Salamu nyingi tunazowasalimia wale tuliopoteana kwa muda huwa zinawaumiza pasipo sisi kujua

Mwanga Lutila

JF-Expert Member
Nov 10, 2016
3,954
12,913
Salamu za kumsalimia mtu na kuanza kumuuliza unafanya kazi gani, umeo/umeolewa au unawatoto wangapi? Nilishaziacha baada ya siku moja kuonana na Classmate ambaye hatujawahi kuonana kwa zaidi ya miaka 10 na nilisikia alishaolewa muda mrefu, nikaanza kumuuliza vip una watoto wangapi sahizi ? Alinijibu kwa huzuni sana "bado sijabarikiwa" niliyaona maumivu moyoni mwake kwa jinsi alivyonijibu.

Nafsi yangu ilinisuta kwanini nimemuuliza?

Ninaandika nimeona mtu anasalimiana hivyo na mwenzie waliopoteana kitambo, swali la una watoto wangapi lilionekana kumuumiza kwa jinsi alivyojibu.

Tukikutana na wenzetu hizi salamu hazna maana.

Zinabakia kuwa maumivu tu na kujiona kama wapo nyuma wamechelewa maisha.
 
Kuna mda wanalazimisha mtu useme uongo. Mtu mnakutana anakuuliza vip sahiv una mishe gan? Unamjibu "bado mambo hayajakaa sawa nipo tu" yeye analazimisha "haa wewe acha uongo we mambo yako yatakuwa sawa sahv hapo unanizuga tu" .mm mtu wa aina hii usishangae nakuacha umesimama pekeako maana naona kama vile hatutaelewana
 
Salaamu zetu nyingi wabongo ni umbea

Iwe mwanaume au mwanamke, unapomsalimia mtu kuna vitu unataka kujua kama amekupita au lah na kama kuna vitu umempita utaanza kufurahi "..kumbe afadhali Mimi.."

Si ajabu kumbe amekudanganya tu.

Ukionesha kutaka kujua yale usiyoyajua hutajua lakini ukionesha kutotaka kujua yale usiyoyajua Utajua tu.
 
KUNA UKWELI KABISA AISEE KWENYE BANDIKO LAKO

Tena ukute mfano yule kipanga darasani yupo tu mtaani halafu wewe uliekuwa average umepata kazi nzuri na una drive ndio ukutane nae aisee uanze kumuuliza hayo maswali daah unaua bendi kihisia sema ndio hivyo anashindwa kukwambia
 
Hii ni kweli kabisa. Kuna muda ukipata katika urafiki bila ya kuonana mnapoteza haki ya kuulizana maswali mengine. Uliza hali ya mtu kuwa anaendeleaje. Mengine tuache aidha muhusika mwenyewe akwambie au kuwa na muendelezo wa kukutana baada ya hapo.
 
Nilikutana na classmate hospital ana mimba kubwa baada tu ya salamu nikamwambia hongeraa mtoto wa ngapi huyo? (Aliolewa miaka mi5 iliyopita so kwa uelewa wangu mdogo nikajua atakua na watoto wengine).

Baada ya lile swali nilimuona kabadilika kawa kama na huzuni, akanijibu 'Huyu ndio wa kwanza'.... nilijiskia vibaya sana na kujuta kwanini nilimuuliza nashukuru tu hakuchukia tukaendelea na story.

Kuna umuhimu wa kupima maneno/maswali yetu kabla hatujayatamka ili tusiumize wenzetu.
 
Umeolewa? Umeoa? Unafanya kazi wapi? Una watoto wangapi? Mbona umekonda? Mbona umenenepa hivyo?wachananeni na hayo maswali jamani yanawaumiza watu

Hahaha kuna ndugu yangu mmoja huyo ni shangazi yangu, siku hizi hata akinipigia simu, sipokeagi simu zake kwa makusudi kabisa, sijui yukoje..kila mwezi akinipigia simu, ataniuliza niko wapi, kazi nilizo-apply zimeendaje, biashara zangu zinaendaje, sasa najiuliza akishajua itamsaidia nini?????? Ni mtu mwema kwangu tangu utoto wangu, sijawahi gombana naye, Najua hata nikimwambia changamoto zangu, cha kunisaidia hana, zaidi ya kunipa maneno ya kujifariji ambayo hayatanisaidia, na Nkimwambia habari zangu najua atazipeleka kwengine, ila Maswali yake yananikeraga kwakweli, Siku hizi ashajua Kabisa namkwepaga ila hajajua sababu ni nini Amehlo Lenie Patra31
 
Hahaha kuna ndugu yangu mmoja huyo ni shangazi yangu, siku hizi hata akinipigia simu, sipokeagi simu zake kwa makusudi kabisa, sijui yukoje..kila mwezi akinipigia simu, ataniuliza niko wapi, kazi nilizo-apply zimeendaje, biashara zangu zinaendaje, sasa najiuliza akishajua itamsaidia nini?????? Ni mtu mwema kwangu tangu utoto wangu, sijawahi gombana naye, Najua hata nikimwambia changamoto zangu, cha kunisaidia hana, zaidi ya kunipa maneno ya kujifariji ambayo hayatanisaidia, na Nkimwambia habari zangu najua atazipeleka kwengine, ila Maswali yake yananikeraga kwakweli, Siku hizi ashajua Kabisa namkwepaga ila hajajua sababu ni nini Amehlo Lenie Patra31
Huyo anaweza kuwa na nia njema ila hayo maswali hapana kwakweli, hata mimi ningemkwepa.
Mtu ambaye anakuuliza mambo yako halafu hana msaada sio wa kumpa info zako, apige anisalimie inatosha.
 
Back
Top Bottom