Sasa Magari yetu pendwa kurudi barabarani

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
6,825
9,528
Wale tuliopaki kwa hofu ya malimbikizo ya Road Licence sasa ikifika Tarehe Mosi Julai tunaingia barabarani CC Wamiliki wa:
1. Datsun
2. AWD (Bedfords)
3. Bettle
4. Volkswagen kombi
5. Mercedes Benz kv W123 Euro
6. NK
3090958985_7fe7b090b9.jpeg
index.jpeg
IMG-20170609-WA0001.jpg
IMG-20170609-WA0005.jpg
 
Hivi hii inamaana mtu aliyekuwa ame park labda sababu anadaiwa hiyo motorvehicle za nyuma inamaana ndo basi tena ikifika julai anatafuta bima tu au denu lipo palepale.. Maana kuna mtu aliniuliza hii kitu nika mute kwanza..
 
Hivi hii inamaana mtu aliyekuwa ame park labda sababu anadaiwa hiyo motorvehicle za nyuma inamaana ndo basi tena ikifika julai anatafuta bima tu au denu lipo palepale.. Maana kuna mtu aliniuliza hii kitu nika mute kwanza..
Deni limefutwa aka limesamehewa...
 
Mkuu Kama una deni unalipA kwanza ndo uingize muwa wako barabarani.
Hapana Mkuu kwa Mujibu wa Hotuba ya Bajeti jana inasema

"Sehemu ya 70(i) Mheshimiwa Supika napendekeza Marekebisho kwenye sheria ya Usalama Barabarani Sura 168 kama ifuatavyo;

Kufuta Ada ya Mwaka ya Leseni ya Magari ili ada hii ILIPWE MARA MOJA TU GARI LINAPOSAJILIWA NA BAADA YA HAPO IENDELEE KULIPWA KUPITIA USHURU WA BIDHAA KWENYE MAFUTA ya Petroli ,Dizeli na Taa kama ilivyoainishwa katika aya ya 69ii.

Aidha SERIKALI INATOA MSAMAHA WA KODI,RIBA NA ADHABU ZINAZOAMBATANA NA MADENI YOTE(Tax Amnesty) YA ADA HIYO YALIYOLIMBIKIZWA KWA MIAKA YA NYUMA" Kilichopo ni kwamba Ada ya Leseni ya Gari wakati wa usajili mara ya kwanza ndiyo itaongezeka kwa kuzingatia CC za gari husika MFANO:

CC: 501 HADI 1500 Ada itakuwa Laki Mbili badala ya Laki Unusu ya sasa
CC 1501 HADI 2500 Ada itafika Laki mbili Unusu tofauti na ya sasa laki 2
CC 2501 NA ZAIDI Itakuwa Laki Tatu
 
Mkuu Kama una deni unalipA kwanza ndo uingize muwa wako barabarani.
Kumbe madeni yanalipwa kwanza? Maana mimi roho imeniuma wiki iliyopita nimelipa 1,087,500 kodi ya kuanzia 2015 sasa niliposikia wamefuta nusu nilie kuwa ningejua ningesubiri. Ila kama watadai madeni ya nyuma kabla ya uamuzi huu nitajiona mjanja vinginevyo bado naugulia maumivu!
 
Imekaa poa sana... binafsi nadaiwa karibu m3 na pia kuna mtu aliniuzia gari likafa sikuwahi lipia lishafika 1M ananidai nimlipe so deni ndio lishakata
 
Hapana Mkuu kwa Mujibu wa Hotuba ya Bajeti jana inasema

"Sehemu ya 70(i) Mheshimiwa Supika napendekeza Marekebisho kwenye sheria ya Usalama Barabarani Sura 168 kama ifuatavyo;

Kufuta Ada ya Mwaka ya Leseni ya Magari ili ada hii ILIPWE MARA MOJA TU GARI LINAPOSAJILIWA NA BAADA YA HAPO IENDELEE KULIPWA KUPITIA USHURU WA BIDHAA KWENYE MAFUTA ya Petroli ,Dizeli na Taa kama ilivyoainishwa katika aya ya 69ii.

Aidha SERIKALI INATOA MSAMAHA WA KODI,RIBA NA ADHABU ZINAZOAMBATANA NA MADENI YOTE(Tax Amnesty) YA ADA HIYO YALIYOLIMBIKIZWA KWA MIAKA YA NYUMA" Kilichopo ni kwamba Ada ya Leseni ya Gari wakati wa usajili mara ya kwanza ndiyo itaongezeka kwa kuzingatia CC za gari husika MFANO:

CC: 501 HADI 1500 Ada itakuwa Laki Mbili badala ya Laki Unusu ya sasa
CC 1501 HADI 2500 Ada itafika Laki mbili Unusu tofauti na ya sasa laki 2
CC 2501 NA ZAIDI Itakuwa Laki Tatu
Sasa hapa wengi ndo wataelewa mimi nikiwa mmoja wapo... Kwaiyo ilikifika july 1 ni kutafuta bima tu... Labda na ile ya usalama barabarani
 
  • Thanks
Reactions: tz1
Sasa hapa wengi ndo wataelewa mimi nikiwa mmoja wapo... Kwaiyo ilikifika july 1 ni kutafuta bima tu... Labda na ile ya usalama barabarani
Yaani ni stika hizo tu mkuu kuanzia tarehe Mosi Julai...labda akukamate kwa kosa jingine
 
Kumbe madeni yanalipwa kwanza? Maana mimi roho imeniuma wiki iliyopita nimelipa 1,087,500 kodi ya kuanzia 2015 sasa niliposikia wamefuta nusu nilie kuwa ningejua ningesubiri. Ila kama watadai madeni ya nyuma kabla ya uamuzi huu nitajiona mjanja vinginevyo bado naugulia maumivu!
Mkuu madeni ya nyuma,adhabu na faini zote zimefutwa kwa hiyo sasa hivi hakutakuwa na swali kutoka kwa Mamlaka yoyote iwe Polisi au TRA juu ya Motor Vehicle Licence, ni mwendo wa Stika ya Bima na Inspection tu...Labda waibue stika za fire!
 
Hapo hapo jamaa walishatangaza kuanza kufanya emission Test,hahah watakula vichwa vya watu balaa vya wamiliki wa magari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom