Nsame
JF-Expert Member
- Mar 12, 2012
- 477
- 123
Asalaam alaykum wanajamvi,
Ni mara yangu ya kwanza kushiriki kwa namna ya kutuma post mpya, nimekuwa nikishiriki kwa kusoma tu post za wanajf wengine, lkn sasa msaada wenu wa kimawazo unaweza kunisaidia nikajua ni jinsi gani naweza kufanya.
Kiufupi ni muda mfupi nimejipatia jiko baada ya kukaa kwa muda mwingi sana bila mke, nimejikusanya saana kwa muda mrefu na kwa kujibana ili nipate mke ambaye tutasaidiana kupata suluhisho la matatizo ya kimaisha, lakini sasa naona ndio kwanza matatizo yameongezeka, nimeoa kama mwezi mmoja uliopita na namshukuru mwenyezi Mungu mke wangu nampenda sana ila kikwazo kikubwa kinakuja upande wa wakwe zangu, nimekuwa nikisumbuliwa tangu siku ya pili kugunga ndoa kuwa natakiwa kuwajengea.
Mara ya kwanza nilifikiri labda ni utani wa mashemeji zangu wa kike maana ndiwo walianzisha maada hiyo lkn siku zinavyozidi kwenda napigiwa simu na watu waheshima sana kwangu [wakwe] na kusisitiza jambo hilo, nikajaribu kumueleza habari hizo mwandani wangu nikakuta naye anawaunga mkono, sina uwezo wa kifedha ni maisha ya kawaida saaaaana ambayo sioni sababu ya kukandamizwa kiasi hiki kwa kitu ambacho sii ridhaa yangu au kwa muda mfupi kiasi hiki? yaani kwakweli mpaka sasa nimekoswa furaha na ndoa yangu hata hamu ya kuwa karibu na mke wangu pia imetoweka.
Sasa ndugu zngu nishaurini maana mpaka sasa naanza kujuta kuoa sababu uwezo wa kuwatimizia kile wanacholazimisha kwasasa sina na pia inaonekana hawanielewi na utafikiri labda tulifunga nao mkataba huo.
Asanteni sana.
Ni mara yangu ya kwanza kushiriki kwa namna ya kutuma post mpya, nimekuwa nikishiriki kwa kusoma tu post za wanajf wengine, lkn sasa msaada wenu wa kimawazo unaweza kunisaidia nikajua ni jinsi gani naweza kufanya.
Kiufupi ni muda mfupi nimejipatia jiko baada ya kukaa kwa muda mwingi sana bila mke, nimejikusanya saana kwa muda mrefu na kwa kujibana ili nipate mke ambaye tutasaidiana kupata suluhisho la matatizo ya kimaisha, lakini sasa naona ndio kwanza matatizo yameongezeka, nimeoa kama mwezi mmoja uliopita na namshukuru mwenyezi Mungu mke wangu nampenda sana ila kikwazo kikubwa kinakuja upande wa wakwe zangu, nimekuwa nikisumbuliwa tangu siku ya pili kugunga ndoa kuwa natakiwa kuwajengea.
Mara ya kwanza nilifikiri labda ni utani wa mashemeji zangu wa kike maana ndiwo walianzisha maada hiyo lkn siku zinavyozidi kwenda napigiwa simu na watu waheshima sana kwangu [wakwe] na kusisitiza jambo hilo, nikajaribu kumueleza habari hizo mwandani wangu nikakuta naye anawaunga mkono, sina uwezo wa kifedha ni maisha ya kawaida saaaaana ambayo sioni sababu ya kukandamizwa kiasi hiki kwa kitu ambacho sii ridhaa yangu au kwa muda mfupi kiasi hiki? yaani kwakweli mpaka sasa nimekoswa furaha na ndoa yangu hata hamu ya kuwa karibu na mke wangu pia imetoweka.
Sasa ndugu zngu nishaurini maana mpaka sasa naanza kujuta kuoa sababu uwezo wa kuwatimizia kile wanacholazimisha kwasasa sina na pia inaonekana hawanielewi na utafikiri labda tulifunga nao mkataba huo.
Asanteni sana.