Kamende
JF-Expert Member
- Mar 1, 2008
- 416
- 45
Ninaandika hoja yangu hii nikiwa makini vya kutosha baada ya kuchuja kwa undani ukweli na chanzo cha matatizo ya nchi yetu kwa leo.
Ninakumbuka kwa kiasi kuwa enzi za siasa ya chama kimoja Tanzania ilikuwa imelemaa kutokana na mfumo wenyewe kwamba isingewezekana hata kidogo kutoa mawazo yanayokinzana na imani, mwelekeo na msimamo wa chama tawala. Kibaya zaidi ingehesabiwa kuwa uhaini endapo ungetofautiana na Mwenyekiti wa chama.
Mwaka 1992 tukatangaza kuingia katika siasa za mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Lengo kubwa likiwa ni kuongeza demokrasia, uwazi na uwajibikaji.
Siasa ya vyama vingi ilimaanishwa kuifanya serikali iliyoko madarakani kuongoza wakiwa makini wakihofia kuwa kosa lolote lingeweza kuwaondoa madarakani. Kwa imani hii yeyote atakayekuwa madarakani atakuwa makini kwa kuhofia kuwa mzaha wowote utamnyima kuendelea kushika dola siku zijazo.
Kwa bahati mbaya sana Tanzania ilipoingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa CCM iliyokuwa madarakani wakati huo iliendelea na mamlaka yake na nguvu zake nyingi ilizokuwa nazo. Wakati vyama vingine vinazaliwa vikiwa vichanga na masikini kabisa viliikuta CCM ikiwa chama kikubwa chenye mtandao nchi nzima, mali nyingi sana na uzoefu mkubwa wa kujikita katika utawala.
Hii ni kusema kwamba Tanzania iliingia kwenye mfumo wa vyama vingi kama kiini macho tu. Serikali iliyokuwa madarakani kwa wakati ule kwanza kwa kutambua na kushangilia ujuzi mdogo wa mambo ya siasa kwa wananchi wake na kwa kutumia mabavu ilipoka demokrasia kwa lengo la kuihakikishia CCM uhakika wa kukaa madarakani milele kutokana na kuweka tofauti kubwa ya kiuwezo baina yake na vyama vingine vya siasa.
Kwa kosa hili sasa haiwezekani kuwalazimisha viongozi kutii kiapo chao cha utii kwa utumishi wao. Wanajua wazi kuwa hali ya kupingwa itaendelea kwa maneno tu na wala hakuna jinsi ambavyo kitatokea chama kingine kikaweza kuitoa CCM madarakani. Hawana hofu ya kuondolewa madarakani kwa nini wawajibike kwa wananchi?
Katika hila zao ili waweze kuiibia nchi wanavyotaka, mafisadi wamefanikiwa kuwekeza kwa nguvu nyingi CCM na kuiimarisha ili ividhoofishe vyama vingine na kubakia yenyewe imara lakini kwa sharti la kutokuzuia wizi wa mafisadi hao.
Sasa tunapozungumzia nguvu ya CCM kuwa kubwa sana dhidi ya vyama vingine tunazungumzia fursa ya wezi (mafisadi) kupora kwa nguvu sana mali za Tanzania.
Kama Tanzania inataka kupona dhidi ya wizi na uporaji unaoendelea leo basi ni lazima turudi kujadili upya na kwa umakini tuone kanuni za kuingia kwenye siasa za vyama vingi vya siasa.
Hata hivyo ni lazima sheria itumike kuifuta CCM kwani kutokana na ulaghai wake wa kujibakizia mali zote ambazo wananchi walivuna kwa pamoja walipokuwa katika mfumo wa chama kimoja cha siasa.
Sababu ya pili ya kuifuta CCM ni kutokana na chama chenyewe kuwa maficho ya mafisadi na ya kwamba haiwezekani kukiachanisha chama hicho na mafisadi.
Sababu ya tatu ya kuifuta CCM ni kuwa kutokana na chama hicho kukubuhu kwa rushwa kwenye kila kitu kinachofanya basi vita ya rushwa haiwezi kufanikiwa nchini. Kwa kuwa tumetangaza kuwa rushwa ni adui mkubwa wa nchi hii na kwa kuwa nguvu kubwa ya CCM inatokana na matumizi makubwa ya rushwa basi njia pekee ya kuinusuru nchi dhidi ya rushwa ni kuifuta CCM.
Sababu ya nne ya kuifuta CCM ni kutokana na kuwafanya watanzania wengi hata vijana kuishi maisha ya kutegemea upendeleo. CCM ni chama ambacho watu hujiunga ili kupata manufaa fulani. Kwa hiyo watu wote wasiopenda kujibidiisha, hujiunga na chama hicho. Sasa ili kuwafanya watanzania hasa vijana kuwa na tabia ya kuwajibika na kujibidiisha basi ni lazima tufyeke kichaka kinachowavutia watu wavivu (CCM)
Sababu ya tano ya kuifuta CCM ni ili kuifanya demokrasia iweze kufanya kazi. CCM ni kikwazo kikubwa cha demokrasia. Kila siku CCM inabuni mbinu za kuvihujumu vyama vingine na kupunguza fursa za watanzania za kukemea uovu. Wanafanya hivyo kwa kutumia nguvu ambazo wanazo tayari. Na kwamba kwa kweli hawaoni aibu hata kidogo kutumia fedha za nchi kuihujumu nchi. Nakiri kuwa CCM haiwezi kuacha hii tabia ya kuhuni. Dawa pekee ni kuifuta.
Zipo sababu zingine nyingi sana za kuifuta CCM, Hatua hii ni ya kizalendo yenye nia ya kuikomboa nchi yetudhidi ya uduni ambao inao na inaendelea kuwa nao kutokana na uwepo wa CCM.
Hapa mtandaoni nawakaribisha sana tujadili hoja hii na kuiboresha, ili kuinusuru nchi yetu. Najua watanzania hatuthubutu kujadili kufutwa kwa CCM. Huu ni mkakati wao mmojawapo pia. Wamewafanya watanzania waamini kuwa maana ya uongozi ni kutawaliwa na CCM. Kumbe huku ndiko kuimaliza nchi yetu.
Hatuwezi kuthubutu kuiondoa CCM madarakani kama hatuthubutu hata kujadili kuifuta kwa makosa ya wazi kabisa ambayo imefanya.
Sitanyamaza: hadi CCM ifutwe!!
Ninakumbuka kwa kiasi kuwa enzi za siasa ya chama kimoja Tanzania ilikuwa imelemaa kutokana na mfumo wenyewe kwamba isingewezekana hata kidogo kutoa mawazo yanayokinzana na imani, mwelekeo na msimamo wa chama tawala. Kibaya zaidi ingehesabiwa kuwa uhaini endapo ungetofautiana na Mwenyekiti wa chama.
Mwaka 1992 tukatangaza kuingia katika siasa za mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Lengo kubwa likiwa ni kuongeza demokrasia, uwazi na uwajibikaji.
Siasa ya vyama vingi ilimaanishwa kuifanya serikali iliyoko madarakani kuongoza wakiwa makini wakihofia kuwa kosa lolote lingeweza kuwaondoa madarakani. Kwa imani hii yeyote atakayekuwa madarakani atakuwa makini kwa kuhofia kuwa mzaha wowote utamnyima kuendelea kushika dola siku zijazo.
Kwa bahati mbaya sana Tanzania ilipoingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa CCM iliyokuwa madarakani wakati huo iliendelea na mamlaka yake na nguvu zake nyingi ilizokuwa nazo. Wakati vyama vingine vinazaliwa vikiwa vichanga na masikini kabisa viliikuta CCM ikiwa chama kikubwa chenye mtandao nchi nzima, mali nyingi sana na uzoefu mkubwa wa kujikita katika utawala.
Hii ni kusema kwamba Tanzania iliingia kwenye mfumo wa vyama vingi kama kiini macho tu. Serikali iliyokuwa madarakani kwa wakati ule kwanza kwa kutambua na kushangilia ujuzi mdogo wa mambo ya siasa kwa wananchi wake na kwa kutumia mabavu ilipoka demokrasia kwa lengo la kuihakikishia CCM uhakika wa kukaa madarakani milele kutokana na kuweka tofauti kubwa ya kiuwezo baina yake na vyama vingine vya siasa.
