Samia Suluhu kuwa mgeni rasmi mechi ya Everton ya nchini Uingereza na Gor Mahia

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,491
54,884
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amekubali ombi la kuwa mgeni rasmi katika mchezo kirafiki kati ya Timu ya Everton ya nchini Uingereza na timu ya Gor Mahia ya Kenya ambayo ilitwaa kombe la michuano ya Sportpesa iliyofayika hapa nchini hivi karibuni.
19059793_1491621414214605_6480530658787981882_n.jpg

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amekubali ombi hilo baada ya Kukutana na kufanya mazungumzo na Watendaji wa Kampuni inayojishughulisha na ubashiri wa michezo ya Sports Betting nchini ambao waliongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji Tarimba Abbas Ikulu- Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amepongeza mipango na mikakati mizuri ya kampuni hiyo ya kutaka kukuza vipaji vya wanamichezo hasa kwa mpira wa miguu kwa Tanzania Bara na Zanzibar na kusema kama malengo hayo yatafikiwa Tanzania itakuwa bora katika mchezo wa mpira wa katika bara la Afrika na Dunia kwa ujumla.

Makamu wa Rais pia amewahakikishia watendaji wa kampuni hiyo kuwa milango ya ofisi yake ipo wazi na pindi wakiwama katika jambo lolote wawasiliane na ofisi yake ili tatizo linalowakabili liweze kutafutiwa ufumbuzi ili lisikwamishe shughuli za kampuni hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa Kampuni ya Sports Betting nchini Tarimba Abbas amemweleza Makamu wa Rais kuwa kampuni hiyo ina malengo makubwa ya kufanya biashara hapa nchini kwa kuzingatia sheria na kanuni za nchini.

Mkurugenzi huyo Tarimba Abbas amesema katika mipango yao wanataka katika kipindi cha miaka Mitatu ijayo kampuni yao iwe ni moja ya kampuni bora nchini katika ulipaji wa kodi kwa Serikali kama wanavyofanya kwa sasa katika Serikali ya Kenya.
 
Mhhh wabongo wanavyopenda vya bure! Watajazana vinandani kucheki mechi kwa 500 badala ya kufurika uwanjani
 
Back
Top Bottom