Sasa ni dhahiri kuwa CHADEMA si Mbowe, Dr. Slaa, Lissu wala Lema. CHADEMA ni imani na haitakufa kirahisi!

Bora umekiri Dr. Slaa alikubali kuingia kwenye mfuko wenu, natumai wale wasiosikia sasa atleast wataanza kuelewa kwamba Dr. Slaa alifika bei ya CCM wakamchukua.
 
Nasikia Dr. yupo town kuisambaratisha CDM kwa mara ya pili.
 
Bora umekiri Dr. Slaa alikubali kuingia kwenye mfuko wenu, natumai wale wasiosikia sasa atleast wataanza kuelewa kwamba Dr. Slaa alifika bei ya CCM wakamchukua.
yule mzee mkewe anamtesa sana, kabadilisha hadi itikadi na msimamo kisa the 2nd wife..laah

wengi alikuwa ni mentor wetu ila baada ya hapo tukaona mzee kakengeuka.
 
Kuhusu Chadema kuwa ni itikadi na falsafa ya haki, amani, na upendo uliojengeka miongoni mwa watanzania nakubaliana nawe.

Kwa ule ushahidi unaotolewa mahakamani na kina Adamoo na wenzake, uminywaji wa haki unaofanywa na jaji wa ile kesi, vinazidi kuipandisha juu Chadema.

Inshort CCM wanaendelea kuzidi kuifanya Chadema ipate wafuasi kila siku, ndio maana licha ya zuio la mikutano ya siasa, na CCM wakiendelea kuzurura nchi nzima peke yao bado Chadema inaendelea kuwasumbua kila dakika.
 
Kwa wasionifahamu (angalau kwa ufahamu wa humu JamiiForums), mimi ni kada kindakindaki wa CCM. Nimejiunga na chama hiki miaka ya mwanzoni mwa 80 baada tu ya kuhitimu shahada yangu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Nilisomea sheria. Nikafanya kazi chamani, serikalini na hata kwenye vyombo vya ulinzi na usalama. Naijua nchi hii vyema, hasa kisiasa, ilipotoka-ilipo-na inapokwenda.

Katika utumishi wangu chamani, nimeshiriki kupanga na kutekeleza mipango mingi ya kisiasa. Mipango ya ushindi yenye na isiyo na ushindani. Mipango ya sirini iliyokwenda kutekelezwa sirini na hadharani. Mipango iliyoibakisha CCM madarakani kuanzia uchaguzi wa mwaka 1995 hata sasa. Kuanzia kurejeshwa kwa vyama vingi mwaka 1995, CCM imekuwa ikilenga vyama au chama pinzani chenye nguvu na ku-deal nacho.

Kwa mwaka 1995, NCCR-Mageuzi ililengwa na kusambaratishwa. Mwaka 2000 na 2005 ilikuwa zamu ya CUF. Kuanzia mwaka 2010 hadi sasa, CHADEMA imekuwa target ya CCM kisiasa. Imekuwa mpinzani wa karibu na wa kuharibu wa CCM uchaguzini, uraiani na hata maishani. Wapo makada waliokuwa wakiamini kuwa ili kuisambaratisha CHADEMA, ni lazima kuwasambaratisha viongozi wake. Kuwafanya wasiwe wamoja na hata kucheza na mmojammoja.

Hakika, CCM tulifanikiwa kwa Dr. Slaa na viongozi/wanachama waandamizi wa CHADEMA wengineo. Walinyoosha mikono na kujiunga nasi. Wakabaki akina Mbowe, Lissu, Lema na wengineo. Kazi ikaendelea. Iliendelea katika imani ya kuwa wakidhibitiwa na kumalizwa nguvu zao za kisiasa (zikiwemo na za kiuchumi) CHADEMA itasawajika na kusambaratika kwelikweli. Ilikuwa IMANI POTOFU.

Kama mkongwe wa kisiasa na kiserikali, nimejiridhissha kuwa CHADEMA si viongozi. Ni IMANI inayoishi ndani ya wanachama, wapenzi na mashabiki wao. CHADEMA imejitengeneza katika falsafa ya kiuanaharakati. falsafa ya kupambania usawa, haki, mshikamano, amani na utulivu. Imani hukaa moyoni na rohoni mwa watu. Ni ngumu kuichomoa huko. Wale makada wa CCM waliokuwa wakiamini katika kushughulika na viongozi ili kuidhibiti CHADEMA, sasa wamejiunga nami niliyekuwa nikipingana nao tangu mwanzo.

Sasa wamekuwa wafuasi wa msimamo wangu kuwa siasa ni kushindanisha na kuonesha sera na utekelezaji wake. Katika kuonesha mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, hakuna haja ya kutumika kwa Polisi au chombo chochote cha ulinzi kufanikisha hilo. Kitu halisi huonekana kiurahisi sana. Aliyekuwa Mwenyekiti wetu Mzee Jakaya Kikwete aliwahi kutuusia kuwa tusitegemee polisi hata katika kubishana kwa hoja.

Lakini, bado wapo makada wengi ambao bado wanaamini kuwa CHADEMA ni Mbowe, Lissu na viongozi wengine. Bado wanaamini kuwa 'muunganiko wa tangu enzi' wa CCM na vyombo vya usalama ni nguzo na nyenzo ya ushindi wa chama. Bado wanaamini katika siasa kale za kutumia ulaghai, wizi wa kura, mabavu na vitisho kubaki madarakani-eti tubaki kuwa chamadola. Wanajidanganya.

Utafika wakati, vyombo vya ulizi na usalama vitatamani kusikia kwanza sera bila hela na kushawishiwa na ahadi bila zawadi. Vitatamani kuona ushindani wa nje na ndani ya uwanja wa kisiasa kabla ya kuelendelea kulinda maslahi ya nchi badala ya chama. Vitatuacha solemba tukilia na kusaga meno. Tuoneshe maendeleo na maendeleo yaseme tukiwa tuko kimya. Na, imani ya wananchi kwa upinzani itapungua kwa kasi.

Wasiojulikana sasa wamejulikana?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Hoja imesimama kwa miguu kumi na 12 na imepita mkuu
 
Kifikiria wa matumbo zaidi kuliko kichwa kama wanacho lkini ndo kinasababisha hayo yote wako radhi kupindisha mambo kwa kuwasifia viongozi katika maamuzi yasiyo na maana yoyote ili matumbo yao yajae...nio Arusha kwa Sasa...kwa hii Hali ninayoiona kisiasa na kiuchumi vyama vya upinzani wakizichanga karata zao vizuri 2025. Wabunge wa upinzani wataingi wengi Sana bungeni
Lakini sio bila kuwepo TUME HURU
 
Nakuunga mkono kwa maana kuwa mimi nijiunga Tanu mwaka 1968 na CCM mwaka 1977 nimesoma shule nzuri. Mchango wangu kuelekea uamuzi wa CCM kukubali sera ya vyama vingi upo. Nyerere alikuwa binadamu mwenye elimu, hekima, busara na upeo wa hali ya juu Kila kiongozi angekuwa anafikiria mbali na siyo tumbo lake, matumbo ya ndugu au rafiki zake tungekuwa mbali sana. Nyerere alijali sana damu ya mtu.

Tujifunze namna ya kuendesha nchi kistaarabu. Hata Simba na Yanga hawapotezi viongozi wa timu pinzani, wanatafuta wachezaji bora ili kushinda msimu husika.Tanzania ni Taifa kubwa tukiwa pamoja. Hili siyo Taifa la kujifunza kutoka Rwanda au Uganda. Tuwe na aibu tusifanye mambo ya ovyo. Historia itatusuta. Nakushukuru sana kwa andiko lako.
Amen
 
Ukweli ni mchungu sana... bado sijaona uvccm wakija na kusema kuwa umechanganyikiwa na unazeeka vibaya wewe mzee.. utaambiwa pumzika ule mafao yako siasa hii haikuhusu na hujui kitu.. na bado utaambiwa unaoayuka payuka... hawachelewi watasema unaumwa ugonjwa wa akili na n.k.

