Sasa Bunge limekuwa kama idara ya Ikulu. Haliisimamii tena Serikali!

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
RASMI: BUNGE SASA NI IDARA YA IKULU

Zaidi ya asilimia 70 ya wabunge wote kwenye Bunge letu, wanatoka CCM. Kitendo cha MKATA UMEME kuwadhibiti wabunge hawa ni sawa na kudhibiti Bunge zima ili lisiwe na meno.

Kwa mujibu wa habari iliyoandikwa kwenye gazeti la Mwananchi la leo, MKATA UMEME alikutana nao jana pale Ikulu ya Dom na kuwapiga mkwara mzito akiwataka wafanye kazi ya kulinda maslahi ya chama.

Amewaambia hawapaswi kuchangia kwa kuipinga serikali hata kama inaboronga.

Amewaambia marufuku kushirikiana wabunge wa upinzani.

Amewaambia ni marufuku mbunge wa CCM kumwachia muda wa kuchangia mbunge wa upinzani.

Amewathibithibitishia mbele ya Spika Ndugai kuwa yeye ndiye aliyezuia BUNGE LIVE kwa kuwa anakerwa na jinsi wapinzani walivyokuwa wakipata umaarufu kupitia Bunge live.

Amewapa Onyo wabunge waliokuwa wanapanga kwenda kumtembelea mbunge wa upinzani Godbless Lema gerezani,

Amemshtaki kwa baba yake mbunge mmoja binti ambaye inasemekana huwa anavujisha mambo yao kwa wapinzani.

Amewaonya wabunge waliokuwa wanapanga kuandaa hoja ya kumng'oa waziri mkuu,

Baadaye akawaambia waseme shida zao za majimboni kwao TU, wakazisema, akawaahidi kuzishughulikia (UBAGUZI)

Kimsingi MKATA UMEME anachokifanya ni kulitawala Bunge liwe KIBOGOYO kwa kuwapandikiza roho yake ya CHUKI, UBAGUZI na VISASI wabunge wote wa chama chake huku akitishia kulivunja Bunge ili wote warudi kwenye uchaguzi endapo wataenda kinyume na anachokitaka.

Je, hapo tuna BUNGE au IDARA YA IKULU?
 
kwa wenye akili tunarudi chini na kusema this is a challenge,wapinzani wanakitu cha kufanya 2020 na si kingine kuongeza idadi ya wabunge bungeni,na hicho ndicho tulikua tunakitaka 2015 lakini wapinzani wakang'ang'ania urais zaidi badala ya kuweka nguvu zaidi huku chini....mnawabunge asilimia 30 hata mngeshinda urais mngeyumbishwa tuu na upepo wa asilimia 70 ya wabunge wa Ccm

kwanini upinzani mnadhani kuchukua nchi ni kama kushuka mlima unaanzia juu unashuka chini wakati ni kupanda mlima lazima uanzie chini ndo upande juu...hii ni tanzania siasa za tanzania tusizifananishe na siasa za hayo manchi mengine..
 
Hata wafanya nn hawa ccm,mwisho wao ndo umewadia hivyo. Hata wenyewe hilo wanalifahamu ndo mana mkiti wao yupo busy na mikwara pamoja na vitisho. Kitu ambacho hakitamsaidia 2020.

Kiufupi,hichi chama kinajibomoa chenyewe. Hakuna wazazi watakaofurahia vijana wao wasome then wakose ajira wakati huo huo kuna kilaza analindwa na mtu kufuta. Ccm kwisha habari Yake!!
 
kwa wenye akili tunarudi chini na kusema this is a challenge,wapinzani wanakitu cha kufanya 2020 na si kingine kuongeza idadi ya wabunge bungeni,na hicho ndicho tulikua tunakitaka 2015 lakini wapinzani wakang'ang'ania urais zaidi badala ya kuweka nguvu zaidi huku chini....mnawabunge asilimia 30 hata mngeshinda urais mngeyumbishwa tuu na upepo wa asilimia 70 ya wabunge wa Ccm..kwanini upinzani mnadhani kuchukua nchi ni kama kushuka mlima unaanzia juu unashuka chini wakati ni kupanda mlima lazima uanzie chini ndo upande juu...hii ni tanzania siasa za tanzania tusizifananishe na siasa za hayo manchi mengine..
wataiba kura kama kawaida
 
RASMI: BUNGE SASA NI IDARA YA IKULU

Zaidi ya asilimia 70 ya wabunge wote kwenye Bunge letu, wanatoka CCM. Kitendo cha MKATA UMEME kuwadhibiti wabunge hawa ni sawa na kudhibiti Bunge zima ili lisiwe na meno.

Kwa mujibu wa habari iliyoandikwa kwenye gazeti la Mwananchi la leo, MKATA UMEME alikutana nao jana pale Ikulu ya Dom na kuwapiga mkwara mzito akiwataka wafanye kazi ya kulinda maslahi ya chama.

Amewaambia hawapaswi kuchangia kwa kuipinga serikali hata kama inaboronga.

Amewaambia marufuku kushirikiana wabunge wa upinzani.

Amewaambia ni marufuku mbunge wa CCM kumwachia muda wa kuchangia mbunge wa upinzani.

Amewathibithibitishia mbele ya Spika Ndugai kuwa yeye ndiye aliyezuia BUNGE LIVE kwa kuwa anakerwa na jinsi wapinzani walivyokuwa wakipata umaarufu kupitia Bunge live.

Amewapa Onyo wabunge waliokuwa wanapanga kwenda kumtembelea mbunge wa upinzani Godbless Lema gerezani,

Amemshtaki kwa baba yake mbunge mmoja binti ambaye inasemekana huwa anavujisha mambo yao kwa wapinzani.

Amewaonya wabunge waliokuwa wanapanga kuandaa hoja ya kumng'oa waziri mkuu,

Baadaye akawaambia waseme shida zao za majimboni kwao TU, wakazisema, akawaahidi kuzishughulikia (UBAGUZI)

Kimsingi MKATA UMEME anachokifanya ni kulitawala Bunge liwe KIBOGOYO kwa kuwapandikiza roho yake ya CHUKI, UBAGUZI na VISASI wabunge wote wa chama chake huku akitishia kulivunja Bunge ili wote warudi kwenye uchaguzi endapo wataenda kinyume na anachokitaka.

Je, hapo tuna BUNGE au IDARA YA IKULU?
halafu utakuta viongozi wa dini wapo kimya tu...
 
Watanzani tuko katika kipindi kigumu kuli vyote.Dawa ni kuingia mtaani kujitoa mhanga kuupinga utawala wake.Huyu jamaa nia yake kubwa ni kuua upinzani ili iwe rahisi kuidhinisha udikteta wake.
upinzani mmejiua wenyewe hembu niambie hivi sasa mkiruhusiwa kufanya mikutano mnahoja gani ya kujenga taifa mtakayokuja nayo jamii ikawaelewa zaidi wanavyomuelewa magufuli,mmekosa hoja ya kuisimamia tangia magufuli aanze utekelezaji wake mnabaki kudandia matukio mara leo ajira mara kesho dawa za kulevya mara kesho bashite nini mnafanya???halafu unampango wakuingia mtaani uingie mtaani na nani ??kwa ushawishi upi huo utakao utumia kuwaleta watu barabarani??
 
Back
Top Bottom