Peter Madukwa
JF-Expert Member
- Sep 20, 2012
- 3,134
- 2,465
Salaam;
Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mh Amos Makalla ametoa maagizo ya kuwataka wamachinga waliopanga bidhaa zao barabarani kuondoka mara moja katika maeneo hayo.
Maagizo haya yametokana na mgogoro uliopo kati ya wafanyabishara rasmi waliopanga katika maduka dhidi ya wamachinga wanaopanga bidhaa mbele ya maduka na katika barabara kwa kile kinachoelezwa kuwa wafanyabiashara rasmi kukosa soko huku wakilipa kodi lukuki kulinganisha na wamachinga ambao hulipa 20000 tu kwa mwaka.
Aidha agizo hilo linatokana na ukweli kuwa wamachinga wanaopanga bidhaa barabarani wanaleta usumbufu ktk usafiri kwa sababu barabara zinakuwa hazipitiki kutokana na wao kuzibana barabara kwa kupanga bidhaa ktk barabara.
Kimsingi wafanyabiashara waliopanga ktk maduka wanayo haki ya kulalamika kwa sababu
1. Wanafanya biashara rasmi kwa mujibu wa sheria
2. Wanalipa kodi ya mapato
3. Wanalipia leseni ya biashara
4. Wanalipa gharama ya kodi ya jengo na ushuru wa huduma na gharama zingine kedekede
5. Mauzo yao yanaporomoka na hivyo wanakuwa ktk wakati mgumu na hata kupunguza mapato ambayo serikali ingeweza kukusanya.
Kwa mtizamo wangu kutokana na utata wa jambo hili serikali ichukue hatua zifuatazo
1. Wafanyabiashara rasmi walindwe maslahi yao kwa kuwa wao ndiyo hulipa kodi nyingi kwa serikali na kwamba wanafanya biashara kwa mujibu wa sheria.
2. Wamachinga waondolewe mara moja na kama serikali ina nia ya kuwalinda wamachinga basi wawatengee eneo lao katikati ya mji wawajengee vbanda vyao vidogovidogo wawapangishe na walipe kodi
3. Wakati serikali inaendelea kuwabeba wamachinga iwape muda wa kufanya biashara isiyo rasmi na kuwasisitiza kurasimisha biashara zao na umachinga isichukuliwe kama jambo la kudumu kwa kuwa serikali inapoteza mapato mengi kupitia informal business. (Serikali isimamie sheria na ikibidi hata kwa kulazimisha watu kuhama kutoka ktk machinga kwenda ktk mfumo rasmi wa kibishara)
4. Serikali itenge maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo na miundombinu ijengwe (inaweza kuwa vibanda vidogovidogo ila vya kisasa na siyo mfumo wa ghorofa kama machinga complex). Katika utekelezaji wa jambo hili serikali ni vema ikashirikisha wadau mbalimbali kabla ya utekelezaji ili kukwepa kufeli kama ilivyofeli machinga complex. Serikali ijenge vibanda hivyo katika maeneo yanayozunguka masoko makubwa kama kariakoo, Tegeta, mbagala, gongolamboto, temeke, kimara, mbezi, ubungo, mwenge n.k. aidha wafanyabiashara wadogo ni lazima wawe na leseni ya biashara na walipe kodi lakini gharama ya kupangisha ktk vibanda vyao angalau iwe nafuu. Hili lisiwe jambo la hiyari; kurasimisha biashara iwe jambo la lazima; asiyeweza kufanya biashara rasmj akatafute shughuli ya kufanya.
5. SERIKALI iboreshe mazingira ya kibiashara mikoani na kuimarisha sekta zingine kama kilimo, uvuvi, madini n.k ili kupunguza kasi ya vijana wanaohamia mjini Dsm na ktk majiji mengine.
FAIDA YA KURASIMISHA BIASHARA
1. Itapunguza mgogoro kati ya wafanyabiashara rasmi na machinga
2. Itarahisisha ukusanyaji mapato
3. Itakuwa rahisi kuwa na takwimu halisi za wafanyabiashara kuanzia ngazi ya kitongoji hadi kitaifa
4. Itakuza uchumi wetu na kuboresha miundombinu
5. Itakuwa ni rahisi kwa serikali kuboresha huduma za kijamii
6. Kuokoa muda katika jiji la Dsm unaotokana na msongamano usio wa lazima
7. Majiji yetu yatakuwa safi na katika mpangilio unaovutia
8. Taasisi za kifedha itakuwa rahisi kuwafikia wafanyabiashara ikiwemo katika mikopo
Nasisitiza kuwa; linapokuja suala la serikali kufanya maamuzi iwalinde zaidi wale wanaofanya biashara rasmi kwa kuwa ndiyo wanaolipa kodi na stahili mbalimbali kwa mujibu wa sheria.
Kwa hiyo naunga mkono suala la serikali kuwaondoa wamachinga kwa namna yoyote ile na kwamba umachinga usichukuliwe kama mfumo rasmi na wa kudumu wa kibiashara ni lazima tubadilike ili serikali ikusanye mapato kwa uhakika na kila mwananchi awajibike kwa nafasi yake.
Kwa ujumla maamuzi yasiegamie ktk maslahi ya kisiasa bali yaegamie ktk maslahi ya kiuchumi ya nchi yetu ili tuweze kuwa na taifa linalojiendesha ktk misingi ya haki na sheria, nidhamu na uwajibikaji.
Tukumbuke kuwa kila mwananchi ajue ana wajibu wa kulipa kodi stahili ili tuweze kujenga nchi yetu.
Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mh Amos Makalla ametoa maagizo ya kuwataka wamachinga waliopanga bidhaa zao barabarani kuondoka mara moja katika maeneo hayo.
Maagizo haya yametokana na mgogoro uliopo kati ya wafanyabishara rasmi waliopanga katika maduka dhidi ya wamachinga wanaopanga bidhaa mbele ya maduka na katika barabara kwa kile kinachoelezwa kuwa wafanyabiashara rasmi kukosa soko huku wakilipa kodi lukuki kulinganisha na wamachinga ambao hulipa 20000 tu kwa mwaka.
Aidha agizo hilo linatokana na ukweli kuwa wamachinga wanaopanga bidhaa barabarani wanaleta usumbufu ktk usafiri kwa sababu barabara zinakuwa hazipitiki kutokana na wao kuzibana barabara kwa kupanga bidhaa ktk barabara.
Kimsingi wafanyabiashara waliopanga ktk maduka wanayo haki ya kulalamika kwa sababu
1. Wanafanya biashara rasmi kwa mujibu wa sheria
2. Wanalipa kodi ya mapato
3. Wanalipia leseni ya biashara
4. Wanalipa gharama ya kodi ya jengo na ushuru wa huduma na gharama zingine kedekede
5. Mauzo yao yanaporomoka na hivyo wanakuwa ktk wakati mgumu na hata kupunguza mapato ambayo serikali ingeweza kukusanya.
Kwa mtizamo wangu kutokana na utata wa jambo hili serikali ichukue hatua zifuatazo
1. Wafanyabiashara rasmi walindwe maslahi yao kwa kuwa wao ndiyo hulipa kodi nyingi kwa serikali na kwamba wanafanya biashara kwa mujibu wa sheria.
2. Wamachinga waondolewe mara moja na kama serikali ina nia ya kuwalinda wamachinga basi wawatengee eneo lao katikati ya mji wawajengee vbanda vyao vidogovidogo wawapangishe na walipe kodi
3. Wakati serikali inaendelea kuwabeba wamachinga iwape muda wa kufanya biashara isiyo rasmi na kuwasisitiza kurasimisha biashara zao na umachinga isichukuliwe kama jambo la kudumu kwa kuwa serikali inapoteza mapato mengi kupitia informal business. (Serikali isimamie sheria na ikibidi hata kwa kulazimisha watu kuhama kutoka ktk machinga kwenda ktk mfumo rasmi wa kibishara)
4. Serikali itenge maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo na miundombinu ijengwe (inaweza kuwa vibanda vidogovidogo ila vya kisasa na siyo mfumo wa ghorofa kama machinga complex). Katika utekelezaji wa jambo hili serikali ni vema ikashirikisha wadau mbalimbali kabla ya utekelezaji ili kukwepa kufeli kama ilivyofeli machinga complex. Serikali ijenge vibanda hivyo katika maeneo yanayozunguka masoko makubwa kama kariakoo, Tegeta, mbagala, gongolamboto, temeke, kimara, mbezi, ubungo, mwenge n.k. aidha wafanyabiashara wadogo ni lazima wawe na leseni ya biashara na walipe kodi lakini gharama ya kupangisha ktk vibanda vyao angalau iwe nafuu. Hili lisiwe jambo la hiyari; kurasimisha biashara iwe jambo la lazima; asiyeweza kufanya biashara rasmj akatafute shughuli ya kufanya.
5. SERIKALI iboreshe mazingira ya kibiashara mikoani na kuimarisha sekta zingine kama kilimo, uvuvi, madini n.k ili kupunguza kasi ya vijana wanaohamia mjini Dsm na ktk majiji mengine.
FAIDA YA KURASIMISHA BIASHARA
1. Itapunguza mgogoro kati ya wafanyabiashara rasmi na machinga
2. Itarahisisha ukusanyaji mapato
3. Itakuwa rahisi kuwa na takwimu halisi za wafanyabiashara kuanzia ngazi ya kitongoji hadi kitaifa
4. Itakuza uchumi wetu na kuboresha miundombinu
5. Itakuwa ni rahisi kwa serikali kuboresha huduma za kijamii
6. Kuokoa muda katika jiji la Dsm unaotokana na msongamano usio wa lazima
7. Majiji yetu yatakuwa safi na katika mpangilio unaovutia
8. Taasisi za kifedha itakuwa rahisi kuwafikia wafanyabiashara ikiwemo katika mikopo
Nasisitiza kuwa; linapokuja suala la serikali kufanya maamuzi iwalinde zaidi wale wanaofanya biashara rasmi kwa kuwa ndiyo wanaolipa kodi na stahili mbalimbali kwa mujibu wa sheria.
Kwa hiyo naunga mkono suala la serikali kuwaondoa wamachinga kwa namna yoyote ile na kwamba umachinga usichukuliwe kama mfumo rasmi na wa kudumu wa kibiashara ni lazima tubadilike ili serikali ikusanye mapato kwa uhakika na kila mwananchi awajibike kwa nafasi yake.
Kwa ujumla maamuzi yasiegamie ktk maslahi ya kisiasa bali yaegamie ktk maslahi ya kiuchumi ya nchi yetu ili tuweze kuwa na taifa linalojiendesha ktk misingi ya haki na sheria, nidhamu na uwajibikaji.
Tukumbuke kuwa kila mwananchi ajue ana wajibu wa kulipa kodi stahili ili tuweze kujenga nchi yetu.