Binafsi napenda sana mtu anaejipambanua kwa kusema ukweli... ukweli unatabia sawa sawa na haki... haki hubaguwa watu vivyo hivyo na ukweli utenganisha watu.
Ukweli haufutiki milele hata kama unafichwa kiasi gani na haki haipotei kamwe hata kama aliekunyang'anya ananguvu kama tembo au simba huko polini.
Siipendi kesi hii ya ugaidi toka inaanza mpaka sasa.
Japo naamini kwa wale ccm maslahi kama alivyosema mzee TUPA TUPA. Wao hawajisikii vibaya wanachotaka ni zamu yao ifike na sio ikatikie njiani.
Walianza mapema kuonesha nia zao toka awamu ya tano ilipoingia madarakani jambo hili likapata nguvu..
Kesi na kupotezana kwa kupitia ushauri wa uongo.. mnukuu hayati JPM akiwa anatoa husia kwenye msiba wa MAALIMU SEIF.
Nukuu isiyo rasmi " Nilikuwa nakataliwa kukutana nae na kuambiwa ni mtu mbaya sana na kumbe sio kweli nimekaa naye kwa muda mfupi ni mtu mwenye mawazo mazuri yenye kujenga nchi na kwa kweli alikuwa mwenye kuipenda na kuwapenda sana wazanzibari na Tanzania kwa ujumla"

Kwa kifupi ukiwa kiongozi ogopa kurithi maadui ambao uliwakuta wakiwa na ugomvi na watangulizi wako.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Kingai, Aziz, Goodluck, Mahita na Jumanne ndo wale wasiojulikana makada wa CCM tawi la dola. Hawa watu wametuharibia Sana CCM. Wanajali matumbo Yao na ya viongozi kuliko maslahi ya Taifa. Imani ya kuikataa CCM na viashiria vyake vyote ni kubwa Sana mtaani. Kuwashughulikia viongozi wa chadema ni sawa na kujilisha upepo.
Ndiyo kwanza wafuasi wao wamejazwa ges muda ukifika andiko lako litapata majibu
 
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Leo umekuwa muwazi kweli. Heshima kwako mkuu.

Andiko lako linastahili 'rejoinder' yenye nguvu za hoja. Pengine tutapata muda na nguvu kuitendea haki mada yako hii mhimu huko mbele ya safari.

Kuna watu, tuliipenda sana CCM kikiwa chama cha wakulima na wafanya kazi; sasa kimekuwa chama ambacho ni adui mkubwa wa taifa letu! CCM kimegeuka kujiona kuwepo kwacho ni muhimu zaidi kuliko uwepo wa taifa letu, ndiyo maana wamejiingiza kwenye kulihujumu taifa hili.

Nyinyi wanachama wachache mliobaki huko mnaoona udhaifu huu wa chama chenu mmeshindwa kuwa na msaada wa kubadili mwelekeo wa chama chenu huko ndani kwa ndani; kwa hiyo iliyobaki ni hukumu ya wananchi tu, na wala siyo hukumu ya vyombo vya ulinzi wala taasisi zingine zilizotekwa na chama chenu ziwatumikie nyinyi.

Pamoja na kusema CHADEMA si viongozi, lakini ukweli ni kwamba bila ya uwepo wa hao wachache waliokataa kuisujudia CCM, chama hicho kingesambaratika vibaya na lengo la CCM lingetimia.

Sasa hivi uwepo wa Mbowe, Lissu. Msigwa, Sugu. Henche, Mnyika na wengi wengine inawezekana isiwe muhimu sana kama ilivyokuwa huko nyuma kwa vile wananchi wa nchi hii hata wasiokuwa wanachama wa chama chochote cha siasa wametambua uovu wa CCM, na wapo tayari kushirikiana na vyama kama CHADEMA kuiondoa CCM bila kujali ni nani anakiongoza chama hicho, kama ilivyokuwa huko siku za nyuma; mradi tu viongozi hao wawe na uwezo wa kuwaunganisha wananchi kutimiza wajibu wao wa kuilinda nchi yao dhidi ya adui huyu mkubwa CCM.

Hawa viongozi ni lazima wawepo ndani ya CHADEMA kuweza kuendesha harakati hizi mpya za ukombozi wa nchi yetu.
 
Chadema inafanywa kama ilivyofanywa CUF na hautokuja amini hizo iman kama zitaendelea kuwepo.
 
Walianza mapema kuonesha nia zao toka awamu ya tano ilipoingia madarakani jambo hili likapata nguvu..
Hapana.
Hujuma zilianza toka zamani, hata Kikwete kwa njia zake kahujumu upinzani kwa kiasi kikubwa. Mkapa naye hivyo hivyo, hata kama haikuwa kwa kiasi kilichoonekana wakati wa Magufuli.
 
Na iwapo wapinzani watasusia chaguzi zote iwapo hakuna mabadiliko ya tume ya uchaguzi na katiba mpya, vituo vya kura havitakuwa na wapiga kura tena hasa vijana, kwani
"Iwapo wapinzani watasusia"?
Nashukuru kwamba huko mwishoni umerekebisha kauli hii...,"Hivyo CCM ijiandae kung'olewa madarakani kwa machafukoivyo"

Sioni kamwe ni kwa jinsi gani chama kama CHADEMA kitashiriki tena uchaguzi wa aina yoyote ile bila ya uwepo wa Tume huru ya Uchaguzi.
 
CCM siku waweke uchaguzi wa majaribio wapime kina cha maji kwa miguu. Naamini siku iyo ndio itakua siku ya zama
 
Nakuunga mkono kwa maana kuwa mimi nijiunga Tanu mwaka 1968 na CCM mwaka 1977 nimesoma shule nzuri. Mchango wangu kuelekea uamuzi wa CCM kukubali sera ya vyama vingi upo. Nyerere alikuwa binadamu mwenye elimu, hekima, busara na upeo wa hali ya juu Kila kiongozi angekuwa anafikiria mbali na siyo tumbo lake, matumbo ya ndugu au rafiki zake tungekuwa mbali sana. Nyerere alijali sana damu ya mtu.

Tujifunze namna ya kuendesha nchi kistaarabu. Hata Simba na Yanga hawapotezi viongozi wa timu pinzani, wanatafuta wachezaji bora ili kushinda msimu husika.Tanzania ni Taifa kubwa tukiwa pamoja. Hili siyo Taifa la kujifunza kutoka Rwanda au Uganda. Tuwe na aibu tusifanye mambo ya ovyo. Historia itatusuta. Nakushukuru sana kwa andiko lako.
Eti kuna watu wanamfananisha Nyerere na Jiwe 😡
 
Kwa wasionifahamu (angalau kwa ufahamu wa humu JamiiForums), mimi ni kada kindakindaki wa CCM. Nimejiunga na chama hiki miaka ya mwanzoni mwa 80 baada tu ya kuhitimu shahada yangu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Nilisomea sheria. Nikafanya kazi chamani, serikalini na hata kwenye vyombo vya ulinzi na usalama. Naijua nchi hii vyema, hasa kisiasa, ilipotoka-ilipo-na inapokwenda.

