Salome Makamba aomba Serikali itumie magari ya "Washawasha" kuwaondoa Wamasai Ngorongoro badala ya kudhibiti Wapinzani

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,779
141,665
1644565868400.png

Mbunge wa viti maalumu, Salome Makamba ameitaka Serikali itumie magari ya Washawasha kuwaondoa Wamasai huko Ngorongoro badala ya kuyatumia kudhibiti Wapinzani.

Makamba amesema yeye ni balozi wa tembo hivyo anaelewa kinachoendelea hifadhini Ngorongoro kiukweli mbuga inaangamia kwa ukorofi wa Wamasai na matajiri kutoka Arusha na nchi jirani.

Mbunge huyo amekuwa wa pili kuitaka serikali itumie nguvu kuondoa Wamasai baada ya yule wa Mtwara mjini kutaka Vifaru vya Jeshi vitumike kuwaondoa.

Chanzo: TBC 2

Maendeleo hayana vyama!
 
Vita Na wamasai Ni ngumu Sana, Kama mnabisha jaribni, mnaweza kukuta Mnaua 80% Na watarudi tena ngorongoro

Kwa nini mambo magumu yote mnafanya kipindi cha Mama? Hakuna malengo Ovu? Yani agombane Na kila kikundi!

Ccm hamuaminiki nyinyi, angalieni hii michezo yenu isiyoeleweka ya kukurupuka maana mnamharibia Mama yenu!
Hivi ule mkondo wa rubby epitia wapi vile
 
Vita Na wamasai Ni ngumu Sana, Kama mnabisha jaribni, mnaweza kukuta Mnaua 80% Na watarudi tena ngorongoro

Kwa nini mambo magumu yote mnafanya kipindi cha Mama? Hakuna malengo Ovu? Yani agombane Na kila kikundi!

Ccm hamuaminiki nyinyi, angalieni hii michezo yenu isiyoeleweka ya kukurupuka maana mnamharibia Mama yenu!
Ameridhia wamuharibie....
She will have to swallow the pills of her carelessness
 
Back
Top Bottom