Masalu Jacob
JF-Expert Member
- Jul 26, 2017
- 947
- 1,088
Habari Tanzania!
Kura & Uhusika: Hii ni kwako wewe ndugu mtanzania na kwa wale wote wanaohusika na upigaji kura. Nakuomba kwa kukuwekea msisitizo ewe mpiga kura na Mtanzania tafadhali sana, hakikisha unakwenda kukipigia chama chenye mgombea mzuri, makini na ambaye mwenye sera safi inayogusa na kuakisi maisha na mahitaji yako; jiepushe na ushabiki; kumbuka hayo ni maisha yako na taifa lako ulipendalo.
Sasa: Wananchi tumebahatika kwa usawa na pamoja kusikiliza sera na ahadi juu ya nini vyama vitatutendea tukivipa nafasi kupitia kura. Kazi ni kwako. Jiangalie wewe, jirani, ndugu na jamaa yako kuhusu mahitaji na maisha yenu ya kidunia.
Mwisho: Nawatakia watanzania wote amani, upendo na usawa sahihi katika upigaji kura nchi nzima. Mungu awatangulie kila mmoja kwa namna itakavyompendeza Mungu katika mapenzi yake.
"Tanzania ni nchi nzuri sana; Tanzania inapendeza sana kwa mambo yote; Tanzania ni tulizo la moyo wako".
Bye.
Kura & Uhusika: Hii ni kwako wewe ndugu mtanzania na kwa wale wote wanaohusika na upigaji kura. Nakuomba kwa kukuwekea msisitizo ewe mpiga kura na Mtanzania tafadhali sana, hakikisha unakwenda kukipigia chama chenye mgombea mzuri, makini na ambaye mwenye sera safi inayogusa na kuakisi maisha na mahitaji yako; jiepushe na ushabiki; kumbuka hayo ni maisha yako na taifa lako ulipendalo.
Sasa: Wananchi tumebahatika kwa usawa na pamoja kusikiliza sera na ahadi juu ya nini vyama vitatutendea tukivipa nafasi kupitia kura. Kazi ni kwako. Jiangalie wewe, jirani, ndugu na jamaa yako kuhusu mahitaji na maisha yenu ya kidunia.
Mwisho: Nawatakia watanzania wote amani, upendo na usawa sahihi katika upigaji kura nchi nzima. Mungu awatangulie kila mmoja kwa namna itakavyompendeza Mungu katika mapenzi yake.
"Tanzania ni nchi nzuri sana; Tanzania inapendeza sana kwa mambo yote; Tanzania ni tulizo la moyo wako".
Bye.