Elections 2015 Sasa naanza kupata picha kwamba Apson Mwang'onda yupo kwa Lowassa kikazi zaidi...

Hapa nitoe pongezi kwa ndugu yetu Consigliere kwa maono ya mbali, naweza amini sasa upo ndani ya kampuni.

Mkuu nachelea kupokea pongezi zako sababu ya neno hili kwenye Kijani, ni taaluma na kazi za watu hizo. Mimi sijui hata 'a' yake inaandikwaje.
 
Jieleze vizuri. Mara unaunga unga kiingereza, mara kiswahili. Nyoosha lugha yako na maneno yako.
 
Au wewe ndiyo Pacha wa Pasco wa JF? Sijui mlioteshwa sawa au imetokea tu kama ya Sheick Kipozeo?

Nilishaongea na jamaa mmoja ambaye na yeye aliachwa kwenye mataa ya Apson. Huyu jamaa ni hatari sana.

Ukiangalia alivyokuwa karibu na Lowassa, alikuwa anajua kila kitu na nadhani hili walilitumia kumtisha Edo.

Sasa hivi atatengwa na wote maana kila mtu ataogopa kushikamana naye. CCM kuna unafiki sana.
Sinyooshi!!
 
Last edited by a moderator:
Nimeanza kuunganisha dots na kwa mbaali naiona picha kuwa kitendo cha Jasusi mkuu mstaafu wa nchi yetu kujiunga na kambi ya Lowasa kilikua ni cha kimkakati zaidi. Kwa wanaomfajamu Apson na utendaji wake tulijiuliza sana lakini tulikosa majibu.

Leo hii mara baada ya Edward kumaliza kufanya kampeni (Ninasisitiza kuwa ni kampeni na si kutangaza nia) yake pale uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ndipo nikazinduka na kutambua kuwa Apson alikua 'under cover' akiwa na jukumu maalum la kumdhoofisha Edward and Kingunge nailed it. Hili suala la magenge ya wasaka madaraka yaliyumbisha sana idara yetu ya usalama wa taifa kitu kilichopelekea idara hii kushutumiwa sana mitandaoni pia na makundi mbalimbali ya kijamii.

Ilikua si kazi rahisi kulimudu hili genge maana lilishajijenga vya kutosha na namna pekee ya kulisimamisha ilikua ni lazima the big man aingie in the war front and to begin with ilibidi ku step down then kujipenyeza ndani ya kambi hii ambapo na ku gain trust. Seems lengo la yeye kwenda front ilikua ni kulinda nguvu kazi ambazo idara hii ilikua ikizipoteza mara tu magenge haya yalipoona maslahi yao yanahatarishwa, (kujua zaidi unaweza ukarejea kingo za sakafu za mzee Kapinga na Daudi Mwakawago and others of a like zilipoishia).

Kwa kuwa magenge haya yanawakilisha maslahi mapana zaidi ya mataifa ya kigeni yanayoangalia namna ya kubena rasilimali zetu na yenye mitandao ya nguvu ya kijasusi, seems yali smell something fishy with Apson na hapo ndipo tukatangaziwa the return of The Kingmaker ambapo tukasikia kuwa Apson anawekwa kando (thou it was too late) kimtindo and the Kingmaker took over.

Kwa speech ya Edward na kila kitu kilichoendelea pale na kinachoendelea ndani ya kambi yake I can draw the conclusion kwamba the Game is Over. Ninaanza kupata hisia kuwa kutakuwa na transition kubwa zaidi mwaka huu.

Tanzania inarudi katika ubora wake, this is my country, I belong here. Hakika moyo wangu una furaha sana kuliko wakati wowote ndani ya miaka hii kumi. Si jambo dogo kuachia nafasi kubwa kama ile katika ofisi nyeti wakati muda ukiwa unamruhusu na kuamua kwenda under cover, hakika napata hisia idara yetu bado ingaki hai na nguvu na makali yake.

NB: Hizi ni hisia zangu baada ya kuunganisha dots kadhaa. Hazina uhusiano na taarifa yoyote rasmi. Unaweza ukawaza tofauti na kuwasilisha au kuchangia kwa namna yako mimi sitakuwa na cha kuongeza wala kupunguza.

huwezi ukabisha kuwa ww si sehemu ya hiyo Idara, nakumbuka nilikuwa mtu wa kwanza kusoma hii post nikiri niliona hili ni gumu kutokea kwa sababu ya nguvu alizokuwa nazo EL na mazingira halisi.
Ila kwa hali ilivyotokea DoDoma na hili andiko lako hakuna tofauti
na katika hili JK pamoja na mapungufu yake yote yaliyowahi tokea Watanzania wazalendo hawatamsahau kajijengea heshima kubwa sana kwa kitendo kile tu alichokifanya Juzi.
Ameonyesha kwamba yeyote yule atakaepewa cheo akafanya kazi kwa bidii, maarifa, na uzalendo bila ya kuwa na tamaa ya wizi,,, iko siku anaweza kuwa kiongozi mkubwa wa nchi hii.
 
Je mnaweza kutuambia kwa nini Wagombea Uraisi wa CCM kama ni Wakiristo basi wote ni Wakatoliki?
Je Jaji Augustino Ramadhani aliyesheheni ma CV kibao mchungaji wa Kanisa la Kiprotestanti imekuwaje amekatwa hata kwenye tano bora hayumo?
 
huwezi ukabisha kuwa ww si sehemu ya hiyo Idara, nakumbuka nilikuwa mtu wa kwanza kusoma hii post nikiri niliona hili ni gumu kutokea kwa sababu ya nguvu alizokuwa nazo EL na mazingira halisi.
Ila kwa hali ilivyotokea DoDoma na hili andiko lako hakuna tofauti
na katika hili JK pamoja na mapungufu yake yote yaliyowahi tokea Watanzania wazalendo hawatamsahau kajijengea heshima kubwa sana kwa kitendo kile tu alichokifanya Juzi.
Ameonyesha kwamba yeyote yule atakaepewa cheo akafanya kazi kwa bidii, maarifa, na uzalendo bila ya kuwa na tamaa ya wizi,,, iko siku anaweza kuwa kiongozi mkubwa wa nchi hii.

Mkuu, hayo mengine siyajui. Ila hili la juzi Kikwete alitaka awekee 'TV' yake pale Ikulu halafu astaafu na remort akiwa nayo yeye. Kikwete hana cha kujivunia, hata ukikutana naye ukampongeza atahisi unamng'ong'a tu na atakachokufanya hutataka kusimulia.
Ukweli ni kuwa Magufuli hakuwemo hata kwenye tano bora ya awali bali mashinikizo ya watu kuhoji na kutishia kuwang'oa wote wakianza na yeye ndipo Ben alipoicheza karata ya Magufuli. Kwa kifupi Kikwete anaondoka na machozi.
 
Back
Top Bottom