Rugby Union
JF-Expert Member
- Nov 21, 2012
- 402
- 249
Timu ya rugby ya Samoa ya wachezaji saba kila upande imefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Dubai Sevens baada ya kuwafunga New Zealand kwa pointi 26-15 kwenye mchezo wa fainali uliofanyika nchini humo.
Ubingwa huo ni wa kwanza kwa timu hiyo ya Samoa kwenye michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya ndege ya Emirates.
Wawakilishi wenye nguvu toka Afrika, Kenya walifanikiwa kushika nafasi ya tatu baada ya kuwafunga Ufaransa kwa pointi 15-12. Mapema siku hiyo, Kenya walipoteza mchezo dhidi ya New Zealand kwa pointi 27-7 kwenye nusu fainali za michuano hiyo.
Ubingwa huo ni wa kwanza kwa timu hiyo ya Samoa kwenye michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya ndege ya Emirates.
Wawakilishi wenye nguvu toka Afrika, Kenya walifanikiwa kushika nafasi ya tatu baada ya kuwafunga Ufaransa kwa pointi 15-12. Mapema siku hiyo, Kenya walipoteza mchezo dhidi ya New Zealand kwa pointi 27-7 kwenye nusu fainali za michuano hiyo.