Kwa kosa hili sasa haiwezekani kuwalazimisha viongozi kutii kiapo chao cha utii kwa utumishi wao. Wanajua wazi kuwa hali ya kupingwa itaendelea kwa maneno tu na wala hakuna jinsi ambavyo kitatokea chama kingine kikaweza kuitoa CCM madarakani. Hawana hofu ya kuondolewa madarakani kwa nini wawajibike kwa wananchi?
Katika hila zao ili waweze kuiibia nchi wanavyotaka, mafisadi wamefanikiwa kuwekeza kwa nguvu nyingi CCM na kuiimarisha ili ividhoofishe vyama vingine na kubakia yenyewe imara lakini kwa sharti la kutokuzuia wizi wa mafisadi hao.
Sasa tunapozungumzia nguvu ya CCM kuwa kubwa sana dhidi ya vyama vingine tunazungumzia fursa ya wezi (mafisadi) kupora kwa nguvu sana mali za Tanzania.
Kama Tanzania inataka kupona dhidi ya wizi na uporaji unaoendelea leo basi ni lazima turudi kujadili upya na kwa umakini tuone kanuni za kuingia kwenye siasa za vyama vingi vya siasa.
Hata hivyo ni lazima sheria itumike kuifuta CCM kwani kutokana na ulaghai wake wa kujibakizia mali zote ambazo wananchi walivuna kwa pamoja walipokuwa katika mfumo wa chama kimoja cha siasa.
Sababu ya pili ya kuifuta CCM ni kutokana na chama chenyewe kuwa maficho ya mafisadi na ya kwamba haiwezekani kukiachanisha chama hicho na mafisadi.
Sababu ya tatu ya kuifuta CCM ni kuwa kutokana na chama hicho kukubuhu kwa rushwa kwenye kila kitu kinachofanya basi vita ya rushwa haiwezi kufanikiwa nchini. Kwa kuwa tumetangaza kuwa rushwa ni adui mkubwa wa nchi hii na kwa kuwa nguvu kubwa ya CCM inatokana na matumizi makubwa ya rushwa basi njia pekee ya kuinusuru nchi dhidi ya rushwa ni kuifuta CCM.
Sababu ya nne ya kuifuta CCM ni kutokana na kuwafanya watanzania wengi hata vijana kuishi maisha ya kutegemea upendeleo. CCM ni chama ambacho watu hujiunga ili kupata manufaa fulani. Kwa hiyo watu wote wasiopenda kujibidiisha, hujiunga na chama hicho. Sasa ili kuwafanya watanzania hasa vijana kuwa na tabia ya kuwajibika na kujibidiisha basi ni lazima tufyeke kichaka kinachowavutia watu wavivu (CCM)
Sababu ya tano ya kuifuta CCM ni ili kuifanya demokrasia iweze kufanya kazi. CCM ni kikwazo kikubwa cha demokrasia. Kila siku CCM inabuni mbinu za kuvihujumu vyama vingine na kupunguza fursa za watanzania za kukemea uovu. Wanafanya hivyo kwa kutumia nguvu ambazo wanazo tayari. Na kwamba kwa kweli hawaoni aibu hata kidogo kutumia fedha za nchi kuihujumu nchi. Nakiri kuwa CCM haiwezi kuacha hii tabia ya kuhuni. Dawa pekee ni kuifuta.
Zipo sababu zingine nyingi sana za kuifuta CCM, Hatua hii ni ya kizalendo yenye nia ya kuikomboa nchi yetudhidi ya uduni ambao inao na inaendelea kuwa nao kutokana na uwepo wa CCM.
Hapa mtandaoni nawakaribisha sana tujadili hoja hii na kuiboresha, ili kuinusuru nchi yetu. Najua watanzania hatuthubutu kujadili kufutwa kwa CCM. Huu ni mkakati wao mmojawapo pia. Wamewafanya watanzania waamini kuwa maana ya uongozi ni kutawaliwa na CCM. Kumbe huku ndiko kuimaliza nchi yetu.
Hatuwezi kuthubutu kuiondoa CCM madarakani kama hatuthubutu hata kujadili kuifuta kwa makosa ya wazi kabisa ambayo imefanya.
Sitanyamaza: hadi CCM ifutwe!!