Katika utumishi wangu chamani, nimeshiriki kupanga na kutekeleza mipango mingi ya kisiasa. Mipango ya ushindi yenye na isiyo na ushindani. Mipango ya sirini iliyokwenda kutekelezwa sirini na hadharani. Mipango iliyoibakisha CCM madarakani kuanzia uchaguzi wa mwaka 1995 hata sasa. Kuanzia kurejeshwa kwa vyama vingi mwaka 1995, CCM imekuwa ikilenga vyama au chama pinzani chenye nguvu na ku-deal nacho.

Kwa mwaka 1995, NCCR-Mageuzi ililengwa na kusambaratishwa. Mwaka 2000 na 2005 ilikuwa zamu ya CUF. Kuanzia mwaka 2010 hadi sasa, CHADEMA imekuwa target ya CCM kisiasa. Imekuwa mpinzani wa karibu na wa kuharibu wa CCM uchaguzini, uraiani na hata maishani. Wapo makada waliokuwa wakiamini kuwa ili kuisambaratisha CHADEMA, ni lazima kuwasambaratisha viongozi wake. Kuwafanya wasiwe wamoja na hata kucheza na mmojammoja.

Hakika, CCM tulifanikiwa kwa Dr. Slaa na viongozi/wanachama waandamizi wa CHADEMA wengineo. Walinyoosha mikono na kujiunga nasi. Wakabaki akina Mbowe, Lissu, Lema na wengineo. Kazi ikaendelea. Iliendelea katika imani ya kuwa wakidhibitiwa na kumalizwa nguvu zao za kisiasa (zikiwemo na za kiuchumi) CHADEMA itasawajika na kusambaratika kwelikweli. Ilikuwa IMANI POTOFU.

Kama mkongwe wa kisiasa na kiserikali, nimejiridhissha kuwa CHADEMA si viongozi. Ni IMANI inayoishi ndani ya wanachama, wapenzi na mashabiki wao. CHADEMA imejitengeneza katika falsafa ya kiuanaharakati. falsafa ya kupambania usawa, haki, mshikamano, amani na utulivu. Imani hukaa moyoni na rohoni mwa watu. Ni ngumu kuichomoa huko. Wale makada wa CCM waliokuwa wakiamini katika kushughulika na viongozi ili kuidhibiti CHADEMA, sasa wamejiunga nami niliyekuwa nikipingana nao tangu mwanzo.

Sasa wamekuwa wafuasi wa msimamo wangu kuwa siasa ni kushindanisha na kuonesha sera na utekelezaji wake. Katika kuonesha mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, hakuna haja ya kutumika kwa Polisi au chombo chochote cha ulinzi kufanikisha hilo. Kitu halisi huonekana kiurahisi sana. Aliyekuwa Mwenyekiti wetu Mzee Jakaya Kikwete aliwahi kutuusia kuwa tusitegemee polisi hata katika kubishana kwa hoja.

Lakini, bado wapo makada wengi ambao bado wanaamini kuwa CHADEMA ni Mbowe, Lissu na viongozi wengine. Bado wanaamini kuwa 'muunganiko wa tangu enzi' wa CCM na vyombo vya usalama ni nguzo na nyenzo ya ushindi wa chama. Bado wanaamini katika siasa kale za kutumia ulaghai, wizi wa kura, mabavu na vitisho kubaki madarakani-eti tubaki kuwa chamadola. Wanajidanganya.

Utafika wakati, vyombo vya ulizi na usalama vitatamani kusikia kwanza sera bila hela na kushawishiwa na ahadi bila zawadi. Vitatamani kuona ushindani wa nje na ndani ya uwanja wa kisiasa kabla ya kuelendelea kulinda maslahi ya nchi badala ya chama. Vitatuacha solemba tukilia na kusaga meno. Tuoneshe maendeleo na maendeleo yaseme tukiwa tuko kimya. Na, imani ya wananchi kwa upinzani itapungua kwa kasi.

Wasiojulikana sasa wamejulikana?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
huyo ndiye Vua nkuvue ametema cheche
 
Back
Top Bottom