Salaam kutoka Zanzibar - Hotuba kamili - Msikie SEIF SHARIF HAMAD-Si mchezo

4. Mimi ninavyojuwa – na tunavyoambiwa – ni kwamba Mapinduzi yale yalikuwa ni ya Wazanzibari, kwamba kiongozi wa Mapinduzi alikuwa Mzee Abeid Amani Karume na wenzake kina Said Washoto. Tunaambiwa ni Wazanzibari ndio waliofanya Mapinduzi, au sio? Haya Kikwete ni Mzanzibari? Mimi ninavyojuwa – na Profesa (Lipumba, ambaye ni Mnyamwezi na kimila ni mtani wa Kikwete) – kwamba Kikwete ni Mkwere. Zanzibar haimuhusu shikio wala ndewe. Leo vyereje Kikwete asema: “Tutayalinda Mapinduzi yetu!” Vyereje!?

- Ni wajibu kikatiba kwa rais wa Muungano kuulinda kwa nguvu zake zote kama alivyosema Kikwete hapa hilo sio suala la mjadala, hata Seif alipokuwa Waziri wa CCM, aliapa maneno hayo hayo, again hapa Seif hana hoja ila uchochezi kwa wananchi.
 
Na Mwandishi Wetu
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele​

WAKATI Rais Jakaya Kikwete anajua kwamba Zanzibar kuna mgogoro, hata kama anaupaka rangi na kuuita “mpasuko;” na mgogoro umeleta maafa kisiasa, kiuchumi na kijamii, kauli zake akiwa ziarani Pemba zimepanua ufa.

Rais ameshangaza na hasa amesikitisha kila mpenda amani ya kweli kwa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

BAK, shukrani kwa hili bandiko, ningelinukuu katika post yangu iliyopita, ila nilikuwa naandika, haya ndio nilikuwa nayazungumza. Kama Viongozi walio madarakani wanatoa kauli za ajabu, unataraji nini?. Sasa na wabaguzi wengine wanaibuka kuwa wanatetea WATU WEUSI TU WA ZANZIBAR, ni aibu kubwa!!!!.
 
- Aibu ni kuyazima na kujidai hayapo, wakati yapo na ndio hasa siasa za Seif, ndio maana Kikwete amesema atalinda Muungano kwa nguvu zote, ninakumbuka siku Mwalimu alipofariki, tulikuwa kwenye mkutano na kiongozi mmoja wa Visiwani ambaye sasa ni waziri wa muungano, aliongea maneno siwezi sahau hata siku moja na ndio siku mawazo yangu yalipobadilika kuhusu Zanzibar na siasa zao, infact at onepoint yule mkuu alikuwa akitoa hotuba huku akitoka machozi kumlilia Mwalimu na kwamba wanaofikiri kufa kwake kutawapa mwanya wa kuichukua Zanzibar ni ndoto tupu, toka siku hiyo mkuu sizitizami siasa za huko kama zamani, lakini samahani kama mtizamo wangu haufikii level yako ya kuficha ficha kuwa hayapo, huku Sumaye a former PM akiandika wazi jinsi udini na urangi ulivyotawala uchaguzi wa rais mwaka 2005.

- Tafuta ile article ya "CCM tumekula nyama ya mtu", utayakuta yote ninayosema wazi hapa!

Thanxs!
 
- Aibu ni kuyazima na kujidai hayapo, wakati yapo na ndio hasa siasa za Seif, ndio maana Kikwete amesema atalinda Muungano kwa nguvu zote, ninakumbuka siku Mwalimu alipofariki, tulikuwa kwenye mkutano na kiongozi mmoja wa Visiwani ambaye sasa ni waziri wa muungano, aliongea maneno siwezi sahau hata siku moja na ndio siku mawazo yangu yalipobadilika kuhusu Zanzibar na siasa zao, infact at onepoint yule mkuu alikuwa akitoa hotuba huku akitoka machozi kumlilia Mwalimu na kwamba wanaofikiri kufa kwake kutawapa mwanya wa kuichukua Zanzibar ni ndoto tupu, toka siku hiyo mkuu sizitizami siasa za huko kama zamani, lakini samahani kama mtizamo wangu haufikii level yako ya kuficha ficha kuwa hayapo, huku Sumaye a former PM akiandika wazi jinsi udini na urangi ulivyotawala uchaguzi wa rais mwaka 2005.

- Tafuta ile article ya "CCM tumekula nyama ya mtu", utayakuta yote ninayosema wazi hapa!

Thanxs!

Suala la ubaguzi usilikwepe, kama unaona Seif ni mbaguzi hakukufanyi nawe uwabague watu wa rangi tofauti na Nyeusi Zanzibar, nilikuuliza ukiwamaliza hao wenye rangi tofauti utahamia wapi?. Kwanza ni Nyeusi gani unaizungumzia, ukifananisha mjaluo na mrangi. Ama msukuma na mtu wa Sudan Kusini. hapo tena kutakuwa na matabaka ya weusi.

Kuhusu huyo jamaa aliyozungumza baada ya kufariki Mwalimu, mimi siyajui, labda utuwekee hapa. Manake nitaaminije huyo mtu mmoja, tena kwa kukusikia ukisema alisema, na bila kutuambia alisema nini?. Hata mimi najua yaliyo mabaya Seif aliyafanya nyuma na yana mcost sasa, wakati huo alijipendekeza kwa Mwalimu, sasa yamegeuka. Lakini siwezi fikiria bagua mtu kwa rangi, dini, kabila nk. Unapomzungumzia huyo aliyetoa mada (ambaye sasa ni waziri) na kusema eti alisema wasifikiri kufariki kwa Mwalimu kutawapa mwanya wa kuichukua nchi. Sasa hapo huoni hata enzi ya Mwalimu demokrasia ilikuwa inapindwa, na unakubaliana nami bado kwa hiyo kauli inaonesha kuwa bado watapinda demokrasia. Msiba unahusiana vipi na chaguzi. Huyo Waziri huenda alikuwa hamlilii Mwalimu, bali aliona maslahi ya kuondolewa madarakani yanakaribia. Mh. Sumaye alizungumzia CCM, ina maana CCM ndio inaendekeza udini na urangi. Ukiweza nitumie hiyo article ya Sumaye.

Nakubaliana nawe Rais Kikwete anatakiwa kulinda Muungano, manake kaapa kuulinda. Ila hatakiwi kuulinda kwa mizengwe ama kuua watu. Muungano ni wetu wananchi, tuna haki ya kuujadili, bila kutishwa wala mizengwe.

Naomba"-

-muweke huyo waziri alisema nini ili nasi tupime.
-Jaribu kuwa Muungwana kwa kusema uliteleza kuwabagua Wazanzibar wasio Weusi.
-Jaribu kutofautisha upenzi wa chama (CCM) na maslahi ya nchi, manake kucheza na uchaguzi ni kutafuta matatizo. Na si Zanziba tu, hata Bara.
-Naomba tuache huu mjadala tuangalie hotuba ya Maalim Seif, naona zaidi kama tulitoka nje ya mada, lakini kamautazidi onesha ubaguzi nitaendelea kukuelewesha.
 
there is this Kenyan fella who had the cheek to say that Tanzania one huge BEACH. That we are all a bunch of lazybones and compared to rather hard working Kenyans. I slapped him right away and reminded him about the history of the East African coast all the way from Somalia and well into Kilwa and beyond under the rulers who had MAD eyes. Look into Maalim Seif and the same characteristic is there! No wonder Mzee Mkapa had at one time said, “Tunatoa salamu kwa mababu za hao wapinga Mapinduzi, vijukuu vyao, vitukuu vyao hawatawali hapa.” (salamu za Mkapa katika sherehe za mwaka 2002 za Mapinduzi ya Zanzibar) By the way men with mad eyes is an expression favoured by republicans to describe current Iranian rulers and their likes. To me, the likes of Maalim Sefu are exactly bonafide residents of that hypothetical huge beachland described above. Very PAROCHIAL minded Tanzanians!
 
there is this Kenyan fella who had the cheek to say that Tanzania one huge BEACH. That we are all a bunch of lazybones and compared to rather hard working Kenyans. I slapped him right away and reminded him about the history of the East African coast all the way from Somalia and well into Kilwa and beyond under the rulers who had MAD eyes. Look into Maalim Seif and the same characteristic is there! No wonder Mzee Mkapa had at one time said, “Tunatoa salamu kwa mababu za hao wapinga Mapinduzi, vijukuu vyao, vitukuu vyao hawatawali hapa.” (salamu za Mkapa katika sherehe za mwaka 2002 za Mapinduzi ya Zanzibar) By the way men with mad eyes is an expression favoured by republicans to describe current Iranian rulers and their likes. To me, the likes of Maalim Sefu are exactly bonafide residents of that hypothetical huge beachland described above. Very PAROCHIAL minded Tanzanians!

I guess Mkapa Hakujua kama aliwatukana watu hapo kwa kauli zake za mapinduzi maana asilimia kubwa ya wazanzibari wanaguswa na kauli hiyo including hao CCM kwa zile ndoa zao za kupeana.
 
- Ameanza vizuri, lakini hap[o kwenye kubaka anasema uongo na hana sababu kwani wote tunajua kwua wananchi waliuliwa siku hiyo, lakini ya kubaka ni kuongeza chumvi for what?



- Huyo sasa anazidi kuharibu, maandamano hayakupewa kibali na serikali kwa hiyo yalikuwa ni maandamano haramu, swali ni je serikali ilikuwa right kwenye kuwawua wananchi hao? hapana ilikuwa ni excessive na un-necessary force na linaweza kujadiliwa legally kuhusu makosa ya Mkapa kuruhusu mauaji, lakini Seif hana sababu ya kubadili ukweli kwa sababu ya ku-score cheap na short term popularity ambazo in the long run haziwezi kuwasiadia wananchi wa huko Visiwani, kwa sababu yeye aksiema uongo kama anavyofanya so far kwenye hii hotuba, then anawapa nafasi ya kujibiwa uongo na watawala!

FMES!!

Punguza ushabiki please; ushahidi upo tena ukitaka utapelekwa nyumba hadi nyumba ukawaone/ukawahoji waliobakwa.

Huo ukoko wako uliolishwa na CCM usikudhuru kiasi hicho; turn back ur feelings, hivi lile tukio la 2001 lingekukuta wewe either mama au dada yako angebakwa (achilia mbali kuuliwa) ungekuwa unaongea huo ugoro wako? Kama umefundishwa kuwa mtukanaji mzuri kwa maalim seif hatushangai, maana hata huku Unguja watu kama wewe wapo tena wengi sana. Ila hilo la kudai hakuna aliebakwa ila Maalim au CUF wanatafuta huruma ya jamii ni kuvuka UTU

Thanx
 
FMES!!

Punguza ushabiki please; ushahidi upo tena ukitaka utapelekwa nyumba hadi nyumba ukawaone/ukawahoji waliobakwa.

- Mawazo yangu kwa sababu hayakubaliani na yako inakuwa ni ushabiki,na wako ni ushabiki wa nini mkuu?

Huo ukoko wako uliolishwa na CCM usikudhuru kiasi hicho; turn back ur feelings,

- Wooow! kumbe wewe umelishwa ukoko na Seif na CUF yake ndio maana una mawazo uliyonayo, kwa sababu umedhurika na huo ukoko sasa unafikiri watu wote wengine wamelishwa ukoko kama wewe? Hamuwezi siasa bila vitisho hivi ni kwa nini mkuu?

hivi lile tukio la 2001 lingekukuta wewe either mama au dada yako angebakwa (achilia mbali kuuliwa) ungekuwa unaongea huo ugoro wako? Kama umefundishwa kuwa mtukanaji mzuri kwa maalim seif hatushangai, maana hata huku Unguja watu kama wewe wapo tena wengi sana. Ila hilo la kudai hakuna aliebakwa ila Maalim au CUF wanatafuta huruma ya jamii ni kuvuka UTU Thanx

- Nijuavyo mimi ni kwamba wananchi waliuliwa, lakii ya kubakwa sijawahi kusikia na siamini lakini una haki ya kuweka ushahidi wako hapa bila hapa kunitishia na matusi ya ugoro, ukianza kuleta ugoro maana yake ni moja tu kwamba huna ukweli na hoja yako!

- Seif sikuwa namjua vizuri, lakini kama nilivyokuambia nilipokuwa US kuna kijana wangu mmoja ex-baharia kutoka Boston ndiye aliyekua akimlipia kila kitu na Seif alikuwa akija sana kule ndio nikamfahamu kwa karibu kwa sababu ya ukaribu wangu na yule msela, baada ya muda yule kijana akamkatia kabisa Seif akidai kuwa ni msaliti ana-work for CCM,

- Seif hawezi kumtukana rais wetu na sisi wananchi wa bara bila kujibiwa, akitaka siasa za vitisho wewe na yeye mnajua vizuri, lakini akitaka siasa za kistaraabu atapewa, ila muache vitisho na huu ni wakati muafaka mkamuondoa huyu loser Seif kwenye uongozi maana amepitwa na wakati.

Ahsante Mkuu!
 
-

- Hawawezi kuiba kura Unguja kwa sababu hakuna wa kumpigia kura Seif kule Unguja, huwa wanaiba kura za Pemba tu, ubaguzi upo na ni lazima uemwe wazi, hapa ndicho kinachomsumbua Seif, na hatutampa nafasi kuleta siasa zake za ki-Pemba kwenye Muungano.

Kubali au USIKUBALI ukweli ni kwamba jamaa hakuna sehemu wanakoiba kura kwa wingi kama UNGUJA ushahidi upo; kuna maeneo wao wenyewe wanachama na wapenzi wa CCM ukikaa nao wanshangaa wameshindaje wakati wanajua kuwa hawana chao!!!

CCM kwa wizi wa kura hawawezi kukataa hilo maana kama wanaweza kuibiana ktk chaguzi za ndani ya chama chao watashindwa kuiba kura ktk chaguzi zinazoshirikisha wapinzani?

NIlibahatika kushiriki Uchaguzi mmoja jimbo la Ubungo mwaka 2005 nikiwa ni mwangalizi, katika pitapita zetu mitaani tulifika eneo la Manzese, kuna kituo kimoja kama nakumbuka ni kata ya manzese/midizini. Ilivyokuwa inaonekana ktk kata hiyo kulikuwa na wafuasi wengi wengi sn wa CUF na mazingira yalikuwa yanaonyesha jamaa wanashinda tena kwa kasi ya ajabu sn.

Kuanzia mida ya saa 1 jioni tulianza kushuhudia defender 2 za askari waliovaa kiraia wazungukaaaa badae wakaondoka. Saa 4 ucku matokeo yakatangazwa CUF walishinda kata hiyo but CCM wakagoma na wakaomba hesabu zirudiwe tena, wkt marudio ya hesabu yanaanza umeme ukazimwa eneo lote; kwa bahati watu walikuwa tayari tayari zikaletwa taa za karabai, rechargable na chemli so kazi ikaendelea; nusu saa nyingi zikaja defender km 6 na kuanza kumwaga risasi hewani kama mvua; watu wakasambaratika hadi msimizi wa kituo hakuonekana. Wakaonekana askari waliovaa soksi usoni wakiingiza masanduku ya kuara ktk gari walizokuja nazo na kondoka kwa mbwembwe zote. Alfajiri tukasikia CCM ni washindi!!!

FMES, huo ni ushahidi mdogo tu tena umetokea huko unakosema CUF hawana nguvu - Tanganyika!!! Sasa kama ni huku kwenye wafuasi wa kumwaga unafikiria wanashinda kwa uhalali wa uchaguzi?

Please usitoneshe vidonda kuna watu wana-machungu na mafundo mengi nyoyoni mwao, usiwatoneshe!!!

Thanx
 
Kubali au USIKUBALI ukweli ni kwamba jamaa hakuna sehemu wanakoiba kura kwa wingi kama UNGUJA ushahidi upo; kuna maeneo wao wenyewe wanachama na wapenzi wa CCM ukikaa nao wanshangaa wameshindaje wakati wanajua kuwa hawana chao!!!CCM kwa wizi wa kura hawawezi kukataa hilo maana kama wanaweza kuibiana ktk chaguzi za ndani ya chama chao watashindwa kuiba kura ktk chaguzi zinazoshirikisha wapinzani?

- Mkuu wangu kwanza natoa heshima kwamba sasa unaweza kuandika hoja bila matusi wala vitisho, sio kama ulivyoanza mwanzoni, mimi nimewahi kuona madaftari ya kura ndio nika-conclude kuwa kura huwa zinaibiwa zaidi Pemba, kwa sababu huwa uwiano unazidiana hapo tu, yaani kura chache sana za Pemba, lakini si kweli kwamba ndio ukweli wa mwisho huenda you know better na la kuiba kura huko Visiwani, ninalikubali kwa 100%.

- Ni muhimu mkuu mkaacha siasa za vitisho, rais ni lazima aulinde Muungano kwa njia yoyote ile kama sheria inavyosema, CUF mnahitaji kumuondoa Seif maana hizi siasa zake za ubabe zimepitwa na wakati.

Ahsante Mkuu.
 
1. CUF ilishiriki katika sherehe hizo kama chama na Mkapa aliogopeshwa sana na namna umma wa Kizanzibari wenye sare za CUF na CCM ulivyokusanyika pamoja kwa mara ya mwanzo kwenye sherehe kama hizo).

2. Ebo! Wewe badala ya kufurahi kwamba Wazanzibari kwa umoja wao wanasherehekea Mapinduzi kwa mara ya mwanzo, unakasirika.

3. Jakaya Kikwete, kwa hili kashtushwa sana na mshikamano wa Wazanzibari. Kashtushwa sana na umoja wa Wazanzibari. Wazanzibari sasa hivi wamekuja juu kusema kuwa tutalinda nchi yetu, Zanzibar ni nchi na itabaki kuwa nchi mpaka Kiama. Wazanzibari wameshikamana kulinda rasilimali zao, hasa za mafuta. Sasa Kikwete hili linamuuma sana.

4. Linamuuma sana tu, kwa sababu wao wamo katika kutekeleza mkakati tangu aliouwacha Julius Nyerere kwamba Zanzibar itoweke katika ramani ya dunia.

5. Sasa mshikamano wenu Wazanzibari unawafanya wao wasifanikiwe. Kwa hivyo, alilokuja kufanya Kikwete ni kujaribu kuwagawa tena Wazanzibari kwa kutumia wimbo wa Mapinduzi. Tena, mimi nashukuru Mungu, kasema ‘Mapinduzi yetu,’ katumia wimbo wa Mapinduzi yao. ‘Mapinduzi yao’ si Mapinduzi ya Wazanzibari, jamani. Mujuwe hilo!

6. Kwa hivyo, anataka kutumia wimbo huo atugawe, lakini kachelewa. Kachelewa. Hatugawiki tena ng’o! Tena namwambia Jakaya wa Mrisho wa Kikwete akome, akome, akome! Akome kutuletea fitna katika nchi yetu. Akome, akome kuja kutugawa Wazanzibari. Fanya chokochoko zako huko huko Bara. Namna gani, bwana!?

- Mkuu wangu Aljunior, haya maneno ya Seif lets say ni ya kweli, kwamba wa-Zanzibari ni one thing, sasa kwa nini kuna tatizo na muafaka? Mbona hakubaliani huko mkyamaliza wenyewe na nyinyi mnapendana sana sasa tatizo ni nini kuelewana huko?

- Halafu hivi kweli unaamini kwamba Mwalimu angetaka kuifuta Zanzibar kama anavyosema Seif, ingekuwepo leo kwenye ramani ya Dunia?
 
Wakuu mwalimu wakati anataka kuunganisha nchi za kenya, TZ na Uganda kupata east africa federation ili yeye mwalimu awe permanent represantives wa EAF kule UN,Kenyata na Obote walimwambia ni wazo nzuri sana lakini subiri kwanza tutakujibu,NDIPO akaongea na Mzee karume kwamba tuunganishe nchi zetu wakati tunawasubiri wenzetu,mwalimu akamwambia Mzee Karume sasa ukiona vyema na ukiwa Tayari unanijulisha kwa ili.

Mzee karume akamwambia unamaana gani unaposema nikiwa tayari,nipo tayari sasa hivi ita vyombo vya habari tuwaeleza nia hii nawe utakuwa Rais wa kwanza.


Sasa wakuu siasa za vyama vingi si kuvunja muungano, mema waliofanya wazee wetu lazima tuyalinde kwa nguvu zote bila uCUF wala CCM.

