Salamu zangu za eid kwako Hanifa

MO11

JF-Expert Member
Mar 23, 2014
18,857
38,596
Ni mwaka sasa umepita tangu niifute namba yako kwenye simu yangu

Japo juzi juzi umenitafuta ila sio kupitia namba yangu kupitia kwa ndugu yangu habari nikazipata nikamwambia achana nae

Kiukweli baada ya kuniambia kichwa changu hakikukaa sawa ndo nikajua bado upo moyoni mwangu na kichwani ila mikononi mwangu haupo

Nikikumbuka tulivyokuwa pamoja japo kwa kipindi kifupi ulikaa sana moyoni kuliko yeyote yule nilikupenda kweli sijawahi kupenda hivi hata ile nyimbo yetu niliifuta siitaki tena kuisikia picha zako nikafuta ila kukufuta moyoni nimeshindwa nasikitika kwa kweli

Sijui nilipokosea nahisi uliniona mtoto nilipokuwa nakuimpress ndo tatizo

Kwa kweli nilikupigia simu tukaongea nachoshukuru hukuniuliza mimi nani ulinijua japo nimebadili namba kwa ajili yako ila sauti yangu umeikumbuka sijui unawaza nini huko ulipo

Ila nahisi utakuwa unafuraha umempata mwengine labda mrefu kuliko mimi hensam boi na mweupe au labda ana hela kunizidi

Mimi bado nipo vile vile mcheshi as always nikiwa na buku mfukoni nitakupa mia 9 mia iliyobaki nitakudanganya ya kukwangulia vocha

Nilipanga tutazunguka sehemu nyingi ila mpaka nikizipata ukachoka ahadi zangu

Ni mimi uliyeukodi moyo wangu kwa kipini chako puani

Mr H
 
Hanifa wengi ni quiet sluts..
Wapo wachache decent ..
Comment yako imefanya nijiulize nawajua Hanifa wangapi nimegundua sijawahi soma na Hanifa kuanzia mwanzo mpaka mwisho.

Sijawahi kua na Hanifa ninayemjua.

Ila sifa uliyompa Hanifa ni ya wakina Salma.
 
Aahahahahaaa pale mmoja wa ma Legendary wa JF anaposhikwa kunako Mahaba.

Pole mwaya, nakuombea upate Hanifa mwingine mwenye kukukubali vile ulivyo.

Mahaba ukijua kucheza nayo hata ulishwe nini kwenye dimbwi la Mahaba siku dimbwi likikauka hupati shoti 😅😅😅😅.

Hii inawezekana iwapo tuu u mkongwe wa Mahaba 😜.

Eid Mubaraka ⭐️🌙.
 
Aahahahahaaa pale mmoja wa ma Legendary wa JF anaposhikwa kunako Mahaba.

Pole mwaya, nakuombea upate Hanifa mwingine mwenye kukukubali vile ulivyo.

Mahaba ukijua kucheza nayo hata ulishwe nini kwenye dimbwi la Mahaba siku dimbwi likikauka hupati shoti 😅😅😅😅.

Hii inawezekana iwapo tuu u mkongwe wa Mahaba 😜.

Eid Mubaraka ⭐️🌙.
Hata ndege mjanja hunasa kwenye tundu bovu
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom