Samson Kipepe afariki dunia

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Wadau,

Hii iacheni kwa muda kabla ya kuipeleka kwenye matangazo.

Kwa masikitiko makubwa nawajulisheni kifo cha Samson Kipepe ambaye alikuwa anafanya kazi umoja wa vijana wa CCM. Kifo kimetokea asubuhi hii pale hospitali ya Lugalo.

Aliwahi kugombea kuwa mwenyekiti wa vijana nafikiri wakati ule Nchimbi anagombea kwa mara ya kwanza. Mwaka 2005 aligombea ubunge wa Kyela pamoja na akina Dr. Mwakyembe na Mwakipesile.

Nilimpokea Kipepe Rungwe miaka ya 80 baada ya kuombwa na mamake ambaye wakati huo alikuwa ameolewa kijijini kwetu. Nilikuwa mentor wake kwa muda mpaka nilipomaliza Rungwe sec. School.

Baadaye nilionana na Kipepe nchini Sweden miaka ya 90 wakati tukiwa wanafunzi Ulaya. Wakati huo alikuwa anasoma Ukraine.

Alikuwa mchekeshaji mzuri sana na furaha kuwa naye karibu.

Alivyorudi TZ alijiunga na umoja wa vijana wa CCM kama mhasibu wao, kazi ambayo aliendelea nayo kwa muda mrefu.

Nawapa pole ndugu na marafiki wote wa marehemu kwa msiba huu. Ni pigo kubwa kwa watu wa Kyela maana alikuwa katika vijana ambao walikuwa wanajishughulisha na maendeleo ya wilaya yetu.
 
Duh, Nilimjua vizuri Kipepe. ALikuwa mcheshi na mpole vilevile. Aliumwa nini? Tunamwombea bwana ampokee. Amen.
 
Man who is born of a woman is few of days and full of trouble. He comes out like a flower and withers.
Rip Samson
 
Duh, Nilimjua vizuri Kipepe. ALikuwa mcheshi na mpole vilevile. Aliumwa nini? Tunamwombea bwana ampokee. Amen.

Alikuwa anasumbuliwa na ini. Michango ilikuwa inachangwa ili apelekwe India kwa matibabu. Nafikiri walichelewa kugundua tatizo lake au yeye alichelewa kuomba msaada.

Ni aibu kweli kwa taifa letu, tuko hoi kweli kwenye huduma za afya.

Jana ndio alihamishiwa Lugalo kutokea Muhimbili.
 
Kipepe kaka yangu na ndugu yangu,nimepata taarifaza kifo chako kwa uchungu mkubwa sana sana.Jambo pekee linalonifariji ni kwamba umeenda ukuiwa na imani kubwa kwa Mugu wetu aliye hai.Baada ya kupata taarifa ya kuugua kwako kwa muda nilifunga safari kuja dar,jumamosi iliopita na nikakuta ukiwa katika maandalizi ya mwisho ya kwenda india....ulikuwa ni mchangamfu na mwenye matumaini makubwa...tuliongea masaa mawili tukiwa pamoja na viongozi mbalimbali na mpendwa mama yako mzazi na familia yako.buriani kakayangu Samson Kipepe.
 
RIP Kipepe. Ni kweli alikuwa mcheshi sana. Pole pia kwa mke wake ambaye pia namfahamu vizuri sana pamoja na familia na ndugu zake especially walipo Dar.
 
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Kifo kingine ambacho pengine kingeweza kuepukwa.
 
Wadau,

.

Nilimpokea Kipepe Rungwe miaka ya 80 baada ya kuombwa na mamake ambaye wakati huo alikuwa ameolewa kijijini kwetu. Nilikuwa mentor wake kwa muda mpaka nilipomaliza Rungwe sec. School.

.

Pole sana kwa ndugu na familia yake Mungu amlaze mahali pema peponi.

Mtanzania, Rungwe mkuu ulikuwa mwaka gani? nilikuwepo pale 87 mpaka 90 wakati ilipokuwa best school in TZ chini ya Dubu.
 
Mkuu Mtanzania,

Sawa sawa tumekusikia, Mungu amlaze pema marehemu na tunawatakia heri huko Kyela ingawa nako kumejaa mafisadi na maopportunists wengi hatari sana kwa taifa letu, ukisoma vizuri hii topic utawaona wako wazii lakini mkiwepo huko kina Mtanzania tunajua kutakuwa na usafi.
 
Wadau,

Hii iacheni kwa muda kabla ya kuipeleka kwenye matangazo.

Kwa masikitiko makubwa nawajulisheni kifo cha Samson Kipepe ambaye alikuwa anafanya kazi umoja wa vijana wa CCM. Kifo kimetokea asubuhi hii pale hospitali ya Lugalo.

Aliwahi kugombea kuwa mwenyekiti wa vijana nafikiri wakati ule Nchimbi anagombea kwa mara ya kwanza. Mwaka 2005 aligombea ubunge wa Kyela pamoja na akina Dr. Mwakyembe na Mwakipesile.

Nilimpokea Kipepe Rungwe miaka ya 80 baada ya kuombwa na mamake ambaye wakati huo alikuwa ameolewa kijijini kwetu. Nilikuwa mentor wake kwa muda mpaka nilipomaliza Rungwe sec. School.

Baadaye nilionana na Kipepe nchini Sweden miaka ya 90 wakati tukiwa wanafunzi Ulaya. Wakati huo alikuwa anasoma Ukraine.

Alikuwa mchekeshaji mzuri sana na furaha kuwa naye karibu.

Alivyorudi TZ alijiunga na umoja wa vijana wa CCM kama mhasibu wao, kazi ambayo aliendelea nayo kwa muda mrefu.

Nawapa pole ndugu na marafiki wote wa marehemu kwa msiba huu. Ni pigo kubwa kwa watu wa Kyela maana alikuwa katika vijana ambao walikuwa wanajishughulisha na maendeleo ya wilaya yetu.

Mtanzania,
Nilikutana na huyu jamaa huko Sweden kijijini kwa mama Korin kwenye kazi za summer mashambani. Ni kweli alikuwa always smilling. Yeye na kundi zima la vijana kutoka Sweden akina Baraka, Issa, Marehemu Madodi S Madodi, Marehemu Chex Mkumbi nk nk. Nilikuja pata habari kuwa yuko umoja wa vijana na ndiyo ilikuwa habari ya mwisho. Too painful kwa kijana active kama yeye kutuacha. Naomba unifikishie rambi rambi zangu kwa ndugu na jamaa wote. Kama walivyosema wengine, Kipepe tangulia mwenzentu na siye twaja. Huyu kweli alikuwa mwenzetu. Mungu ampe mapumziko mema, Amen.
 
mkuu Mtanzania,

Sawa Sawa Tumekusikia, Mungu Amlaze Pema Marehemu Na Tunawatakia Heri Huko Kyela Ingawa Nako Kumejaa Mafisadi Na Maopportunists Wengi Hatari Sana Kwa Taifa Letu, Ukisoma Vizuri Hii Topic Utawaona Wako Wazii Lakini Mkiwepo Huko Kina Mtanzania Tunajua Kutakuwa Na Usafi.
Unajua Wewe Ni Ki Kati Ya Watu Wa Pumbavu Sijapata Kuona Katika Maisha Yangu...hapa Watu Wanatoa Pole Za Msiba Na Kumwaga Mpendwa Wao.wewe Unajifanya Mwanamapinduzi Wa Kupambana Kila Mahali Kibaraka Wa Jm.mila Za Afrika Hatubagui Watu Ktk Misiba Au Kujifanya Wewe Ndiwe Mwanamapindizi Sana Falasi Wewe.
 
Back
Top Bottom