Kangi Lugola: Hakuna mtu muongo kama CAG Assad! Akithibitisha madai yake nitajiuzulu

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Waziri wa Mambo ya Ndani, Lugola amesema hakuna mtu muongo kama CAG na kwamba yupo tayari kuweka uwaziri wake rehani, ikiwa itabainika kuwa taarifa zake za ukaguzi kuhusu sare hewa za jeshi la polisi zilizogharimu Sh16bilioni ni ya kweli.

Kutokana na ukaguzi alioufanya, Profesa Assad alisema ukaguzi ulibaini mahitaji ya kitaalamu kutoka idara inayotumia mfumo wa Utambuzi wa Alama za Vidole (AFIS), ulibaini kuwa mahitaji ya kitaalamu kutoka idara inayotumia mfumo huo hayakuzingatiwa wakati wa kuthamini na kutoa zabuni.





























“Malipo ya Sh3.30 bilioni yalifanyika kwa mzabuni kwa ajili ya huduma ya matengenezo na msaada wa kitaalamu wa mfumo wa utambuzi wa alama za vidole,” amesema.

Alisema huduma hiyo ilipangwa kufanyika kwenye mikoa nane ya kipolisi ya Temeke, Mwanza, Simiyu, Tabora, Kigoma, Geita na Kinondoni lakini Polisi ilishindwa kuthibitisha kuwa matengenezo hayo na msaada wa kitaalamu ulifanyika.

Profesa Assad alisema vifaa vya utambuzi wa alama za vidole vyenye thamani ya Sh1.73 bilioni havikufungwa kwenye magereza 35 kama ilivyoainishwa badala yake, vilihifadhiwa katika ofisi ya upelelezi Makuu ya Polisi.

“Malipo ya Sh604.39 milioni kwa ajili ya mafunzo kwa wataalamu 30 hayakufanyika,” amesema.

Alisema jeshi la Polisi lilishindwa kuionyesha timu yake ya ukaguzi zilipo monita 58 za kompyuta aina ya Dell zenye thamani ya Sh159.16 milioni zilizopelekwa kwenye kitengo cha cha uchunguzi wa kisayansi cha Makao Makuu ya Polisi (Forensic).

Pia, alisema monita 213 za kompyuta aina Dell zilizolipiwa Sh195.22 milioni kwa mzabuni Lugumi Enterprises Limited lakini mzabuni hakuzikabidhi.

Pia, alisema ukaguzi wa ununuzi wa sare za askari umebaini jeshi hilo lilipa Sh16.66 bilioni zililipwa bila kuwapo na ushahidi wa uagizaji na upokeaji wa sare hizo za polisi wa Boharia Mkuu wa Polisi.

“Pia nilibaini maoni ya kisheria ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yanayohusu uwasilishaji wa kiapo cha nguvu ya kisheria (Power of Attorney) na leseni halali ya biashara hayakuzingatiwa na Katibu Mkuu wa Wizara wa Mambo ya Ndani wakati wa kusaini mkataba namba ME 014/PF/2015/2016/G/30 Lot 2 uliohusu ununuzi wa sare za polisi,” alisema.

Profesa Assad alisema anapendekeza Jeshi la Polisi lihakikishe vifaa vya utambuzi wa alama za vidole vinafungwa maeneo husika na kuanza kutumika ilivyokusudiwa.

MY TAKE:

Tunaomba msimdhuru CAG wetu Assad wala kumsumbua. Tunataka mbishane kwa hoja sio Vitisho. Msanii wa Bongo Fleva Roma Mkatoriki aliimba "WEKA SILAHA CHINI TUBISHANE KWA HOJA".

Kwa hili Swala naomba Lugola na Polisi wako muwe wapole kama mnanyolewa.

Kumbuka: Mwigulu Nchemba alijaribu kimshambulia Assad akaondoka kwenye uwaziri akamuacha Assad anadunda. Assad ni kitukuu cha mtume.

=====

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema hajawahi kumuona mtu muongo katika nchi hii kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad.

Amesema anauweka rehani uwaziri wake ikiwa itathibitika kuwa taarifa za ukaguzi wa CAG kuhusu sare hewa za Jeshi la Polisi zinazofikia Sh. bilioni 16 ni ya kweli.

“Sijawahi kuona mtu muongo kama CAG, Jeshi la Polisi hakuna sare hewa. Ninaomba maofisa wa ofisi ya CAG twende nao stoo wakaone sare mpya za jeshi la polisi. Kama nasema uongo nitajivua nguo na ninaweka uwaziri wangu rehani” Kangi Lugola - Waziri Mambo ya Ndani

Waziri Lugola aliuweka rehani uwaziri wake huo, wakati akijibu hoja za Wabunge alipokuwa akihitimisha mjadala wa hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2019/2020 ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Amesema sare hizo ziko katika makontena


 
CAG awatizame kwa makini wale watu anaowatuma kufanya ukaguzi, ni vichwa ngumu kwelikweli, wakiamua kukomalia jambo hata uwape vielelezo vyote bado watang'ang'ana tu. Mwisho wa siku watu wanaamua kutokubishana nao, wanawaacha waandike utumbo wao kisha wakati ukifika audit queries zote zinakua cleared na kamati.
 
Back
Top Bottom