Samatta, Manula watemwa, Kelvin John arejeshwa Taifa Stars inayoenda kuwavaa Morocco mechi ya kufuzu Kombe la Dunia 2026

Waufukweni

JF-Expert Member
May 16, 2024
2,463
6,919
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kitakachoingia kambini kujiandaa kwa mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Morocco.

1741943371046.png
Kikosi hicho kinajumuisha wachezaji kutoka klabu mbalimbali za ndani na nje ya nchi, wakiongozwa na kocha Hemed Suleiman. Miongoni mwa wachezaji walioteuliwa ni pamoja na;

Ally Salim (Simba SC), Hussein Masaranga (Singida BS), Dickson Job (Young Africans), na Novatus Miroshi (Göztepe FC, Uturuki).

Katika safu ya ushambuliaji, wachezaji kama Simon Msuva (Al-Talaba SC, Iraq), Selemani Mwalimu (Wydad Casablanca, Morocco), na Kelvin John (Aalborg BK, Denmark) wanatarajiwa kuongeza nguvu kwenye kikosi.

Pia, Kiungo wa Simba SC, Yusuph Kagoma ameitwa Taifa Stars kujiandaa na mchezo wa kufuzu kombe la Dunia 2026 dhidi ya Morocco.

1741943072895.png
Hata hivyo, Taifa Stars itamkosa nahodha wake Mbwana Samatta katika mchezo huo muhimu dhidi ya Morocco kutokana na majeraha. Kukosekana kwake ni pigo kwa timu, lakini benchi la ufundi lina matumaini ya kufanya vizuri licha ya changamoto hiyo.

1741941850618.png


 
Kwanini kipa hajaitwa Diara yani hata Aziz ki ameonekana hana nafasi timu ya taifa? Naomba nafasi niwe Rais wa TFF ili niwaokoe ndugu zangu watanzania, laiti kama ningekua Rais wa TFF nisingekubali mchezaji kama Mukwala, Nouma, Aucho na Pacome wasiwepo
 
Kushiriki kombe la Dunia Kwa Tanzania Huwa kama vichekesho.Maana lazima watolewe hatua za awali kabisa.
 
Au Samata ameomba hasiwepo?,maana naona kwenye timu anayo cheza anafanya vizuri.
 
Ni sahihi kabisa kumtoa Samattq. Hajawahi kufanya maajabu kama qnavyokuwa na timu anazochezea. Qtakuwa anaogopa kuumia
 
Mbwana Samata Kwa level alizopo kumuita kuchezea timu kama Taifa Stars ni kumshushia heshima.
 
Hivi Ali Salim na Abutwalib Msheri Nani amecheza mechi nyingi za mashindano msimu huu?
Kwanini wasiitwe kipa toka timu zingine wanaofanya vizuri tofauti na Yanga na Simba?
 
Kwanini kipa hajaitwa Diara yani hata Aziz ki ameonekana hana nafasi timu ya taifa? Naomba nafasi niwe Rais wa TFF ili niwaokoe ndugu zangu watanzania, laiti kama ningekua Rais wa TFF nisingekubali mchezaji kama Mukwala, Nouma, Aucho na Pacome wasiwepo
Asante kwa kutuconfuse 🙏
 
Back
Top Bottom