GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,052
- 107,536
Najua kuwa kuna Misiba ya Watu ambao huwa tunawapenda huwa inatuuma na kutugusa sana kwa kila hali hasa kutokana na ule umuhimu Wao Kwetu hasa pale walipokuwa Hai na yale mema ambayo walikuwa wakifanya Kwetu au katika Jamii nzima.
GENTAMYCINE leo nasemea tu Suala moja la Utaratibu hasa wa Watu pale Mwili wa Mpendwa Wao ukiwa unapita. Kuna Msiba Mmoja nauona ambao kwa Ratiba yake iliyokuwepo mpaka hivi sasa Saa 8 Mwili ulitakiwa zamani sana uwe umeshafika ulikokusudiwa kwa ajili ya Kuhifadhiwa ila Ratiba hiyo imeshindikana kutokana na Watu Kuuingilia hali iliyofanya icheleweshe kila Kitu na kusababisha Usumbufu kwa Wafiwa na hata Wageni wengine walioko katika Msafara huo.
Nadhani kungekuwa na utaratibu ' Maalum ' kutoka katika Kamati za hii Misiba kwamba kama wanajua Wapendwa Wao walikuwa wakipendwa mno na Watu basi wangekuwa wanaweka tu Utaratibu fulani wa Miili ya Marehemu hao kuwekwa sehemu moja ili Watu waage kisha ratiba zingine ziendelee na kusiwe na Ucheleweshwaji wowote huko njiani hali ambayo inasababisha Foleni zisizo za lazima kwa Watu wengine ambao nao wanaendelea Kujenga nchi yao kama vile ambavyo hao Marehemu nao waliijenga nchi.
Kwanza ni HATARI sana pale Msiba ukiwa katika Msafara wake mkubwa Kuingiliwa tena na Watu walioko pembeni kwani kunaweza pia kukatokea ' balaa ' la Mtu / Watu ' Kugongwa ' au hata ' Kujeruhiwa ' hivyo ikawa ni kuzidisha tu matatizo kama si usumbufu.
Ila lawama zangu kubwa na nyingi nazipeleka kwa Kamati za Misiba na Ulinzi na Usalama za hiyo Mikoa ambayo Watu hawa Maarufu wanaishi au wanatokea. Kama Ratiba tayari imeshapangwa hakuna tena haja ya Kuiharibu kwasababu tu kuna Watu wamesimama barabarani na wengi Wao wakiwa hadi wanaingia barabarani Kuzuia Gari na kusababisha Ucheleweshwaji wa Mwil kufika kule ambako umekusudiwa na kwa wakati ( muda ) fulani.
Tukumbuke kuwa wenye ' Uchungu ' na Marehemu siyo wale tu waliojipanga Barabarani huku wakiwa wanalia, wamebeba Maua, Majani na Kutandika khanga Barabarani bali pia kuna wale ambao nao wamechukuwa muda Wao wamesafiri umbali mrefu ama kwa Magari au Ndege kuweza Kuusindikiza Mwili ( Marehemu ) hivyo kwa Kiasi fulani nina uhakika kuwa hata Wao ' wanakwazika ' kwa namna moja au nyingine kwa hii ' tabia zoeleka ' ya Kuingilia Misafara ya Mazishi ya Watu Maarufu, Wakubwa na Mashuhuri nchini.
Ni kweli kabisa kwamba hawa Marehemu huwa tunakuwa tunawapenda sana na mno ( kama vile ambavyo hata Mimi GENTAMYCINE ) nawapenda na nawalilia ila ' Concern ' yangu Kubwa tu ni huu ' Utaratibu ' wa Kuingilia Misafara hovyo wakati tayari kuna muda ' Maalum ' unakuwa umeshapangwa kwa Mwili na Waombolezaji kuweza kufika Kijijini ili kupisha ratiba zingine kuweza kuendelea.
Sasa kama leo tu Safari ya Kilometa 39 kutoka Uwanjani KIA hadi Kijijni kwa Marehemu ambayo ilitakiwa ichukue takribani Saa Moja au Mawili tu kwa Msafara huo Kuingiliwa na Watu hovyo na mara kwa mara barabarani sasa umecheleweshwa kwa takribani Masaa 5 kama siyo 6.
Tunaochelewesha hii Misiba humu Barabarani tukumbuke kuwa tunawatesa pia na Wajane, Ndugu, Jamaa na Marafiki wengine waliopo katika Misafara kwa Kuzidi Kuwachosha zaidi njiani na hata kuwazidishia Majonzi japo wanaweza wasiseme ila kimoyomoyo ' wanakwazika ' sana tu. Kuna Watu wapo katika hayo Magari ya Misafara labda wanaumwa au wengine wameshikwa na Haja na kutoka katika Misafara Kwao inakuwa ngumu je hapa kwa Sisi Kuiingilia hovyo na mara kwa mara hii Misafara hatuoni kama tunawapa nao Usumbufu wa kilazima na usiotarajiwa?
Naomba radhi kama kuna nitakaowakwaza kwa huu Uzi wangu ila dhamira yangu GENTAMYCINE ni njema na nzuri tu japo kwa sasa Mtu unaweza usione kwakuwa tu bado tukio zima linaendelea ila kwa Jicho la mbali zaidi nadhani sasa kunahitajika Elimu hasa kwa Watu namna ya Kuikabili Misiba hii mikubwa na ya Watu maarufu ili kutoleta Usumbufu na kusababisha upotezaji mkubwa wa muda na kuharibu Ratiba ambazo huwa tayari zinakuwa zimepangwa kwa Kuzingatia mambo mengi sana.
