Sasa hivi dispensary za kata za Serikali unalipia kila kitu. Hakuna tofauti na hospitali binafsi. Tozo tunazokatwa za kazi gani sasa?

konda msafi

JF-Expert Member
Sep 5, 2018
1,666
8,582
Leo nimempeleka wife kumfanyia vipimo na matibabu nikidhani labda kwa sababu ni dispensary ya serikali huduma itakuwa bure lakini cha kushangaza kila kitu unalipia. Kuanzia kumwona daktari unalipia. Vipimo vyote unalipia, dawa zote unalipia. Kiufupi kila kitu unalipia kwa 100%.

Sasa nimeshindwa kuelewa serikali inaposema tunalipa kodi na tozo ili kuboresha huduma za afya. Huduma gani wanaboresha kama kila kitu tunalipia? Hii nchi sijui imelogwa na nani?
 
Bado kuna hela za IMF!! Wapo busy kuwekeza kwenye miundombinu, huku huduma mbalimbali zikiendelea kudumaa, na za kusua sua kama zamani.
 
Usishangae ndugu yangu hospital huduma za bure ni kwa mabibi mababu, watoto chini ya miaka 5 akivuka hapo kote unalipia tuu na si kwa kificho unapewa rist
Basi haina haja ya kwenda kwenye hosptali za serikali. Bora uende private hospital tu kule kunakojulikana huduma ni ya kulipia.
 
Basi haina haja ya kwenda kwenye hosptali za serikali. Bora uende private hospital tu kule kunakojulikana huduma ni ya kulipia.
Kata Bima hilo ndio suluhisho. Matibabu ni gharama.

Muhimu angalia sehemu ambayo utapona na siyo sehemu inapotolewa huduma ya bure.

Na hii tabia ya watu kulalamika sana imewafanya mpaka madaktari kuanza kuwaandikia wagonjwa dawa walizonazo kituoni na siyo dawa nzuri zaidi ambazo walipaswa waandikiwe wakanunue.

Jamani wekezeni kwenye Afya maana ndio mtaji wa kwanza.
 
Leo nimempeleka wife kumfanyia vipimo na matibabu nikidhani labda kwa sababu ni dispensary ya serikali huduma itakuwa bure lakini cha kushangaza kila kitu unalipia. Kuanzia kumwona daktari unalipia. Vipimo vyote unalipia, dawa zote unalipia. Kiufupi kila kitu unalipia kwa 100%.

Sasa nimeshindwa kuelewa serikali inaposema tunalipa kodi na tozo ili kuboresha huduma za afya. Huduma gani wanaboresha kama kila kitu tunalipia? Hii nchi sijui imelogwa na nani?
Kama huna bima unalipa,tozo haihusu gharama ya matibabu

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Yaani hiyo 2000 unayokatwa unataka utibiwe bure wewe na familia yako yote? Kata Bima Mkuu, and siku hizi kuna packages za bei rahisi na rafiki za Bima
 
Yaani hiyo 2000 unayokatwa unataka utibiwe bure wewe na familia yako yote? Kata Bima Mkuu, and siku hizi kuna packages za bei rahisi na rafiki za Bima
Tatizo wewe kichwani huna akili. Kwa hiyo kazi ya serikali ni nini sasa?
 
Kata Bima hilo ndio suluhisho. Matibabu ni gharama.

Muhimu angalia sehemu ambayo utapona na siyo sehemu inapotolewa huduma ya bure.

Na hii tabia ya watu kulalamika sana imewafanya mpaka madaktari kuanza kuwaandikia wagonjwa dawa walizonazo kituoni na siyo dawa nzuri zaidi ambazo walipaswa waandikiwe wakanunue.

Jamani wekezeni kwenye Afya maana ndio mtaji wa kwanza.
Of course upo sahihi, hatupaswi kucompromise afya zetu lakini unadhani ni sahihi kwa serikali kutokutoa huduma za afya kwa raia wake? Kodi tunalipa, tozo tunalipa, rasilimali kama vile madini na vitu vingine serikali inapata hela. Viongozi wanatembelea V8 za 500,000,000. Unadhani serikali bado haina wajibu wa kutoa huduma za afya bure kwa raia wake?
 
Zerikali za Kiafrika zina laana.
Kodi wanakusanya
Misaada wanapewa
Mikopo rahisi wanapewa
Rasilimali lukuki
** Wananchi wanaishi kama ndege**
 
Leo nimempeleka wife kumfanyia vipimo na matibabu nikidhani labda kwa sababu ni dispensary ya serikali huduma itakuwa bure lakini cha kushangaza kila kitu unalipia. Kuanzia kumwona daktari unalipia. Vipimo vyote unalipia, dawa zote unalipia. Kiufupi kila kitu unalipia kwa 100%.

Sasa nimeshindwa kuelewa serikali inaposema tunalipa kodi na tozo ili kuboresha huduma za afya. Huduma gani wanaboresha kama kila kitu tunalipia? Hii nchi sijui imelogwa na nani?
BIMA, BIMA, BIMA ndio jibu. Sasa hivi iko bima ya kila saizi na ya uwezo wako kwa wananchi wote. Waziri Ummy alipokuwa Afya alimaliza mzizi wa Fitina katika kufanikisha mpango wa BIMA kwa watanzania wote. Ni uamuzi wako tu kama unataka kulipa kila ukiienda zahanati au unalipa bima mara moja kwa mwaka.

Kuna bima za aina nyingi, kwa mfano ya Mwanafunzi, Familia, mtu mmoja pekee ya vikundi n.k. Ya mwanafunzi ni 50 elfu kwa mwaka. Wahi kakate BIMA.
 
Of course upo sahihi, hatupaswi kucompromise afya zetu lakini unadhani ni sahihi kwa serikali kutokutoa huduma za afya kwa raia wake? Kodi tunalipa, tozo tunalipa, rasilimali kama vile madini na vitu vingine serikali inapata hela. Viongozi wanatembelea V8 za 500,000,000. Unadhani serikali bado haina wajibu wa kutoa huduma za afya bure kwa raia wake?
Unachokizungumza ni "movement" ambayo inapaswa kufanywa ili serikali ipange vizuri vipaumbele vyake jambo ambalo siyo la muda mfupi.

Hata wabunge wanapeana Bima za daraja la kwanza kabisa na ndio wawakilishinwa wananchi.
 
Leo nimempeleka wife kumfanyia vipimo na matibabu nikidhani labda kwa sababu ni dispensary ya serikali huduma itakuwa bure lakini cha kushangaza kila kitu unalipia. Kuanzia kumwona daktari unalipia. Vipimo vyote unalipia, dawa zote unalipia. Kiufupi kila kitu unalipia kwa 100%.

Sasa nimeshindwa kuelewa serikali inaposema tunalipa kodi na tozo ili kuboresha huduma za afya. Huduma gani wanaboresha kama kila kitu tunalipia? Hii nchi sijui imelogwa na nani?
Sasa ndugu usilie sana, usipokatwa tozo kila mahali unafikiri wabunge wenu watakula nini? Lazima muwahurumie mliowaweka bungeni.
 
BIMA, BIMA, BIMA ndio jibu. Sasa hivi iko bima ya kila saizi na ya uwezo wako kwa wananchi wote. Waziri Ummy alipokuwa Afya alimaliza mzizi wa Fitina katika kufanikisha mpango wa BIMA kwa watanzania wote. Ni uamuzi wako tu kama unataka kulipa kila ukiienda zahanati au unalipa bima mara moja kwa mwaka.

Kuna bima za aina nyingi, kwa mfano ya Mwanafunzi, Familia, mtu mmoja pekee ya vikundi n.k. Ya mwanafunzi ni 50 elfu kwa mwaka. Wahi kakate BIMA.
Kwa hiyo kazi ya serikali ni nini? Milioni mia tano ya V8 zipo ila za madawa hakuna.
 
Back
Top Bottom