Sambaratisheni Mawazo Ya Watanzania Kwanza Kabla ya Kuisambaratisha Chadema

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Kuna watu wana ham kweli ya kuona Chadema kinapotea katika medani ya siasa.

Ninawasikitikia kwa sababu wamechelewa.

Chadema kimeteka akili za Watanzania waliokwenda shule kama CCM kilivyoteka fikra za majuha wa Tanzania.

Kwa mtindo huo huo Chadema kimeteka fikra za wasomi kama CUF kilivyoteka akili za Wapemba.

Wakibeza, wakikejeli, wakitukana, wakikashifu wasomi watajua tu. Wasomi watawapuuza. Watawadharau.

Wanaowaza kukisambaratisha lazima waanze na sisi tunaokiunga mkono kwanza.

Watusambaratishe sisi kwanza kimawazo (sijui wataanzanzia wapi?).

Vinginenvyo kubalini yaishe.

Kwamba Tanzania sasa kuna chama cha kweli cha upinzani.

Chadema.
 
Agreed!

Wangekuwa na akili ya kusambaratisha mawazo ya wa Tz kwanza... wasingeiba ... kura!
 
Kuna watu wana ham kweli ya kuona Chadema kinapotea katika medani ya siasa.

Ninawasikitikia kwa sababu wamechelewa.

Chadema kimeteka akili za Watanzania waliokwenda shule kama CCM kilivyoteka fikra za majuha wa Tanzania. ...
Ndugu, hii kitu haijakaa sawa, mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini nina ndugu, jamaa na marafiki karibia vyama vyote vikubwa vya kisisasa na tunaheshimiana kwa hilo, lakini hii ya kuwaita wale wote wasiokubaliana na kile unacho kiamini wewe kuwa ni majuha si dhani ni jambo la busara. Tujaribu kuwaheshime wengine ili nasi watuheshimu... Siasa si ugomvi wala matusi, basi ni hoja na sera zenye kutekelezeka.
 
Ndugu, hii kitu haijakaa sawa, mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini nina ndugu, jamaa na marafiki karibia vyama vyote vikubwa vya kisisasa na tunaheshimiana kwa hilo, lakini hii ya kuwaita wale wote wasiokubaliana na kile unacho kiamini wewe kuwa ni majuha si dhani ni jambo la busara. Tujaribu kuwaheshime wengine ili nasi watuheshimu... Siasa si ugomvi wala matusi, basi ni hoja na sera zenye kutekelezeka.

kumbe juha ni matusi?

dah. samahani mkuu.

usukumani tunamsemo mmoja: "nzela yahuwa ntongi"

maana yake njia huharibiwa na yule aliye mbele anayewaongoza. (assume mko kwenye msafara halafu kiranja wenu yuko mbele. akitwist kidogo tu lazima na nyie wa nyuma m-twist).

neno juha nililisikia kwa Mh. Jakaya. ndiyo 'ntongi' wetu WaTZ kwa sasa. Tumlamumu yeye?

Kumbe ni matusi?

Au ni matusi ukilitumia upande mwingine (CCM)? Sikujua.
 
Ndugu, hii kitu haijakaa sawa, mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini nina ndugu, jamaa na marafiki karibia vyama vyote vikubwa vya kisisasa na tunaheshimiana kwa hilo, lakini hii ya kuwaita wale wote wasiokubaliana na kile unacho kiamini wewe kuwa ni majuha si dhani ni jambo la busara. Tujaribu kuwaheshime wengine ili nasi watuheshimu... Siasa si ugomvi wala matusi, basi ni hoja na sera zenye kutekelezeka.
Habari ndiyo hiyo watu wanaita wehu majuha wewe hulioni hilo kaanze kwanza kumshauri katibu wako Makamba aache upuuzi wa kuwatukana waazilishi wa taifa hili ndipo uje utuambie hapa nyambaf.
 
kumbe juha ni matusi?

dah. samahani mkuu.

usukumani tunamsemo mmoja: "nzela yahuwa ntongi"

maana yake njia huharibiwa na yule aliye mbele anayewaongoza. (assume mko kwenye msafara halafu kiranja wenu yuko mbele. akitwist kidogo tu lazima na nyie wa nyuma m-twist).

neno juha nililisikia kwa Mh. Jakaya. ndiyo 'ntongi' wetu WaTZ kwa sasa. Tumlamumu yeye?

Kumbe ni matusi?

Au ni matusi ukilitumia upande mwingine (CCM)? Sikujua.
Huyo Kikwete mimi sijawahi kumsikia, ila nimesikia hapa ukiwaita wegine kuwa ni majuha, narudia tena mimi si mshabiki wa chama chochote cha siasa, ila nina ndugu, jamaa na marafiki kwenye vyama vyote hivyo... Suhala la kuwaita wengine kuwaona wengine ni majuha kwa kuwa tu, wana imani tofauti na wewe ni ukosefu wa heshima!
 
Habari ndiyo hiyo watu wanaita wehu majuha wewe hulioni hilo kaanze kwanza kumshauri katibu wako Makamba aache upuuzi wa kuwatukana waazilishi wa taifa hili ndipo uje utuambie hapa nyambaf.
Makamba si katibu wangu, ila ni katibu wa CCM, na bahati ghafi mimi si mshabiki wa siasa na wala si mwanasiasa...! Ahsante sana quinie kwa maneno yako matamu na yalio jaa busara...! Hivi nyambaf ndio kitu gani!?
 
Huyo Kikwete mimi sijawahi kumsikia, ila nimesikia hapa ukiwaita wegine kuwa ni majuha, narudia tena mimi si mshabiki wa chama chochote cha siasa, ila nina ndugu, jamaa na marafiki kwenye vyama vyote hivyo... Suhala la kuwaita wengine kuwaona wengine ni majuha kwa kuwa tu, wana imani tofauti na wewe ni ukosefu wa heshima!
RANGI ya KIJANI=JUHA; so kama wewe sio rangi ya kijani kaa kimya kama ndio basi wewe juha tetetete usiku mzuri kweli leo nimeumaliza vema
 
Ndugu, hii kitu haijakaa sawa, mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini nina ndugu, jamaa na marafiki karibia vyama vyote vikubwa vya kisisasa na tunaheshimiana kwa hilo, lakini hii ya kuwaita wale wote wasiokubaliana na kile unacho kiamini wewe kuwa ni majuha si dhani ni jambo la busara. Tujaribu kuwaheshime wengine ili nasi watuheshimu... Siasa si ugomvi wala matusi, basi ni hoja na sera zenye kutekelezeka.

Nafikiri Jamaa yuko right............
Lugha ya kisiasa tu hiyo
 
Makamba si katibu wangu, ila ni katibu wa CCM, na bahati ghafi mimi si mshabiki wa siasa na wala si mwanasiasa...! Ahsante sana quinie kwa maneno yako matamu na yalio jaa busara...! Hivi nyambaf ndio kitu gani!?

Si shabiki wa siasa.....

Si mwanasiasa................
UNAFUTA NINI JUKWAA LA SIASA ny....fu
 
Ndugu, hii kitu haijakaa sawa, mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini nina ndugu, jamaa na marafiki karibia vyama vyote vikubwa vya kisisasa na tunaheshimiana kwa hilo, lakini hii ya kuwaita wale wote wasiokubaliana na kile unacho kiamini wewe kuwa ni majuha si dhani ni jambo la busara. Tujaribu kuwaheshime wengine ili nasi watuheshimu... Siasa si ugomvi wala matusi, basi ni hoja na sera zenye kutekelezeka.

Bwana asififiwe Mkuu X-Paster, Sidhani kama kama Ng'wanangwa alitumia neno majuha akiwa na kusudi la kutukana watu bali alizingatia mtaji wa CCM. Mtaji wa CCM ni ujinga na umaskini wa Watanzania. Wale walio wajinga totoro ndio kila siku wanaimba CCM, CCM, CCM hata kudai kuwa damu yao ni ya kijani!!! Hata mimi naungana naye kwani Sidhani kama kuna mtu mwenye akili yake na ambaye hafaidi kitu moja kwa moja kutoka CCM au anayeokoteza okoteza chochote kutokana na mfumo wa utawala ambaye anaweza kuiunga mkono CCM. Vinginevyo atakuwa ni maskini anayetegemea kugawiwa Tshirt, kofia na afu tano ili aweze kuishi!!
 
Si shabiki wa siasa.....

Si mwanasiasa................
UNAFUTA NINI JUKWAA LA SIASA ny....fu
Je sina haki ya kuperuzi majukwaa mengine kwa kuwa tu si shabiki wa siasa!? Ni ajabu kweli!
 
Bwana asififiwe Mkuu X-Paster, Sidhani kama kama Ng'wanangwa alitumia neno majuha akiwa na kusudi la kutukana watu bali alizingatia mtaji wa CCM. Mtaji wa CCM ni ujinga na umaskini wa Watanzania. Wale walio wajinga totoro ndio kila siku wanaimba CCM, CCM, CCM hata kudai kuwa damu yao ni ya kijani!!! Hata mimi naungana naye kwani Sidhani kama kuna mtu mwenye akili yake na ambaye hafaidi kitu moja kwa moja kutoka CCM au anayeokoteza okoteza chochote kutokana na mfumo wa utawala ambaye anaweza kuiunga mkono CCM. Vinginevyo atakuwa ni maskini anayetegemea kugawiwa Tshirt, kofia na afu tano ili aweze kuishi!!
Sikubaliani na wewe, kuwa mwanachama wa chama fulani si ujinga bali ni kukubaliana na sera ya kile chama unacho kiunga mkono... Kutukanana na kuitana majina yasio pendeza ni kuingiza chuki zisizo na msingi wowote... Siasa si chuki bali ni sera, lazima watu wakubaliane kuto kukubliana kwa amani na heshima...!
 
Kuna watu wana ham kweli ya kuona Chadema kinapotea katika medani ya siasa.

Ninawasikitikia kwa sababu wamechelewa.

Chadema kimeteka akili za Watanzania waliokwenda shule kama CCM kilivyoteka fikra za majuha wa Tanzania.

Kwa mtindo huo huo Chadema kimeteka fikra za wasomi kama CUF kilivyoteka akili za Wapemba.

Wakibeza, wakikejeli, wakitukana, wakikashifu wasomi watajua tu. Wasomi watawapuuza. Watawadharau.

Wanaowaza kukisambaratisha lazima waanze na sisi tunaokiunga mkono kwanza.

Watusambaratishe sisi kwanza kimawazo (sijui wataanzanzia wapi?).

Vinginenvyo kubalini yaishe.

Kwamba Tanzania sasa kuna chama cha kweli cha upinzani.

Chadema.

Tatizo CCM, CUF, NCCR imebaki kutetea Kikundi cha watu fulani na si kuwatetea wananchi walio wengi.
Tuzidi kuelimisha watu.
Na sasa wamejisahau kuelimisha watu na wanachama wao wamebaki kukinyoshea kidole Chadema.

Na chadema walivyo na akili wanahangaika na shughuli za wananchi.
 
Sikubaliani na wewe, kuwa mwanachama wa chama fulani si ujinga bali ni kukubaliana na sera ya kile chama unacho kiunga mkono... Kutukanana na kuitana majina yasio pendeza ni kuingiza chuki zisizo na msingi wowote... Siasa si chuki bali ni sera, lazima watu wakubaliane kuto kukubliana kwa amani na heshima...!
Ningekupa thanks kama ningesikia wewe huyu huyu unapinga kwanza zile nyimbo za Dr Komba anazowatukana wapinzani na kudai wachinjwe! Na hapo ningekubaliana nawe kuwa siasa si uadui kwani kila mwana CCM hawezi kuzipiga!
 
Ningekupa thanks kama ningesikia wewe huyu huyu unapinga kwanza zile nyimbo za Dr Komba anazowatukana wapinzani na kudai wachinjwe! Na hapo ningekubaliana nawe kuwa siasa si uadui kwani kila mwana CCM hawezi kuzipiga!
Sasa mkuu, nitapinga vipi kitu ambacho sijakisikia...!? Who's Dr. komba any way!?
 
Back
Top Bottom