Salamu za pongezi kwa wabunge wateule wa EALA

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,898
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

SALAAM ZA PONGEZI KWA WABUNGE WATEULE WA EALA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinapenda kutoa salaam za pongezi kwa wabunge wateule wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kutoka kundi C, kutokana na nafasi mbili za CHADEMA, waliopatikana leo baada ya uchaguzi uliofanywa na Bunge la Tanzania; Josephine Lamoyan na Pamela Maassay.

Chama kina imani kubwa kuwa wabunge hao wateule wa EALA watakuwa wawakilishi bora wa nchi yetu kwenye bunge hilo wakizingatia manufaa, maslahi na matakwa ya Watanzania na wananchi wa nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Kupitia uwezo, uzoefu na utayari walionao wa kujifunza na kupokea maarifa mapya; Lemoyan na Maassay watabeba matumaini ya MABADILIKO ya Watanzania, ambao wangependa kuona ushirikiano wa EAC unakuwa na nguvu za kiuchumi na kisiasa uliojengwa katika misingi ya kidemokrasia kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi.

Hivyo, chama kinawaahidi ushirikiano wakati wowote watakapohitaji ili waweze kutimiza wajibu na majukumu hayo kwenye uwakilishi wa EALA na EAC kwa ujumla kwa niaba ya nchi yetu.

Imetolewa Jumatano, Mei 10, 2017 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
 
Hii safi, wapeni ushirikiano na watayarisheni wawe wabunge wazuri zaidi Afrika mashariki. Waungwe mkono na wana CDM wote.
 
JAMAN MNISAMEHE; KILIO CHANGU NI SISI WATUMISHI WA WILAYA YA ITILIMA KUCHANGISHWA MCHANGO WA MWENGE 5000 WATU WANAISHIA KUPAUA NYUMBA ZAO KWA MGONGO WA MWENGE MH. MAGUFULI MULIKA HUKU ITILIMA
 
JAMAN MNISAMEHE; KILIO CHANGU NI SISI WATUMISHI WA WILAYA YA ITILIMA KUCHANGISHWA MCHANGO WA MWENGE 5000 WATU WANAISHIA KUPAUA NYUMBA ZAO KWA MGONGO WA MWENGE MH. MAGUFULI MULIKA HUKU ITILIMA

Unachangia katika utaratibu upi kwanza?unaenda mwenyewe kuwapelekea 5000 au wanaikwara kwa lazima kwenye mshahara wako?
Achana na Magufuli kwenye hili suala maana lazima analijua na amelibariki ndio maana wamepata ujasiri wa kuwachangisha ila nawashangaa sana watumishi yaani mpaka leo wana imani na jamaa
 
Makene umeandika huku kijiba cha roho kikibubujikwa na mchozi kama wanavyobubujikwa manyumbu wenzio huku kwenye mitandao ya kijamii????

Any way asante kwa tamko hili maana jinsia ya kike walianza kujihisi kama hawapendwi na chadema kwa kinochoendelea kwenye mitandao, Big up sana.
 
JAMAN MNISAMEHE; KILIO CHANGU NI SISI WATUMISHI WA WILAYA YA ITILIMA KUCHANGISHWA MCHANGO WA MWENGE 5000 WATU WANAISHIA KUPAUA NYUMBA ZAO KWA MGONGO WA MWENGE MH. MAGUFULI MULIKA HUKU ITILIMA
Hiyo unayemshtakia naye kapiga za rambirambi atakusikia kweli?
 
Tuambieni hiyo gender balance iko wapi sasa?Mbona hamkusema uchaguzi urudiwe kwasababu waliochaguliwa wote ni wanawake?

Nyinyi ni wanafiki wakubwa!
ccm ni wanafiki lakini chadema ni wapuuzi..... Kete ilikua ni moja tuu leta watatu basi. Ccm walikua hawana jeuri ya kuteua wote wanawake busara zaidi inapaswa kutumika kuliko ujuaji mwingi.
 
JAMAN MNISAMEHE; KILIO CHANGU NI SISI WATUMISHI WA WILAYA YA ITILIMA KUCHANGISHWA MCHANGO WA MWENGE 5000 WATU WANAISHIA KUPAUA NYUMBA ZAO KWA MGONGO WA MWENGE MH. MAGUFULI MULIKA HUKU ITILIMA
Changia tu hakuna namna
 
Tundu Lisu kila kitu anatishia kwenda mahakamani....

Halafu si alisema atampeleka Makonda mahakamani....?

Bado tu hajaenda?

Walivomshangalia kipindi kile cha uchaguzi wa ki Saccoss chao [TLS] ungedhani ni ujio wa pili wa yesu:D:D
Akili yako imedumazwa na mabox kuli wewe
 
MUNGU wakati mwingine anatuachaniza sana! Yaani anenda kuchukua roho za wale malaika wadogo anatuachia mibunge ya CCM? Kwa nini asiyasubiri yako kwenye caucus anaporomosha jumba lote mara moja?
 
MUNGU wakati mwingine anatuachaniza sana! Yaani anenda kuchukua roho za wale malaika wadogo anatuachia mibunge ya CCM? Kwa nini asiyasubiri yako kwenye caucus anaporomosha jumba lote mara moja?
Unaonaje achukue Leo roho yako? Maana so dhani kama unafaida kwa taifa hili na hiyo roho yako mbaya ya kishetani
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom