Saratani Kanda ya Ziwa - Kipimo cha Upeo wa Akili Zetu

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,467
40,973
Sisi Waafrika, na zaidi Watanzania, huenda ubinadamu wetu haujakamilika. Mataifa ya watu wenye akili za hali ya juu, wanajua kuwa uhai na usalama wa mtu ndiyo kipaumbele cha kwanza cha Serikali na jamii.

Sisi, unaweza kushuhudia pesa ya sherehe za mwenge zikawepo, pesa ya sherehe za CCM ikawepo, pesa ya posho ya viongozi wanaozurura bila sababu za msingi ikawepo, pesa ya kulipana posho wabunge wasiojadili lolote la maana ikawepo, pesa ya msururu wa misafara ya magari ya viongozi wakuu ikawepo, pesa ya kununulia magari ya kifahari kwa viongozi wa serikali ikawepo, lakini pesa ya kufanyia utafiti wa kujua chanzo cha tatizo la saratani kuwa kubwa sana sehemu mojawapo ya nchi yetu, ikawa haipo.

Tena hao wanaoteseka na kufa kwa saratani, ndiyo chamzo kikuu cha hiyo pesa yote wanayotumia hao wapanga matumizi ya pesa ya Serikali.

Tatizo la saratani kuwa kubwa sana Kanda ya Ziwa, inafahamika tangu muda mrefu. Serikali inaliongelea kama habari ya mpira wa simba na yanga, badala ya kuliona ni jambo linalotakiwa kuwekwa kwenye agenda za kipaumbele cha kwanza kwa sababu ni suala linalohusu uhai wa binadamu.

Yaani aheri watu waendelee kufa lakini porojo na tafrija za kutafuna pesa kupitia mambo mbalimbali yasiyo ya lazima, zisikosekane.

Yaani inashangaza kusikia kuwa Marekani wanafanya utafiti juu ya chanzo cha tatizo hili, lakini Serikali yetu ipo tu, na inaona ni kawaida!!

Wananchi tunataka kujua, tangu tatizo hili lifahamike, Serikali imefabya nini? Na matokeo take yamekuwa yapi. Wananchi tuamke, tukiendelea kulala usingizi kwa kufikiria wapo wanaopigania uhai wetu, tunajidanfanya.

Kama Serikali, tangu tatizo hili lifamike, haijafanya chochote, wananchi tuwatake waliotakiwa kuchukua hatua halafu hawakuchukua, wajiuzuru mara moja. Tunataka Serikali na watendaji wanaowajibika kikamilifu kwa maisha ya wananchi, na hasa uhai na usalama wao.
 
Sometimes tukiongea Sana wanasema Sisi sio wazalendo yaani unakubali kufa ili uitwe mzalendo..
Sisi wabongo ndiyo tabaka la mwisho Africa Kwa UJINGA, kuna MAFALA walilaumu Kwa kauli ile ya Dr MPANGO kuwa analeta taharuki.

Nchi hii tumelogwa wote Akili na MWENGE WA UHURU ni Hadi pale siku tutaacha kukimbiza huu UCHAWI (MWENGE)
 
Inashangaza sana, utakuta mtu anagombea uenyekiti wa CCM kata hivyo anakuona unaehoji utendaji wa serikali Kama siyo mzalendo Bali ni yeye tu.
Chama Kama CCM kinatusumbua sana waTanzania siyo kwa kutokuteua viongozi wenye uzalendo Bali kusababisha afya ya akili ya waTanzania walio wengi kudhani kuwa kupata cheo ndani ya Chama Chao ndicho kuipenda nchi.

Siku waTanzania watakapomchua adui yao watasikitika sana.
 
Sisi Waafrika, na zaidi Watanzania, huenda ubinadamu wetu haujakamilika. Mataifa ya watu wenye akili za hali ya juu, wanajua kuwa uhai na usalama wa mtu ndiyo kipaumbele cha kwanza cha Serikali na jamii.

Sisi, unaweza kushuhudia pesa ya sherehe za mwenge zikawepo, pesa ya sherehe za CCM ikawepo, pesa ya posho ya viongozi wanaozurura bila sababu za msingi ikawepo, pesa ya kulipana posho wabunge wasiojadili lolote la maana ikawepo, pesa ya msururu wa misafara ya magari ya viongozi wakuu ikawepo, pesa ya kununulia magari ya kifahari kwa viongozi wa serikali ikawepo, lakini pesa ya kufanyia utafiti wa kujua chanzo cha tatizo la saratani kuwa kubwa sana sehemu mojawapo ya nchi yetu, ikawa haipo.

Tena hao wanaoteseka na kufa kwa saratani, ndiyo chamzo kikuu cha hiyo pesa yote wanayotumia hao wapanga matumizi ya pesa ya Serikali.

Tatizo la saratani kuwa kubwa sana Kanda ya Ziwa, inafahamika tangu muda mrefu. Serikali inaliongelea kama habari ya mpira wa simba na yanga, badala ya kuliona ni jambo linalotakiwa kuwekwa kwenye agenda za kipaumbele cha kwanza kwa sababu ni suala linalohusu uhai wa binadamu.

Yaani aheri watu waendelee kufa lakini porojo na tafrija za kutafuna pesa kupitia mambo mbalimbali yasiyo ya lazima, zisikosekane.

Yaani inashangaza kusikia kuwa Marekani wanafanya utafiti juu ya chanzo cha tatizo hili, lakini Serikali yetu ipo tu, na inaona ni kawaida!!

Wananchi tunataka kujua, tangu tatizo hili lifahamike, Serikali imefabya nini? Na matokeo take yamekuwa yapi. Wananchi tuamke, tukiendelea kulala usingizi kwa kufikiria wapo wanaopigania uhai wetu, tunajidanfanya.

Kama Serikali, tangu tatizo hili lifamike, haijafanya chochote, wananchi tuwatake waliotakiwa kuchukua hatua halafu hawakuchukua, wajiuzuru mara moja. Tunataka Serikali na watendaji wanaowajibika kikamilifu kwa maisha ya wananchi, na hasa uhai na usalama wao.
Mkuu emegusia mambo yenye msingi sana juu ya tatizo lililopo. Serikali inashughulia mambo magumu kama kwa "fire brigade measures" ili ionekane kuwa imeguswa na kuchukua hatua juu ya jambo hilo.

Tatizo la ugonjwa huu katika maeneo tajwa ni la muda mrefu, na tena ni lenye kuathiri maisha ya watu, wengi kiafya na gharama za fedha, lakini ni dhahiri inaonyesha linashughulikiwa kwa kauli tupu za kisiasa zizokuwa na nia ya dhati ndani yake.

Ni vyema zikatafuta njia stahiki za kisayansi ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu. Timu ya wataalamu wa afya ni vyema ikatafuta majibu sahihi kupitia tafiti watakazozifanya na kutoa mapendekezo yao ya kitaalamu.
 
Sisi Waafrika, na zaidi Watanzania, huenda ubinadamu wetu haujakamilika. Mataifa ya watu wenye akili za hali ya juu, wanajua kuwa uhai na usalama wa mtu ndiyo kipaumbele cha kwanza cha Serikali na jamii.

Sisi, unaweza kushuhudia pesa ya sherehe za mwenge zikawepo, pesa ya sherehe za CCM ikawepo, pesa ya posho ya viongozi wanaozurura bila sababu za msingi ikawepo, pesa ya kulipana posho wabunge wasiojadili lolote la maana ikawepo, pesa ya msururu wa misafara ya magari ya viongozi wakuu ikawepo, pesa ya kununulia magari ya kifahari kwa viongozi wa serikali ikawepo, lakini pesa ya kufanyia utafiti wa kujua chanzo cha tatizo la saratani kuwa kubwa sana sehemu mojawapo ya nchi yetu, ikawa haipo.

Tena hao wanaoteseka na kufa kwa saratani, ndiyo chamzo kikuu cha hiyo pesa yote wanayotumia hao wapanga matumizi ya pesa ya Serikali.

Tatizo la saratani kuwa kubwa sana Kanda ya Ziwa, inafahamika tangu muda mrefu. Serikali inaliongelea kama habari ya mpira wa simba na yanga, badala ya kuliona ni jambo linalotakiwa kuwekwa kwenye agenda za kipaumbele cha kwanza kwa sababu ni suala linalohusu uhai wa binadamu.

Yaani aheri watu waendelee kufa lakini porojo na tafrija za kutafuna pesa kupitia mambo mbalimbali yasiyo ya lazima, zisikosekane.

Yaani inashangaza kusikia kuwa Marekani wanafanya utafiti juu ya chanzo cha tatizo hili, lakini Serikali yetu ipo tu, na inaona ni kawaida!!

Wananchi tunataka kujua, tangu tatizo hili lifahamike, Serikali imefabya nini? Na matokeo take yamekuwa yapi. Wananchi tuamke, tukiendelea kulala usingizi kwa kufikiria wapo wanaopigania uhai wetu, tunajidanfanya.

Kama Serikali, tangu tatizo hili lifamike, haijafanya chochote, wananchi tuwatake waliotakiwa kuchukua hatua halafu hawakuchukua, wajiuzuru mara moja. Tunataka Serikali na watendaji wanaowajibika kikamilifu kwa maisha ya wananchi, na hasa uhai na usalama wao.
CCM haijali mambo ya Msingi na hapa ndio tatizo kubwa lilipo kalia maendeleo siku zote ni Afya za watu,serikali nyingi zilizokaa kiwiziwizi huwa haziwezi kuona kwa namna gani watu wanateseka na jambo fulani.Naamini viongozi wanapitia maandiko ya Msingi kama haya lkn changamoto ni kusikia na kuelewa na kufanyia kazi tatizo kama hili la saratani.
 
Mada za maana kama hizi huwa hazina wachangiaji.
Ila ungezungumzia masuala ya kula tunda, uchawi nk thread ingekuwa inakurasa100+
Na sisi hatuna tofauti na walioko Serikalini ambao hela ya kufanyia mambo yasiyo ya lazima ipo, lakini ya kufanyia tafiti za kuokoa maisha ya watu haipo. Muda wa kuchangia vioja tunao lakini wa kuchangia jambo linalohusu uhai wetu, hatuna.
 
CCM haijali mambo ya Msingi na hapa ndio tatizo kubwa lilipo kalia maendeleo siku zote ni Afya za watu,serikali nyingi zilizokaa kiwiziwizi huwa haziwezi kuona kwa namna gani watu wanateseka na jambo fulani.Naamini viongozi wanapitia maandiko ya Msingi kama haya lkn changamoto ni kusikia na kuelewa na kufanyia kazi tatizo kama hili la saratani.
Ccm ni ya hovyo Sana!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kuzaliwa Africa na hasa Tanzania kwa kweli ni kama adhabu. Sisi Watanzania inabidi Mungu atusamehe wote tusiingie motoni isipokuwa viongozi wetu waliojipa dhamana ya kutuongoza.

Hili la Kansa kanda ya ziwa na jinsi Serikali inavyolichukulia poa kwa kweli inasikitisha sana
 
Sisi Waafrika, na zaidi Watanzania, huenda ubinadamu wetu haujakamilika. Mataifa ya watu wenye akili za hali ya juu, wanajua kuwa uhai na usalama wa mtu ndiyo kipaumbele cha kwanza cha Serikali na jamii.

Sisi, unaweza kushuhudia pesa ya sherehe za mwenge zikawepo, pesa ya sherehe za CCM ikawepo, pesa ya posho ya viongozi wanaozurura bila sababu za msingi ikawepo, pesa ya kulipana posho wabunge wasiojadili lolote la maana ikawepo, pesa ya msururu wa misafara ya magari ya viongozi wakuu ikawepo, pesa ya kununulia magari ya kifahari kwa viongozi wa serikali ikawepo, lakini pesa ya kufanyia utafiti wa kujua chanzo cha tatizo la saratani kuwa kubwa sana sehemu mojawapo ya nchi yetu, ikawa haipo.

Tena hao wanaoteseka na kufa kwa saratani, ndiyo chamzo kikuu cha hiyo pesa yote wanayotumia hao wapanga matumizi ya pesa ya Serikali.

Tatizo la saratani kuwa kubwa sana Kanda ya Ziwa, inafahamika tangu muda mrefu. Serikali inaliongelea kama habari ya mpira wa simba na yanga, badala ya kuliona ni jambo linalotakiwa kuwekwa kwenye agenda za kipaumbele cha kwanza kwa sababu ni suala linalohusu uhai wa binadamu.

