Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Katiba ya Jamhuri ya Tanzania inatamka wazi ya kuwa chanzo cha mamlaka yote hapa nchini ni wananchi. Hivyo panapojitokeza jambo lolote lenye utata chombo chenye madaraka yamwisho katika kumaliza utata huo ni wananchi wenyewe. Katika siku za hivi karibuni kulifanyika njama zenye lengo la kukinyima fursa chama cha CDM kutekeleza majukumu yake bungeni; kufuatia njama hizo CDM ikaamua kuwasikiana moja kwa moja na wananchi. Sasa tunaanza kusikia kelele kutoka kwa viongozi mbali mbali wa CCM wanaotaka vyombo vya dola kutumika ili kudhibiti CDM hisiwe na mawasiliano ya moja kwa moja na wananchi. Jambo hilo likifanyika itakuwa ni matumizi mabaya ya vyombo vya dola, kwakuwa mawasiliano ya moja kwa moja kati ya vyama vya siasa na wananchi ni haki ya kila chama.