Shetani
Member
- Oct 23, 2007
- 30
- 0
Majuzi tumepokea salamu za mshikamano kwenye kongamano la wanafunzi lililoitishwa na CHADEMA kutoka kwa mtu anayejiita M.M. Mwanakijiji. Lakini hatukuambiwa kwamba huyu bwana ni nani na ametuma hizi salamu kama nani. Je, iweje chama cha siasa kiruhusu mtu ambaye wameshindwa kumtambulisha alete salamu za mshikamano. Kwenye hizo salamu za MM Mwanakijiji anawahamasisha wanafunzi waafanye uasi, wagome na mambo mengineyo. Sasa hivi hao wanafunzi ni mafala kiasi gani kwa kupokea ujumbe bubu, ambao aliyeuandika ni kunguru asiyejitambulisha?