu.Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Hapana.Walianza mapema kuonesha nia zao toka awamu ya tano ilipoingia madarakani jambo hili likapata nguvu..
"Iwapo wapinzani watasusia"?Na iwapo wapinzani watasusia chaguzi zote iwapo hakuna mabadiliko ya tume ya uchaguzi na katiba mpya, vituo vya kura havitakuwa na wapiga kura tena hasa vijana, kwani
Lakini pamoja na maneno hayo mazuri, polisi bado waliendelea kuwa tawi muhimu la chama hata wakati huo. Rejea RPC Kamuhanda alivyokuwa akishughulikia wapinzani, hadi kifo cha yule mwandishi kulipuliwa na bomu la kutoa machozi na kuuliwa!
Eti kuna watu wanamfananisha Nyerere na Jiwe 😡Nakuunga mkono kwa maana kuwa mimi nijiunga Tanu mwaka 1968 na CCM mwaka 1977 nimesoma shule nzuri. Mchango wangu kuelekea uamuzi wa CCM kukubali sera ya vyama vingi upo. Nyerere alikuwa binadamu mwenye elimu, hekima, busara na upeo wa hali ya juu Kila kiongozi angekuwa anafikiria mbali na siyo tumbo lake, matumbo ya ndugu au rafiki zake tungekuwa mbali sana. Nyerere alijali sana damu ya mtu.
Tujifunze namna ya kuendesha nchi kistaarabu. Hata Simba na Yanga hawapotezi viongozi wa timu pinzani, wanatafuta wachezaji bora ili kushinda msimu husika.Tanzania ni Taifa kubwa tukiwa pamoja. Hili siyo Taifa la kujifunza kutoka Rwanda au Uganda. Tuwe na aibu tusifanye mambo ya ovyo. Historia itatusuta. Nakushukuru sana kwa andiko lako.
huyo ndiye Vua nkuvue ametema checheKwa wasionifahamu (angalau kwa ufahamu wa humu JamiiForums), mimi ni kada kindakindaki wa CCM. Nimejiunga na chama hiki miaka ya mwanzoni mwa 80 baada tu ya kuhitimu shahada yangu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Nilisomea sheria. Nikafanya kazi chamani, serikalini na hata kwenye vyombo vya ulinzi na usalama. Naijua nchi hii vyema, hasa kisiasa, ilipotoka-ilipo-na inapokwenda.
Katika utumishi wangu chamani, nimeshiriki kupanga na kutekeleza mipango mingi ya kisiasa. Mipango ya ushindi yenye na isiyo na ushindani. Mipango ya sirini iliyokwenda kutekelezwa sirini na hadharani. Mipango iliyoibakisha CCM madarakani kuanzia uchaguzi wa mwaka 1995 hata sasa. Kuanzia kurejeshwa kwa vyama vingi mwaka 1995, CCM imekuwa ikilenga vyama au chama pinzani chenye nguvu na ku-deal nacho.
Kwa mwaka 1995, NCCR-Mageuzi ililengwa na kusambaratishwa. Mwaka 2000 na 2005 ilikuwa zamu ya CUF. Kuanzia mwaka 2010 hadi sasa, CHADEMA imekuwa target ya CCM kisiasa. Imekuwa mpinzani wa karibu na wa kuharibu wa CCM uchaguzini, uraiani na hata maishani. Wapo makada waliokuwa wakiamini kuwa ili kuisambaratisha CHADEMA, ni lazima kuwasambaratisha viongozi wake. Kuwafanya wasiwe wamoja na hata kucheza na mmojammoja.
Hakika, CCM tulifanikiwa kwa Dr. Slaa na viongozi/wanachama waandamizi wa CHADEMA wengineo. Walinyoosha mikono na kujiunga nasi. Wakabaki akina Mbowe, Lissu, Lema na wengineo. Kazi ikaendelea. Iliendelea katika imani ya kuwa wakidhibitiwa na kumalizwa nguvu zao za kisiasa (zikiwemo na za kiuchumi) CHADEMA itasawajika na kusambaratika kwelikweli. Ilikuwa IMANI POTOFU.
Kama mkongwe wa kisiasa na kiserikali, nimejiridhissha kuwa CHADEMA si viongozi. Ni IMANI inayoishi ndani ya wanachama, wapenzi na mashabiki wao. CHADEMA imejitengeneza katika falsafa ya kiuanaharakati. falsafa ya kupambania usawa, haki, mshikamano, amani na utulivu. Imani hukaa moyoni na rohoni mwa watu. Ni ngumu kuichomoa huko. Wale makada wa CCM waliokuwa wakiamini katika kushughulika na viongozi ili kuidhibiti CHADEMA, sasa wamejiunga nami niliyekuwa nikipingana nao tangu mwanzo.
Sasa wamekuwa wafuasi wa msimamo wangu kuwa siasa ni kushindanisha na kuonesha sera na utekelezaji wake. Katika kuonesha mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, hakuna haja ya kutumika kwa Polisi au chombo chochote cha ulinzi kufanikisha hilo. Kitu halisi huonekana kiurahisi sana. Aliyekuwa Mwenyekiti wetu Mzee Jakaya Kikwete aliwahi kutuusia kuwa tusitegemee polisi hata katika kubishana kwa hoja.
Lakini, bado wapo makada wengi ambao bado wanaamini kuwa CHADEMA ni Mbowe, Lissu na viongozi wengine. Bado wanaamini kuwa 'muunganiko wa tangu enzi' wa CCM na vyombo vya usalama ni nguzo na nyenzo ya ushindi wa chama. Bado wanaamini katika siasa kale za kutumia ulaghai, wizi wa kura, mabavu na vitisho kubaki madarakani-eti tubaki kuwa chamadola. Wanajidanganya.
Utafika wakati, vyombo vya ulizi na usalama vitatamani kusikia kwanza sera bila hela na kushawishiwa na ahadi bila zawadi. Vitatamani kuona ushindani wa nje na ndani ya uwanja wa kisiasa kabla ya kuelendelea kulinda maslahi ya nchi badala ya chama. Vitatuacha solemba tukilia na kusaga meno. Tuoneshe maendeleo na maendeleo yaseme tukiwa tuko kimya. Na, imani ya wananchi kwa upinzani itapungua kwa kasi.
Wasiojulikana sasa wamejulikana?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
umejidanganya kijinga sana !Chadema inafanywa kama ilivyofanywa CUF na hautokuja amini hizo iman kama zitaendelea kuwepo.
wapuuzi haoEti kuna watu wanamfananisha Nyerere na Jiwe 😡