Jana nimesoma kwa makini sana makala ya Samson Mwigamba kwenye Tanzania Daima na nikashangaa sana. Nimemtumia ujumbe kumuuliza alikuwa na maana gani lakini mpaka sasa hajanijibu. Hili ndilo nililoligundua katika makala aliyoipa kichwa "Arumeru Mashariki ilikuwa kama operation ya Kijeshi"
Ameelezea mambo mengi na kuwashukuru watu wengi sana waliofanya kazi ya ukombozi Arumeru, Ameanzia kwa Mh Mbowe, Mameneja wa Kampeni Mchungaji Natse na V Nyerere, Mkuu wa operation John Mrema, Katibu wa CDM wa mkoa, Viongozi wa Bavicha na wengine wengi. Lakini jambo la ajabu ni kuwa hakuna hata mahali ambapo alimtaja Dr Slaa. Sasa mimi nimejiuliza inawezekanaje Mwigamba asimuone Dr Slaa kwenye kampeni? Vyombo vya habari vilituambia kuwa Dr Slaa alipokewa kifalme Arumeru, tulimuona na kumsikia kwenye majukwaa akimnadi Joshua, ni yeye aliyekashifiwa kuiba pesa za ujio wa Papa, ni yeye alitukanwa matusi mazito na Ndugu Lusinde. Sasa inawezekanaje Mwigamba asimtaje katika shukrani zake? Huu ndio ukamamnda gani, hata kama kuna sintofahamu baina yao kwa nini analionyesha hadharani hivyo? Nilitamani niwawekee vipande vya shukrani zake lakini Tanzania Daima online haikuiweka hiyo makala, sijui ni bahati mbaya ama wameistukia kama mimi nilivyofanya?
Makamanda tuache unafiki, hata kama mtu ameondolewa kuwa mhasibu wa chama sio sababu ya kuweka kinyongo, tujue tu kuwa cheo ni dhamana na si haki ya mtu. Ukombozi utaletwa na watu makini wenye nia ya dhati na wasio na agenda ya siri nyuma yao. Hoja zote ni lazima ziwekwe mezani, zijadiliwe kisha tusonge mbele kwenye mapambano.
Samson angalia sana usije ukajiweka upande mbaya wa historia ya taifa letu. Katika ujumbe wangu wa jana nilitoa wito kwako uombe radhi wasomaji wako na wana CDM popote pale walipo kwa kosa hilo. Inawezekana ulipitiwa tu na hukudhamiria, kama hivyo ndivyo basi nami utanisamehe.
SAA YA UKOMBOZI IMEFIKA
Ameelezea mambo mengi na kuwashukuru watu wengi sana waliofanya kazi ya ukombozi Arumeru, Ameanzia kwa Mh Mbowe, Mameneja wa Kampeni Mchungaji Natse na V Nyerere, Mkuu wa operation John Mrema, Katibu wa CDM wa mkoa, Viongozi wa Bavicha na wengine wengi. Lakini jambo la ajabu ni kuwa hakuna hata mahali ambapo alimtaja Dr Slaa. Sasa mimi nimejiuliza inawezekanaje Mwigamba asimuone Dr Slaa kwenye kampeni? Vyombo vya habari vilituambia kuwa Dr Slaa alipokewa kifalme Arumeru, tulimuona na kumsikia kwenye majukwaa akimnadi Joshua, ni yeye aliyekashifiwa kuiba pesa za ujio wa Papa, ni yeye alitukanwa matusi mazito na Ndugu Lusinde. Sasa inawezekanaje Mwigamba asimtaje katika shukrani zake? Huu ndio ukamamnda gani, hata kama kuna sintofahamu baina yao kwa nini analionyesha hadharani hivyo? Nilitamani niwawekee vipande vya shukrani zake lakini Tanzania Daima online haikuiweka hiyo makala, sijui ni bahati mbaya ama wameistukia kama mimi nilivyofanya?
Makamanda tuache unafiki, hata kama mtu ameondolewa kuwa mhasibu wa chama sio sababu ya kuweka kinyongo, tujue tu kuwa cheo ni dhamana na si haki ya mtu. Ukombozi utaletwa na watu makini wenye nia ya dhati na wasio na agenda ya siri nyuma yao. Hoja zote ni lazima ziwekwe mezani, zijadiliwe kisha tusonge mbele kwenye mapambano.
Samson angalia sana usije ukajiweka upande mbaya wa historia ya taifa letu. Katika ujumbe wangu wa jana nilitoa wito kwako uombe radhi wasomaji wako na wana CDM popote pale walipo kwa kosa hilo. Inawezekana ulipitiwa tu na hukudhamiria, kama hivyo ndivyo basi nami utanisamehe.
SAA YA UKOMBOZI IMEFIKA