Samia atakuwa Rais bora kwa kuwa karuhusu kukosolewa

MdogoWenu

JF-Expert Member
Dec 23, 2009
555
915
Wote tumesikia karuhusu na kiukweli kalazimisha watu waikosoe serikali.

Tumeshaona wabunge tena wa CCM wakiwa mbele kuikosoa serikali. Hawa watataka wawazidi CHADEMA na wenzao katika kuikosoa serikali na tayari tumeona wameshaanza.

Wapinzani kama CHADEMA na wenzao nao wataendelea kukosoa huku na kule kama kawaida yao.

Magazeti yote yatafunguliwa na yatakosoa karibu kila leo, yaani MWANAHALISI, MAWIO, TANZANIA DAIMA na mengine. Humu Jamii Forum watu watakosoa kila dakika.

Matokeo yake ni nini? Kitakachotokea ni hiki. Madudu mengi yataiibuliwa kila kukicha na rais atapenda aonekane anashughulikia.

Kimsingi ni kama vile Rais Rais Samia kaitupa kazi ya uchunguzi na upelelezi kwetu na hatakuwa na kazi kubwa ya kuibua madudu kwani wabunge wataibua, magazeti yataibua, mitandao itaibua yaani yatakuwa ni mashindano ya kuibua madudu.

Yeye atafanya kazi moja rahisi sana yaani madudu yakiibuka anayashughulikia. Atawatumbua wahusika na wengine kuwapeleka mahakamani.

Matokeo yake watatumbuliwa ambao hutatarajia watumbuliwe na atakapofanya hivyo itaonekana siyo yeye aliyeanzisha bali ni madudu yaliyoibuliwa na wadau kama wewe na mimi. Hataonekana ana kinyongo au amempania mtu fulani.

Kwa mfano, tuhuma za hela kuibwa Benki Kuu wakati wa ugonjwa wa Rais Magufuli zilianzishwa na Kigogo. Rais Samia alichofanya ni kumuagiza CAG afanye auditing pale kwa transactions za kuanzia January hadi March.

Hivyo lazima madudu yatapatikana na watatumbuliwa wasiogusika na hivyo ndivyo itakuwa staili yake

Hivyo, tutegemee kuwa na rais bora kuliko wanavyodhani wengi.

Viva Samia,

Jamhuri ya Muungano, kazi inaendelea
 
Mpaka sasa hakuna Rais kama Jakaya aliyeruhusu mifumo huru ikiwemo mpaka kuruhusu kumkosoa popote utakapojisikia iwe bungeni, nyumba za ibada, media houses nk.

Lakini bado alionekana si RAIS BORA kwakuwa Uhuru wa kukosoa uliifanya Serikali yake ionekane imejaa ufisadi, wizi, rushwa, watumishi hewa kila kona.

Na mwisho wapinzani wakaanza kumuita ni Rais dhaifu, na wakasema hii nchi ili isonge mbele inahitaji kupata kiongozi mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu, mwenye uthubutu na mzalendo.

'Wenye nchi' walijua taifa linahitaji nini, ndipo July 2015 ndani ya chama tawala wakatuletea mwamba

Rais bora ni yule mwenye uwezo wa kutimiza kwa asilimia kubwa yale yaliyomo ktk Ilani ya Chama chake kwa maslahi mapana ya nchi yake.

Sasa mleta mada ni either hufatilii siasa vizuri kwa kufanya ulinganifu au umekuwa msahaulifu ama umeanza kufatilia siasa hivi karibuni hasa Jpm alipoingia madarakani
 
Rais asipotaka kukosolewa ataishia kuachiwa kila kitu aamue akili yake inavyotaka.

Hili li nchi ni likubwa, rais wa namna hiyo lazima apate maradhi ya moyo na lazima afe na atakapokufa watashangilia mitandaoni na mitaani.

Mpaka sasa hakuna Rais kama Jakaya aliyeruhusu mifumo huru ikiwemo mpaka kuruhusu kumkosoa popote utakapojisikia iwe bungeni, nyumba za ibada, media houses nk....
 
Ajitahidi kufuta baadhi ya majeraha mabaya yaliyoachwa na mtangulizi wake. Hii itambeba sana kwenye uongozi wake. Hata morali ya kufanyakazi itarudi
 
Rais asipotaka kukosolewa ataishia kuachiwa kila kitu aamue akili yake inavyotaka.

Hili li nchi ni likubwa, rais wa namna hiyo lazima apate maradhi ya moyo na lazima afe na atakapokufa watashangilia mitandaoni na mitaani.
Ohooo! Kumbe!! Basi sawa.
 
Wote tumesikia karuhusu na kiukweli kalazimisha watu waikosoe serikali.

Tumeshaona wabunge tena wa CCM wakiwa mbele kuikosoa serikali. Hawa watataka wawazidi CHADEMA na wenzao katika kuikosoa serikali na tayari tumeona wameshaanza....
Tatizo la "wachambuzi" wa Bongo, ongea vizuri mwanzoni. Sifa zote utapewa bila kujali utamalizaje!
 
Back
Top Bottom