Hotuba kama hiyo ya Seif ni udhaifu wa sera bora ambazo zitawaletea tija na faida wananchi wa ZNZ na Bara pia.

kwa sera na hotuba kama hizo kweli itawachukuaa muda ,maana hata mzee Mwinyi Jana pale TMK kasema bila unazi kuwa vyama vya upinzani bado vina 20% toka 1995 mapka leo na CCM wamebaki na 80% na wataendelea na hizo 20% kama hawatakuwa na sera nzuri mbele ya wanachi.

Muungano lazima tuulinde kwa nguvu zote kwani unafaida nyingi sana kwa taifa letu la TZ kuliko hasara wanazo ziona wanaCUF.

2010 IMEKARIBIA ,twende na sera bora kwa wananchi vingivevyo kwa sera bora na nzuri za CCM basi wataendelea kupata 2010.

na kwa sheria hii mpya ya vyama vya siasa na uchaguzi njia nyeupe kwa chama tawala.


nadi sera na si matusi vijemba, uchochezi utakapelekea kuligawa taifa ki rangi kiudini,kikabila.

watanzani hatuko tayari kupokea sera za namna hiyo, tumezoea amani,upendo, kuheshimiana na uzalendo.

sera za namna hiyo watanzania tutaamua kwa votes zetu chama kipi kina sera bora kwa maendeleo ya taifa na raia wake.

Wabongo si wajinga tena kama mnavyodhania-


tutalinda muungano kwa nguvu zote kwa kuwa unafaida nyingi na serikali ya ccm haiko tayari kuruhu mtu binafsi,taasisi kwa makusudi na interest zake kuuchezea muungano wetu.
 
1. Hotuba kama hiyo ya Seif ni udhaifu wa sera bora ambazo zitawaletea tija na faida wananchi wa ZNZ na Bara pia.

2. kwa sera na hotuba kama hizo kweli itawachukuaa muda ,maana hata mzee Mwinyi Jana pale TMK kasema bila unazi kuwa vyama vya upinzani bado vina 20% toka 1995 mapka leo na CCM wamebaki na 80% na wataendelea na hizo 20% kama hawatakuwa na sera nzuri mbele ya wanachi.

3. Muungano lazima tuulinde kwa nguvu zote kwani unafaida nyingi sana kwa taifa letu la TZ kuliko hasara wanazo ziona wanaCUF.

- Mkuu maneno mazito sana haya na tupo pamoja hapa.
 
Naamini sii msimamo wa Wazanzibari wote ..ni wakina Seif na baadhi ya wanachama wa CUF...na mawazo kama haya basi Seif hawezi kuaminika kuiongoza Zenj!

Mbona Bara Wazanzibari wapo wengi tu wanapeta na biashara zao? Kariakoo na juzi nilikutana nao Mbarali-Mbeya wakifanya biashara ya mchele kule?

I wish to reserve my commenton your posting.
 
- Mkuu wangu kumbe ulikuwa hujui hilo? Kwamba anayetengenezewa njia ya utawala na Seif ni huyo kjana Sultan aliyeko London? Ukienda kwenye archives za JF utakuta tumewahi kuyajadili sana hapa infact kuna topic moja hata picha yake huyo Sultan iliwekwa hapa, Ndio maana tunaomjua vizuri Seif huwa hatumtiliii maanani sana maana tunajua nia yake, hayo maneno hawezi kuyasema akiwa Mbeya, ndio maana anakimbilia kuyasenma Visiwani siku zote, akiwa Bara anakuwa kimyaaa.

Inasikitisha karne hii mtu kuwa na mawazo haya. Inawezekana mtu mwenye elimu yake akazidiwa na utashi tu na labda mzee umepatwa na hilo. Kuamini kuwa Wazanzibari kutaka kuiondoa CCM lengo ni kurejesha usultani ni mambo ya karne iliyopita na huku Bara tunakotaka kuiondosha CCM tunataka kumrejesha Malkia? Tu watu wazima na wenye fikra tuache kuburuzwa na hisia zetu kwani tunapata elimu ili tuvitawale vitu kama hivi.
 
- Ni wajibu kikatiba kwa rais wa Muungano kuulinda kwa nguvu zake zote kama alivyosema Kikwete hapa hilo sio suala la mjadala, hata Seif alipokuwa Waziri wa CCM, aliapa maneno hayo hayo, again hapa Seif hana hoja ila uchochezi kwa wananchi.

Kuulinda nini mzee mfarakano wa Wazanzibari au nini, samahani sijakuelewa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom