Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Salaam zangu zikufikie Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Ndg. Nape Nnauye. Salamu hizi zinaambatana na pongezi za dhati kwa ukimya wako uliosaidia kuwepo kwa utulivu katika chaguzi za ndani ya chama zinazoendelea na kuelekea ukingoni kwa ushwari wa kupongezwa. Matarajio yangu ni kuwa Nape utakuwa umetambua kwa kiasi gani matamshi, matamko na mabandiko yako katika mitandao ya kijamii huathiri sana michakato, sura ya chama na huweka sifongo katika siasa za makundi ndani ya chama.
Ni ushauri wangu kuwa chama kijihoji kama kinaweza kukutumia (Nape) katika nafasi nyingine yenye mahitaji ya vipawa na sifa ulizonazo ili kuendeleza utulivu huu. Niweke wazi, ninakufagilia sana Nape kwa jinsi ulivyosimama kuhesabiwa miongoni mwa Watanzania wachache waliomnyooshea Lowassa kidole na kumwambia kuwa "wewe ni FISADI" bila kupiga ukope wala kumung'unya maneno. Na kubwa zaidi katika hili la Lowassa wewe ni kijana wa pekee uliyebaki na msimamo madhubuti bila kuyumba wala kuyumbishwa. Lakini ninatofautiana nawe katika maeneo mbalimbali na kubwa likiwa ni katika tafsiri halisi ya neno na matendo yanayomaanisha UZALENDO wa kweli.
Nakutakia utendaji mwema na wa mafanikio makubwa zaidi katika majukumu yako.
Ni ushauri wangu kuwa chama kijihoji kama kinaweza kukutumia (Nape) katika nafasi nyingine yenye mahitaji ya vipawa na sifa ulizonazo ili kuendeleza utulivu huu. Niweke wazi, ninakufagilia sana Nape kwa jinsi ulivyosimama kuhesabiwa miongoni mwa Watanzania wachache waliomnyooshea Lowassa kidole na kumwambia kuwa "wewe ni FISADI" bila kupiga ukope wala kumung'unya maneno. Na kubwa zaidi katika hili la Lowassa wewe ni kijana wa pekee uliyebaki na msimamo madhubuti bila kuyumba wala kuyumbishwa. Lakini ninatofautiana nawe katika maeneo mbalimbali na kubwa likiwa ni katika tafsiri halisi ya neno na matendo yanayomaanisha UZALENDO wa kweli.
Nakutakia utendaji mwema na wa mafanikio makubwa zaidi katika majukumu yako.