Tujifunze kuwa Wastaaabu na Kufuata Utaratibu ili tusiwakwaze na wengine.
Nawasilisha.
GENTAMYCINE leo nasemea tu Suala moja la Utaratibu hasa wa Watu pale Mwili wa Mpendwa Wao ukiwa unapita. Kuna Msiba Mmoja nauona ambao kwa Ratiba yake iliyokuwepo mpaka hivi sasa Saa 8 Mwili ulitakiwa zamani sana uwe umeshafika ulikokusudiwa kwa ajili ya Kuhifadhiwa ila Ratiba hiyo imeshindikana kutokana na Watu Kuuingilia hali iliyofanya icheleweshe kila Kitu na kusababisha Usumbufu kwa Wafiwa na hata Wageni wengine walioko katika Msafara huo.
Nadhani kungekuwa na utaratibu ' Maalum ' kutoka katika Kamati za hii Misiba kwamba kama wanajua Wapendwa Wao walikuwa wakipendwa mno na Watu basi wangekuwa wanaweka tu Utaratibu fulani wa Miili ya Marehemu hao kuwekwa sehemu moja ili Watu waage kisha ratiba zingine ziendelee na kusiwe na Ucheleweshwaji wowote huko njiani hali ambayo inasababisha Foleni zisizo za lazima kwa Watu wengine ambao nao wanaendelea Kujenga nchi yao kama vile ambavyo hao Marehemu nao waliijenga nchi.
Kwanza ni HATARI sana pale Msiba ukiwa katika Msafara wake mkubwa Kuingiliwa tena na Watu walioko pembeni kwani kunaweza pia kukatokea ' balaa ' la Mtu / Watu ' Kugongwa ' au hata ' Kujeruhiwa ' hivyo ikawa ni kuzidisha tu matatizo kama si usumbufu.
Ila lawama zangu kubwa na nyingi nazipeleka kwa Kamati za Misiba na Ulinzi na Usalama za hiyo Mikoa ambayo Watu hawa Maarufu wanaishi au wanatokea. Kama Ratiba tayari imeshapangwa hakuna tena haja ya Kuiharibu kwasababu tu kuna Watu wamesimama barabarani na wengi Wao wakiwa hadi wanaingia barabarani Kuzuia Gari na kusababisha Ucheleweshwaji wa Mwil kufika kule ambako umekusudiwa na kwa wakati ( muda ) fulani.
Tukumbuke kuwa wenye ' Uchungu ' na Marehemu siyo wale tu waliojipanga Barabarani huku wakiwa wanalia, wamebeba Maua, Majani na Kutandika khanga Barabarani bali pia kuna wale ambao nao wamechukuwa muda Wao wamesafiri umbali mrefu ama kwa Magari au Ndege kuweza Kuusindikiza Mwili ( Marehemu ) hivyo kwa Kiasi fulani nina uhakika kuwa hata Wao ' wanakwazika ' kwa namna moja au nyingine kwa hii ' tabia zoeleka ' ya Kuingilia Misafara ya Mazishi ya Watu Maarufu, Wakubwa na Mashuhuri nchini.
Ni kweli kabisa kwamba hawa Marehemu huwa tunakuwa tunawapenda sana na mno ( kama vile ambavyo hata Mimi GENTAMYCINE ) nawapenda na nawalilia ila ' Concern ' yangu Kubwa tu ni huu ' Utaratibu ' wa Kuingilia Misafara hovyo wakati tayari kuna muda ' Maalum ' unakuwa umeshapangwa kwa Mwili na Waombolezaji kuweza kufika Kijijini ili kupisha ratiba zingine kuweza kuendelea.
Sasa kama leo tu Safari ya Kilometa 39 kutoka Uwanjani KIA hadi Kijijni kwa Marehemu ambayo ilitakiwa ichukue takribani Saa Moja au Mawili tu kwa Msafara huo Kuingiliwa na Watu hovyo na mara kwa mara barabarani sasa umecheleweshwa kwa takribani Masaa 5 kama siyo 6.
Tunaochelewesha hii Misiba humu Barabarani tukumbuke kuwa tunawatesa pia na Wajane, Ndugu, Jamaa na Marafiki wengine waliopo katika Misafara kwa Kuzidi Kuwachosha zaidi njiani na hata kuwazidishia Majonzi japo wanaweza wasiseme ila kimoyomoyo ' wanakwazika ' sana tu. Kuna Watu wapo katika hayo Magari ya Misafara labda wanaumwa au wengine wameshikwa na Haja na kutoka katika Misafara Kwao inakuwa ngumu je hapa kwa Sisi Kuiingilia hovyo na mara kwa mara hii Misafara hatuoni kama tunawapa nao Usumbufu wa kilazima na usiotarajiwa?
Naomba radhi kama kuna nitakaowakwaza kwa huu Uzi wangu ila dhamira yangu GENTAMYCINE ni njema na nzuri tu japo kwa sasa Mtu unaweza usione kwakuwa tu bado tukio zima linaendelea ila kwa Jicho la mbali zaidi nadhani sasa kunahitajika Elimu hasa kwa Watu namna ya Kuikabili Misiba hii mikubwa na ya Watu maarufu ili kutoleta Usumbufu na kusababisha upotezaji mkubwa wa muda na kuharibu Ratiba ambazo huwa tayari zinakuwa zimepangwa kwa Kuzingatia mambo mengi sana.
Tujifunze kuwa Wastaaabu na Kufuata Utaratibu ili tusiwakwaze na wengine.
Nawasilisha.