the truecaller
JF-Expert Member
- May 8, 2019
- 809
- 940
Nawasalimia wote!
NAMPA POLE SANA "KUB"
Naenda kwenye mada straight.
Matukio haya ya utekaji, upigaji risasi na mengine ya uvunjwaji miguu nchini yamezidi kuendelea.
Kwangu mimi siwezi kukubaliana na hoja za kwamba hii serikali inaweza kujua kama anavyodai tundu lissu na kundi lake.
Hakuna wajinga wa aina hiyo wanaoweza kuwemo Serikalini huku wakijua kitendo hicho ni aidha kibaya kwa kuiweka serikali kwenye picha mbaya zaidi duniani.
Ninachoamini ni kwamba kuna kundi la watu fulani ambao ni wabobezi wa matukio kama haya na wanachofanya ni timing nzuri na wakati muafaka wa kuichafua serikali hii kwa sababu wanazozijua wao.
Kuna watu humu walikwishasema waguswe ili wanuke, ni wabobezi pia wa mambo haya ya taaluma ya kuviziana, lakini pia walikwishasema nchi hii inapoteza muelekeo ki diplomasia.
Lakini pia enzi zao wakiwa kwenye makali ndio utekaji ulipoanza na kungoana meno pia na macho.
Watu hawa maarufu walikwishawahi kuahidi wakati wao ukifika wabaya wao wajiandae pa kutimkia.
Sasa wako kando na wako harakati kimyakimya.
Je, kwanini vyombo vyetu makini visifanye kazi na kuisafisha serikali kutoka kwenye tuhuma hizi za kishetani.
Hata kama wako kwenye mfumo, je kwa nini wasichomolewe tuwajuwe na tumuache JPM aendelee kutimiza safari yetu ya mafanikio?
Nawasilisha.
NAMPA POLE SANA "KUB"
Naenda kwenye mada straight.
Matukio haya ya utekaji, upigaji risasi na mengine ya uvunjwaji miguu nchini yamezidi kuendelea.
Kwangu mimi siwezi kukubaliana na hoja za kwamba hii serikali inaweza kujua kama anavyodai tundu lissu na kundi lake.
Hakuna wajinga wa aina hiyo wanaoweza kuwemo Serikalini huku wakijua kitendo hicho ni aidha kibaya kwa kuiweka serikali kwenye picha mbaya zaidi duniani.
Ninachoamini ni kwamba kuna kundi la watu fulani ambao ni wabobezi wa matukio kama haya na wanachofanya ni timing nzuri na wakati muafaka wa kuichafua serikali hii kwa sababu wanazozijua wao.
Kuna watu humu walikwishasema waguswe ili wanuke, ni wabobezi pia wa mambo haya ya taaluma ya kuviziana, lakini pia walikwishasema nchi hii inapoteza muelekeo ki diplomasia.
Lakini pia enzi zao wakiwa kwenye makali ndio utekaji ulipoanza na kungoana meno pia na macho.
Watu hawa maarufu walikwishawahi kuahidi wakati wao ukifika wabaya wao wajiandae pa kutimkia.
Sasa wako kando na wako harakati kimyakimya.
Je, kwanini vyombo vyetu makini visifanye kazi na kuisafisha serikali kutoka kwenye tuhuma hizi za kishetani.
Hata kama wako kwenye mfumo, je kwa nini wasichomolewe tuwajuwe na tumuache JPM aendelee kutimiza safari yetu ya mafanikio?
Nawasilisha.