Salim Kikeke siyo kwa ubaya ila ni ushauri tu, punguza mbwembwe na mikogo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,516
108,791
Kila nilipokuwa nikimtizama hasa anatangaza Taarifa ya Habari ya Runinga ambayo huwa inarushwa na Kituo cha Runinga cha Star tv kila Jumatatu hadi Ijumaa Saa 3 Kamili hadi Saa 3 Unusu nilikuwa nikidhani labda huwa ni bahati mbaya tu lakini kadri ambavyo nazidi ' Kumkodolea ' nimegundua ya kwamba huyu Mtangazaji ameshalewa pongezi / kongole.

Ewe Mtangazaji wa BBC Swahili Salim Kikeke hizi mbwembwe zako zifuatazo huwa unamfanyia nani?

  1. Taarifa ya Habari ikianza tu unaingia kwa mikogo huku ukidundika
  2. Taarifa ya Habari ikianza tu kila mara unatuzungushia zungushia Kalamu kwa mikogo
  3. Taarifa ya Habari ikianza tu ukienda Kukaa unapiga Nne zisizo na maana hadi unaboa
  4. Taarifa ya Habari ikianza tu na ukiwa katikati mara unaanza kujiangalia ulivyovyaa
  5. Taarifa ya Habari ikianza tu kuna muda huwa unaingiza ' mizaha ' isiyo na maana / tija
  6. Taarifa ya Habari ikianza tu huwa unapenda kutaka kuwa ' dominate ' wenzio hadi katika taarifa zao na nadhani huwa ' wanakumaindi ' ila pengine wanakustahi au wanakuogopa
  7. Taarifa ya Habari ikianza tu kuna muda unaonekana ' Kukonyeza ' vimacho vyako sasa Sijui nani kakuambia kuwa wote wanaotizama hiyo News Bulletin yenu ni Wanawake tupu
Salim Kikeke ambaye nilikuwa nikimfahamu wakati akiwa Tanzania akitangaza katika Media aliyokuwepo na hata Salim Kikeke ambaye alikuwa akitangaza alipokuwa chini ya ' Manguli ' akina Mzee Tido Dustan Mhando na Charles Nkwanga Hillary kabla hawajamuachia ' mikoba ' siyo huyu wa leo.

Yaani Mzee Charles Hillary pamoja na ' Uhenga ' wake wote lakini akisoma taarifa ya Habari ya Azam tv anakuvutia na unamwelewa vyema huku ukiwa na hamu ya kuzidi kumtizama akitiririka na akiserereka Kiusomaji wa Habari na akiwa hana hata chembe ya ' Mbwembwe ' na ' Mikogo ' kama ambavyo Wewe ( Salim Kikeke ) unafanya.

Badilika ' Comrade '.

GENTAMYCINE ni kama Bahari ambayo siku zote huwa haikai na uchafu hivyo kama ' utanimaindi ' kwa haya niliyoyadokeza hapa ' Jamvini ' poa lakini najua nimekuwa mmoja wa ' Mashujaa ' wa kuwa tayari kukupa ukweli ambao najua na nina uhakika ukiufanyia Kazi huenda ukaja kuwa bora zaidi.

Na cha Kushangaza kama siyo Kusikitisha hata hao ' Wazungu ' wenyewe wenye hiyo BBC yao wakiwa wanatangaza taarifa zao za Habari huwa hawana ' mbwembwe ' na ' mikogo ' kama yako na bado huwa tunawaelewa sana tu sasa inakuwaje Wewe ' Wakuja ' tu huko ' Mamtoni ' uwe na ' mashauzi ' ya kupitiliza?

Halafu Weekend hii ukitutangazia mpira naomba unipe majibu kwanini huwa unaichukia sana Timu yangu pendwa ya Liverpool? Imekukosea nini? Kuna chochote labda unawadai wana Liverpool labda tujichangishe tukulipe ili uwe unaacha kutunanga / kutusema? Marefarii wa EPL watuchukie na Wewe tena utuchukie hivi Sisi wana Liverpool tutakuwa Wageni wa nani? Mbona huwa ' huzichambi ' Chelsea, Manchester United na Arsenal ambazo Kiuhalisia ndiyo Timu mbovu kuliko hata Liverpool?

Nawasilisha.
 
Shida ni pale mtu unaemfahamu miaka kumi imepita, umemuona tena ila wew unalazimisha awe kama vile ulivyomuona miaka 10 iliyopita
Nadhani si tabia nzuri, mwache aishi maisha yake. Hutaki abadilike kwani unamlipia mshahara au anakulipa kutazama kipindi.
 
Shida ni pale mtu unaemfahamu miaka kumi imepita, umemuona tena ila wew unalazimisha awe kama vile ulivyomuona miaka 10 iliyopita
Nadhani si tabia nzuri, mwache aishi maisha yake. Hutaki abadilike kwani unamlipia mshahara au anakulipa kutazama kipindi.

Naheshimu mawazo yako Mkuu ila ndiyo hivyo tena nimeshampasha na najua amepashika pia.
 

Halafu Weekend hii ukitutangazia mpira naomba unipe majibu kwanini huwa unaichukia sana Timu yangu pendwa ya Liverpool? Imekukosea nini? Kuna chochote labda unawadai wana Liverpool labda tujichangishe tukulipe ili uwe unaacha kutunanga / kutusema? Marefarii wa EPL watuchukie na Wewe tena utuchukie hivi Sisi wana Liverpool tutakuwa Wageni wa nani? Mbona huwa ' huzichambi ' Chelsea, Manchester United na Arsenal ambazo Kiuhalisia ndiyo Timu mbovu kuliko hata Liverpool?

Nawasilisha.

Yeyote anayeichukia Liverpool ujue huyo ni mchawi.
 
Kila nilipokuwa nikimtizama hasa anatangaza Taarifa ya Habari ya Runinga ambayo huwa inarushwa na Kituo cha Runinga cha Star tv kila Jumatatu hadi Ijumaa Saa 3 Kamili hadi Saa 3 Unusu nilikuwa nikidhani labda huwa ni bahati mbaya tu lakini kadri ambavyo nazidi ' Kumkodolea ' nimegundua ya kwamba huyu Mtangazaji ameshalewa pongezi / kongole.

Ewe Mtangazaji wa BBC Swahili Salim Kikeke hizi mbwembwe zako zifuatazo huwa unamfanyia nani?

  1. Taarifa ya Habari ikianza tu unaingia kwa mikogo huku ukidundika
  2. Taarifa ya Habari ikianza tu kila mara unatuzungushia zungushia Kalamu kwa mikogo
  3. Taarifa ya Habari ikianza tu ukienda Kukaa unapiga Nne zisizo na maana hadi unaboa
  4. Taarifa ya Habari ikianza tu na ukiwa katikati mara unaanza kujiangalia ulivyovyaa
  5. Taarifa ya Habari ikianza tu kuna muda huwa unaingiza ' mizaha ' isiyo na maana / tija
  6. Taarifa ya Habari ikianza tu huwa unapenda kutaka kuwa ' dominate ' wenzio hadi katika taarifa zao na nadhani huwa ' wanakumaindi ' ila pengine wanakustahi au wanakuogopa
  7. Taarifa ya Habari ikianza tu kuna muda unaonekana ' Kukonyeza ' vimacho vyako sasa Sijui nani kakuambia kuwa wote wanaotizama hiyo News Bulletin yenu ni Wanawake tupu
Salim Kikeke ambaye nilikuwa nikimfahamu wakati akiwa Tanzania akitangaza katika Media aliyokuwepo na hata Salim Kikeke ambaye alikuwa akitangaza alipokuwa chini ya ' Manguli ' akina Mzee Tido Dustan Mhando na Charles Nkwanga Hillary kabla hawajamuachia ' mikoba ' siyo huyu wa leo.

Yaani Mzee Charles Hillary pamoja na ' Uhenga ' wake wote lakini akisoma taarifa ya Habari ya Azam tv anakuvutia na unamwelewa vyema huku ukiwa na hamu ya kuzidi kumtizama akitiririka na akiserereka Kiusomaji wa Habari na akiwa hana hata chembe ya ' Mbwembwe ' na ' Mikogo ' kama ambavyo Wewe ( Salim Kikeke ) unafanya.

Badilika ' Comrade '.

GENTAMYCINE ni kama Bahari ambayo siku zote huwa haikai na uchafu hivyo kama ' utanimaindi ' kwa haya niliyoyadokeza hapa ' Jamvini ' poa lakini najua nimekuwa mmoja wa ' Mashujaa ' wa kuwa tayari kukupa ukweli ambao najua na nina uhakika ukiufanyia Kazi huenda ukaja kuwa bora zaidi.

Na cha Kushangaza kama siyo Kusikitisha hata hao ' Wazungu ' wenyewe wenye hiyo BBC yao wakiwa wanatangaza taarifa zao za Habari huwa hawana ' mbwembwe ' na ' mikogo ' kama yako na bado huwa tunawaelewa sana tu sasa inakuwaje Wewe ' Wakuja ' tu huko ' Mamtoni ' uwe na ' mashauzi ' ya kupitiliza?

Halafu Weekend hii ukitutangazia mpira naomba unipe majibu kwanini huwa unaichukia sana Timu yangu pendwa ya Liverpool? Imekukosea nini? Kuna chochote labda unawadai wana Liverpool labda tujichangishe tukulipe ili uwe unaacha kutunanga / kutusema? Marefarii wa EPL watuchukie na Wewe tena utuchukie hivi Sisi wana Liverpool tutakuwa Wageni wa nani? Mbona huwa ' huzichambi ' Chelsea, Manchester United na Arsenal ambazo Kiuhalisia ndiyo Timu mbovu kuliko hata Liverpool?

Nawasilisha.
These ndo Tanzanians....ambao wakati unahaha kutaka kufika sehemu wanakucheka ukishatoa wanageuka kuwa washauri wakubwa na mpk matumizi wanataka wakupangie....Roho za Kishetwan!!
 
hayo mengine uliyesema sina interest nayo ila hapo kwa Liverpool FC ndio pamenishtua,hv ni kweli anaichukia LFC?kama ni kweli basi atakuwa hatutendei haki .YOU WILL NEVER WALK ALONE
 
Tusimchukie mtu anapojinafasi kwenye ofisi yake. Umewahi kumsikia Joooji Maratuuuuu??? Sipendi anavyoivuta ilee sauti yake lakini Sam Mahela ndo kaniudhi zaidi. Wako kazini na wayafanyayo ndiyo hunogesha kazi yako mashabiki wakawa wengi. Kikekeeee chapa kazi
 
Hayo ni matatizo ya watu wafupi. Kwa watu wanaomfahamu au waliowahi kukutana ana kwa ana na huyu jamaa Salum Kikeke watanielewa katika hili. Huyo jamaa ni mfupi sana kwa height ya mwanaume wa kawaida. Na ndio maana huwa anapenda kudunda dunda ili nae aonekane. Lakini sidhani kama ana nia mbaya. Kwa sababu asilimia kubwa tunafahamu tabia na mikogo ya hawa jamaa zetu wafupi.
 
Back
Top Bottom