Yaani aheri watu waendelee kufa lakini porojo na tafrija za kutafuna pesa kupitia mambo mbalimbali yasiyo ya lazima, zisikosekane.

Yaani inashangaza kusikia kuwa Marekani wanafanya utafiti juu ya chanzo cha tatizo hili, lakini Serikali yetu ipo tu, na inaona ni kawaida!!

Wananchi tunataka kujua, tangu tatizo hili lifahamike, Serikali imefabya nini? Na matokeo take yamekuwa yapi. Wananchi tuamke, tukiendelea kulala usingizi kwa kufikiria wapo wanaopigania uhai wetu, tunajidanfanya.

Kama Serikali, tangu tatizo hili lifamike, haijafanya chochote, wananchi tuwatake waliotakiwa kuchukua hatua halafu hawakuchukua, wajiuzuru mara moja. Tunataka Serikali na watendaji wanaowajibika kikamilifu kwa maisha ya wananchi, na hasa uhai na usalama wao.
Umeandika jambo la msingi sana. Hii ilihitaji "kumwaga" hela ya utafiti. kama hatuna uwezo washirikishe CDC or any high ranking academin institution from Western Europe/ USA to do high level research on this catastophe I can call!
 
Yaani hiyo hatari inayoendelea huko kanda ya ziwa ni jambo la kutisha sana. Kwa sasa mimi na familia yangu tumeacha kabisa kutumia samaki wa ziwa Victoria baada ya kujua habari hii ya hatari. Siku serekali itachukua hatua itakuwa madhara ya wazi yameshaenea.
 
Umeandika jambo la msingi sana. Hii ilihitaji "kumwaga" hela ya utafiti. kama hatuna uwezo washirikishe CDC or any high ranking academin institution from Western Europe/ USA to do high level research on this catastophe I can call!
Upo sahihi sana. Kama Serikali haiwezi kujali uhai wa watu wake, ni nini tena itakachojali?

Life, security and safety of your people should come top of your priorities.

Kutothamini uhai wa wananchi, ndio unaofanya hata baadhi ya Polisi kuondoa uhai wa watuhumiwa kiurahisi, na hawaoni kama ni jambo baya.
 
Yaani hiyo hatari inayoendelea huko kanda ya ziwa ni jambo la kutisha sana. Kwa sasa mimi na familia yangu tumeacha kabisa kutumia samaki wa ziwa Victoria baada ya kujua habari hii ya hatari. Siku serekali itachukua hatua itakuwa madhara ya wazi yameshaenea.
Ukweli ni kwamba, yawezekana samaki wakawa sababu mojawapo au isiwe sababu kuu.

Cases za saratani kuwa juu kwa jamii zinazoishi kulizunguka ziwa Victoria, ilionekana pia huko Kenya na Uganda. Je, na huko wanatumia formalin kutunzia samaki wasiuze? It must be something related to the lake but what is it? Ni samaki, ni maji au kitu gani?

Jambo hili lilikuwa rahisi kufanyia utafiti, na ungeweza kufanyika utafiti kuhusisha nchi zote 3 zinazopakana na Lake Victoria. Hata gharama zingekuwa shared, na kungeweza kuundwa taasisi ya kushughulikia utafiti wa Ziwa Victoria ambayo daima ingeangalia usalama wa maji na bonde zima.

Ikumbukwe kuwa maji ya Victoria sasa hivi yanatumika katika mikoa ya:

Mwanza
Geita
Kagera
Mara
Shinyanga
Tabora

Na lengo ni kuyafikisha mpaka Singida hadi Dodoma. Kama tatizo ni maji, hata ukiacha kula samaki bado utakunywa maji ya Ziwa Victoria (sasa hivi kuna makampuni yanayouza maji ya kunywa, wanatumia hayo maji, na pia yanatumika kupikia, na shughuli mbalimbali)
 
Ukweli ni kwamba, yawezekana samaki wakawa sababu mojawapo au isiwe sababu kuu.

Cases za saratani kuwa juu kwa jamii zinazoishi kulizunguka ziwa Victoria, ilionekana pia huko Kenya na Uganda. Je, na huko wanatumia formalin kutunzia samaki wasiuze? It must be something related to the lake but what is it? Ni samaki, ni maji au kitu gani?

Jambo hili lilikuwa rahisi kufanyia utafiti, na ungeweza kufanyika utafiti kuhusisha nchi zote 3 zinazopakana na Lake Victoria. Hata gharama zingekuwa shared, na kungeweza kuundwa taasisi ya kushughulikia utafiti wa Ziwa Victoria ambayo daima ingeangalia usalama wa maji na bonde zima.

Ikumbukwe kuwa maji ya Victoria sasa hivi yanatumika katika mikoa ya:

Mwanza
Geita
Kagera
Mara
Shinyanga
Tabora

Na lengo ni kuyafikisha mpaka Singida hadi Dodoma. Kama tatizo ni maji, hata ukiacha kula samaki bado utakunywa maji ya Ziwa Victoria (sasa hivi kuna makampuni yanayouza maji ya kunywa, wanatumia hayo maji, na pia yanatumika kupikia, na shughuli mbalimbali)

Hapo kweli inahitajika uchunguzi/utafiti wa maana,kuna mtu mwingine alisema pia hizi dawa zinazotumika kwenye mazao/mashamba ni hatari.
 
Sometimes tukiongea Sana wanasema Sisi sio wazalendo yaani unakubali kufa ili uitwe mzalendo..
Sisi wabongo ndiyo tabaka la mwisho Africa Kwa UJINGA, kuna MAFALA walilaumu Kwa kauli ile ya Dr MPANGO kuwa analeta taharuki.

Nchi hii tumelogwa wote Akili na MWENGE WA UHURU ni Hadi pale siku tutaacha kukimbiza huu UCHAWI (MWENGE)
Makamu wa Rais, Dr. Mpango, alitakiwa kwenda mbali zaidi. Alitakiwa aeleze pia Serikali imefanya nini? Aliyoyasema yalitokana na utafiti au hearsay. Hata kama ni hearsay, baada ya kupata taarifa hiyo, Serikali imechukua hatua gani?

Hizo dawa zinatokaje huko hospitalini? Mabwana afya, Taasusi ya kudhibiti ubora wa vyakula na maafisa samaki wanafanya kazi gani, kama kweli samaki wanatunzwa kwa kutumia formalin?
 
, lakini pesa ya kufanyia utafiti wa kujua chanzo cha tatizo la saratani kuwa kubwa sana sehemu mojawapo ya nchi yetu, ikawa haipo.

Tena hao wanaoteseka na kufa kwa saratani, ndiyo chamzo kikuu cha hiyo pesa yote wanayotumia hao wapanga matumizi ya pesa ya Serikali.

Tatizo la saratani kuwa kubwa sana Kanda ya Ziwa, inafahamika tangu muda mrefu. Serikali inaliongelea kama habari ya mpira wa simba na yanga, badala ya kuliona ni jambo linalotakiwa kuwekwa kwenye agenda za kipaumbele cha kwanza kwa sababu ni suala linalohusu uhai wa binadamu.

Yaani aheri watu waendelee kufa lakini porojo na tafrija za kutafuna pesa kupitia mambo mbalimbali yasiyo ya lazima, zisikosekane.
Mkuu Bams Nimeguswa!. Tanzania bado tuna tatizo la upangaji vipaumbele vyetu, baada ya Elimu, Afya na kilimo, ilipaswa ije nishati!. Ni aibu na hatari kupikia kuni na mkaa!.

Ila hata sisi media tunastahili lawama on this, tulipaswa tuwe na kada ya waandishi wabebezi wa masuala ya afya na kuibuka na strong IJ story ya data journalism on cancer ili kuifungua macho serikali yetu!.

Media tulipaswa kufanya survey ya idadi ya wagonjwa wa cancer Kanda ya Ziwa ni wangapi compared to Kanda nyingine, na pia cancer hiyo ni cancer ya nini na waathirika wakubwa ni kina nani?. Kuangalia proximity ya migodi mikubwa na idadi ya wagonjwa kama ile issue ya Mto Tigite.

Matokeo yakionyesha idadi kubwa ya waathirika ni vijiji jirani na migodi mikubwa, ndipo serikali yetu itafungua macho na kuchukua hatua!.
P
 
Back
Top Bottom