Madihani
JF-Expert Member
- Apr 30, 2015
- 5,972
- 6,605
SAMAKI AKIMLA MTU NDO HABARI ILA MTU AKILA SAMAKI SI HABARI HIYO.
NA SHITINDI VENANCE
Kesho asubuhi na mapema ninaratiba ya kwenda centro ya hapa kwetu mbeya ili nikawaone waalimu wa shule ya mbeya sekondali walioswekwa lupango kwa kosa la kumpiga mwanafunzi mithili mwizi.
Kiukweli katika hili mm binafsi siungi mkono kipigo cha kikatili kilichotolewa na walimu hawa kwa mwanafunzi haswa kwa sababu dhaifu inayotolewa kuwa hakufanya kzi ya kiingeleza iliyotolewa.
Licha ya ukweli huu bado hatua zilizochukuliwa dhidi ya waalimu hawa zimekuwa ni zakukurupuka mno na kwa kiasi kikubwa hatua zimetolewa kwa msukumo wa watu katika mitandao ya kijamii badala ya kufata taratibu za kiutumishi na haswa ikizingatiwa kuwa hawa ni wanafunzi wa vyuo vikuu na walikuwa katika mafunzo kwa vitendo.
Ukiwa katika mafunzo unakuwa chini ya uangalizi maalumu na nimajukumu ya yule unayekuwa chini yake kukukosoa na kukurekebisha pale unapokwenda ndivyo sivyo.
Kwamaana kuwa vyuo vikuu na wakufunzi ndio walitakiwa kuchukua hatua za kitaaluma dhidi ya wanafunzi hao ikiwemo kurudia mafunzo kwa vitendo.
Lakini cha kushangaza wanaochukua hatua dhidi ya wanafunzi ni waziri wa mambo ya ndani na waziri wa elimu jambo ambalo ni kinyume na utaratibu wa kawaida na wakitaaluma
RAI YANGU
swala hili lisiendeshwe kimihemko na badala yake tufate utaratibu wa kitaaluma ili kuweza kushughulikia suala hili badala ya kutumia mihemko na mashinikizo ya mitandaoni.
Elimu ya juu na vyuo vikuu viwe huru katika maamuzi yake na hatua za kitaaluma ndizo zionekane kutawala katika sakata hili badala ya kuwaachia wanasiasa kufanya siasa katika hili
Tuwape hakiyao ya asili ya kusikilizwa waalimu haw waliohusika na sakata zima haswa wale ambao mpaka sasa wameshapewa kila aina ya hukumu kwani wameshaswekwa ndani na wakati huohuo wameshafukuzwa vyuo hata kabla ya kusikilizwa na bodi za vyuo vyao.
MWISHO
Elimu ni kumpa mtu maarifa ya jambo fulani kama hakuelewa hafungwi wala kufutwa kwenye mfumo wa elimu.
ALIYEMTOA MTU MACHO KAPELEKWA MAHAKAMANI LAKINI MWALIMU ALIYEPIGA VIBAO AMESHAHUKUMIWA TAYALI.
TUNAHITAJI KUJIFUNZA MENGI KUPITIA SWALA HILI.
SHITINDI VENANCE
VOICE OF VOOICELESS
0759704444
NA SHITINDI VENANCE
Kesho asubuhi na mapema ninaratiba ya kwenda centro ya hapa kwetu mbeya ili nikawaone waalimu wa shule ya mbeya sekondali walioswekwa lupango kwa kosa la kumpiga mwanafunzi mithili mwizi.
Kiukweli katika hili mm binafsi siungi mkono kipigo cha kikatili kilichotolewa na walimu hawa kwa mwanafunzi haswa kwa sababu dhaifu inayotolewa kuwa hakufanya kzi ya kiingeleza iliyotolewa.
Licha ya ukweli huu bado hatua zilizochukuliwa dhidi ya waalimu hawa zimekuwa ni zakukurupuka mno na kwa kiasi kikubwa hatua zimetolewa kwa msukumo wa watu katika mitandao ya kijamii badala ya kufata taratibu za kiutumishi na haswa ikizingatiwa kuwa hawa ni wanafunzi wa vyuo vikuu na walikuwa katika mafunzo kwa vitendo.
Ukiwa katika mafunzo unakuwa chini ya uangalizi maalumu na nimajukumu ya yule unayekuwa chini yake kukukosoa na kukurekebisha pale unapokwenda ndivyo sivyo.
Kwamaana kuwa vyuo vikuu na wakufunzi ndio walitakiwa kuchukua hatua za kitaaluma dhidi ya wanafunzi hao ikiwemo kurudia mafunzo kwa vitendo.
Lakini cha kushangaza wanaochukua hatua dhidi ya wanafunzi ni waziri wa mambo ya ndani na waziri wa elimu jambo ambalo ni kinyume na utaratibu wa kawaida na wakitaaluma
RAI YANGU
swala hili lisiendeshwe kimihemko na badala yake tufate utaratibu wa kitaaluma ili kuweza kushughulikia suala hili badala ya kutumia mihemko na mashinikizo ya mitandaoni.
Elimu ya juu na vyuo vikuu viwe huru katika maamuzi yake na hatua za kitaaluma ndizo zionekane kutawala katika sakata hili badala ya kuwaachia wanasiasa kufanya siasa katika hili
Tuwape hakiyao ya asili ya kusikilizwa waalimu haw waliohusika na sakata zima haswa wale ambao mpaka sasa wameshapewa kila aina ya hukumu kwani wameshaswekwa ndani na wakati huohuo wameshafukuzwa vyuo hata kabla ya kusikilizwa na bodi za vyuo vyao.
MWISHO
Elimu ni kumpa mtu maarifa ya jambo fulani kama hakuelewa hafungwi wala kufutwa kwenye mfumo wa elimu.
ALIYEMTOA MTU MACHO KAPELEKWA MAHAKAMANI LAKINI MWALIMU ALIYEPIGA VIBAO AMESHAHUKUMIWA TAYALI.
TUNAHITAJI KUJIFUNZA MENGI KUPITIA SWALA HILI.
SHITINDI VENANCE
VOICE OF VOOICELESS
0759704444